Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa fursa hii lakini awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu Rahimu ambaye amepitisha mjadala huu katika hali nzuri na usimamizi wako mzuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na wenzangu kushukuru sana kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Niwapongeze pia watoa hoja wenyeviti wote wawili ambao yaani Mwenyekiti wa bajeti na mwenyekiti wa PAC ambao wamewasilisha ripoti zao hapa au taarifa zao ziko vizuri niwapongeze sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kupunguza mzigo kwa wananchi wake wa Tanzania, dhamira hiyo inaendelea katika kuonekana utekelezaji wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hasa katika suala ambalo hoja imezungumzwa ama maoni yametolewa na kamati ya bajeti kuhusu riba. Naomba niongelee hapo kwamba Serikali inachukua hatua mbalimbali katika kupunguza mzigo kwa wananchi wake hasa wale wakopaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuagiza sekta ya bank na taasisi ya fedha kuweka mikakati ya kupunguza gharama za uendeshaji ikiwemo kuhamasisha matumizi ya teknolojia katika kutoa huduma za fedha kwa lengo la kupunguzia mzigo mteja na kuhakikisha viwango vya riba vinashuka kufikia tarakimu moja tu yaani single digit.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kupitia benki kuu inatoa taaluma kwa wateja mbalimbali au kwa wananchi mbalimbali ili kududi wawe na maamuzi sahihi wakati wa kuingia katika mikopo hiyo. Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kutatua changamoto na miongoni mwa hatua hizo mwezi Julai, 2021 hatua kadhaa zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kutoa unafuu wa kisheria katika kiasi cha amana ambacho bank na taasisi ya fedha zinatakiwa kuweka benki.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili kurekebisha kauli za usajili wakala wa benki kwa kuondoa sharti la kuwa na uzoefu wa miezi 18 katika eneo la biashara, jambo la tatu kupunguza kiwango cha riba kinachotolewa kinachotolewa katika account za wateja watoa huduma za fedha kwa njia za simu za mkononi. Lakini benki imechukua hatua ya kuhakikisha benki kuu imeanzisha mfuko maalum wa shilingi trioni moja kwa riba ya asilimia 3 kwa mwaka. Benki Kuu imepunguza kiwango cha mtaji kinachotakiwa kuweka na benki za biashara kwa ajili ya kuweza kutoa mikopo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhakikisha kuwa uwiano wa gharama za uwendeshaji na mapato ya benki kuzidi asilimia 55 na mikopo chechefu isiyozidi asilimia 5, kushirikiana na umoja wa mabenki katika kusimamia maadili ya watendaji, kushirikiana mabenki pamoja na taasisi ya fedha, kufanya ukaguzi maalumu kwa wastaafu yote haya ni matarajio yetu kwa muendelezo huo zote hizi zitasaidia kuendelea kupungua kwa riba za mikopo nchini. Hivi karibuni tumeshuhudia benki kubwa za kibiashara zikipunguza riba kutoka asilimia 20 hadi asilimia 9 katika sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu pendekezo la kuanzisha Ofisi ya kupokea malalamiko ya kodi mapendekezo haya pia tumeyachukua kwa sababu pendekezo la muundo wa Taasisi ya kanuni za uwendeshaji zimeandaliwa tayari na zimekwisha andaliwa na kupelekwa kwa ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala bora kwa evening, tunatarajia hivi karibu kabla ya kumalizika mwaka huu wa fedha itakuwa idhini hiyo tumeshaipa na muundo utaanza kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nijielekeze katika hoja ya pili ambayo imetokewa na Kamati ya PIC ambayo inazungumzia miradi kutokamilika kwa wakati. Serikali inatekeleza bajeti kama ilivyoidhinishwa na Bunge hadi kufikia mwezi Disemba, 2021 kiasi cha shilingi bilioni 585.1 zimetolea kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo sawa na asilimia 86.2 ya lengo nunu mwaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za maendeleo zilizotolewa zinajumuisha shilingi bilioni 5194.3 na fedha za ndani ni shilingi bilioni 167.1 fedha za nje. Aidha shilingi bilioni 443.7 ni fedha za washirika wa maendeleo zilizopelekwa moja kwa moja ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)