Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, kwa sababu ya ufinyu wa muda nianze kwa kukupongeza wewe kwa kupata nafasi ya kuwa Naibu Spika wetu, lakini nichukue nafasi hii poa kumpongeza sana Jirani yangu, dada yangu, Spika, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson Mwansasu kwa nafasi hii ambayo ameteuliwa kuliongoza Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwanza kwa kumpongeza pia Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa inayoendelea hapa nchini; kwenye miundombinu, afya, kwa kweli mimi binafsi ninaridhika kabisa kwamba kazi inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 8(1) (a) inasema;Lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi. Hapa inamaana kazi kubwa ya Serikali ni kuhakikisha kwamba wananchi wake wanaustawi katika afya, katika uchumi, katika miundombinu, katika elimu na mambo mengine yote. Ni kazi ya Serikali nadhani nizungumzie suala moja juu ya uwezeshaji wa wazawa kiuchumi katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nazungumza hili kwa sababu sisi tulioko hapa ndani tumebahatika kuwa Wabunge, tumebahatika kuwa na Maisha tulioyonayo lakini wako watu wenzetu wengi sana huko nje bado wanaishi Maisha duni na kwenye umasikini mkubwa. Bajeti ya Taifa letu kwa mwaka ni tirioni 34.88 najiuliza swali kila siku, tirioni 34.88 ngapi zimerudi kwa wananchi na ngapi zinaenda nje ya nchi yetu. Nimesimama hapa kuzungumza kwa niaba ya watanzania wazawa na ninaposema wazawa simaanishi rangi namaanisha watu wenye asili ya Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, watanzania wanatakiwa wanastahili kunufaika kabisa na fedha hizi tirioni 34.8 inakuwaje fedha hizi sehemu kubwa zinaenda nje ya nchi badala ya kuwasaidia wazawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kwa sababu Bunge lako tukufu mwaka 1994 lilitunga Sheria ya uwezeshaji wazawa kiuchumi na ilisainiwa na Marehemu Rais Benjamini William Mkapa tarehe 19 Januari, 2005 ya kwamba nchi hii itawawezesha wazawa weweze kushikilia vyanzo vya uchumi vya nchi yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa leo ninaposimama hapa bajeti ya miundombinu ya Taifa hili ni tirion 3 nataka nijiulize tirioni 3 hizi za kutengeneza barabara ya miundombinu gapi zinabaki kwa watanzania bajeti hii ya miundombinu peke yake ni trioni 3 ni ngapi zinabaki kwetu sisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania wengi wanaendelea masikini mabilionea ni wale wale toka miaka ile na wajibu wa Serikali ni ustawi wa wananchi wake. Napenda kuona wazawa wengi wanafanikiwa kiuchumi katika Taifa hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani na sitaki kutaja nchi yoyote kama alivyozungumza Rafiki yangu Mpina haiwezekani tirioni 3 za barabara fedha inayoenda kwa wazawa ni asilimia 20 peke yake nyingi zinaenda kwa wageni wanaokuja hapa na magegi peke yake baada ya miaka mitano wamekuwa mabilionea na wanatuona sisi wazawa hatuna akili haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama hapa kukuomba wewe na kuomba Bunge hili tukufu kwa sheria hii ya Mwaka 1994 ya kuwawezesha wazawa kiuchumi, wazawa wapewe kipaumbele ni nchi gani duniani ambayo hakuna mnong’ono wa Taifa ni lazima Taifa hili linong’one na kusema ya kwamba biashara ya kiwango hiki itaenda kwa wazawa, barabara ya kilomita hizi zitaenda kwa wazawa, haiwezekani tukawaachia wageni kila kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninayasema hayo siyo kwamba nachukia wageni nchi yangu inahitaji sana mitaji kutoka nje, lakini pamoja na kuhitaji mitaji kutoka nje bado tuwe na uwezo wa kuwa- protect watu wetu na kuwapa watu wetu kipaumbele ya kwamba tumezungumza hapa ndani nataka haya mambo yaende nje ya kwamba tender za aina fulani zitaenda kwa watu wetu hata kama hatuzungumzi, hata kama hatuandiki kwenye magazeti, hatakama hatusemi huko nje tunajua nitakapo tenda mimi na akatenda na huyu kutoka nje nitapewa mimi kwa sababu fedha hizo zitazunguka hapa hapa nchini kwa ajili ya uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili lizingatiwe kwa sababu watanzania wamechoka kuona wageni wanaendelea kutajirika wao wanaendelea kuwa maskini. Ni lazima wao wapewe nafasi ya kutajirika kwenye nchi yao nah ii nchi ni ya kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitaandika kwa maandishi mambo yote ninayoyazungumza ahsante kwa kunipa nafasi nashukuru sana. (Makofi)