Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa nafasi ambayo umenipa ili niweze kuchangia hizi hotuba mbili, Hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya PAC pamoja na Hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti. Kwa ujumla wenyeviti wote hawa wawili wametoa hotuba nzuri sana hapa Bungeni, na kwa kweli tunawapongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza nizungumzie Mashirika ya Umma ambayo Mwenyekiti pamoja na Kamati nzima ni vizuri kwenda kuisimamia Serikali kule ili kuhakikisha kwamba TR anajengewa uwezo mkubwa wa kifedha na rasilimali watu ili aweze kuyasimamia mashirika haya kikamilifu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni kwamba hapa tunazungumzia mapato ya Serikali. Kwenye taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ukurasa wa 31 ameeleza performance ya ukusanyaji wetu wa mapato. Pale kwenye mapato yasiyo ya kodi tuna asilimia 36 tu, yaani hadi mwezi wa 12 tuna asilimia 36; kwa hiyo ni likely kwamba hatuwezi kufikia asilimia 100. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuliomba tuletewe jedwali la wizara na taasisi zote zinazohusika na ukusanyaji ili tujue ni nani ambaye hakusanyi vizuri na sababu zake. Kwa bahati mbaya sana mpaka tunawasilisha hotuba hii hatukuweza kuletewa jedwali hilo. Lakini bado tunasisitiza kwamba jedwali la wakusanyaji wote wa kodi liletwe tulione na tuone ni nani ambaye anashindwa kukusanya mapato ya Serikali sawasawa, kwa sababu pale nyuma walikuwa wanasingizia Corona haipo, sasa kwa nini wameshindwa kukusanya mapato kama ilivyotakiwa kwenye Bajeti ya Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine ninalotaka kulizungumzia, wengi wamezungia ajira za Watanzania hapa. Ni ukweli usiopingika kabisa kwamba tusipojipanga vizuri kuhakikisa kwamba tunalinda ajira za Watanzania, na Watanzania hawa milioni 60 wasiposhiriki kikamilifu katika uchumi wao hatuwezi kupata maendeleo, hata tungefanyaje.

Mheshimiwa Naibu Spika, zipo hujuma nyingi zinazofanywa, nyingine zinafanywa hata na Serikali yenyewe. Kwa mfano kwenye manunuzi, inakuwaje mpaka leo hii Serikali inaenda kununua bidhaa na huduma nje ya nchi ilhali ina viwanda hapa nchini ambavyo vinazalisha bidhaa hiyo? Mfano sasa hivi Serikali imeanza kununua dawa za kuogesha mifugo katika bajeti ya mwaka 2021/2022, wameanza kununa dawa za kuogesha mifugo kwa wazabuni wanaoingiza kutoka nje ya nchi ili hali hapa nchini tuna kiwanda kinachozalisha dawa nyingi za kutosha kuhudumia mifugo ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hiyo haitoshi, bado hadi leo hii Wizara ya Ujenzi inaajiri mkandarasi na mshauri mwelekezi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kujenga barabara ya kilometa 11 za lami; ili hali kuna Watanzania wenye uwezo wa kujenga mradi huo na wana weledi wa kutekeleza mradi huo. hivi ni kwa nini tufikie hapo? Haya yote yamefanyika na Bunge hili lipo na Serikali ipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni hili ambalo tumelizungumza sana, nalo hili ni sababu kubwa ya kukosesha Watanzania ajira, katakata ya umeme. Katakata ya umeme imeelezwa kwenye Bunge lako, na jana ilizungumzwa na Bunge lako Kamati husika ilipowasilisha, na majibu ya Serikali yaliyotolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kushauri hapa, kwa majibu yaaliyotolewa na Serikali na taarifa ya Kamati ya Nishati iliyowasilishwa, na majibu yaliyotolewa zamani na Serikali kwenye Bunge hili, ninaomba jambo hili tulifikishe mwisho. Tulishawahi kuyafikisha mwisho mambo mengi magumu. Tuliwahi ufikisha Richmond, ESCROW; na hili kwa majibu ya mkanganyiko yanayotolewa na Serikali kuhusu katakata ya umeme na kuwasababishia Watanzania kuingia kwenye dhiki kubwa, viwanda vnafungwa, uzalishaji unashuka na inaleta mfumuko mkubwa wa bei…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Ningependa kumpa taarifa mzungumzaji kuhusiana na suala la katakata ya umeme. Nimpe taarifa tu kwamba Mheshimiwa ukiendelea kuliongelea suala hili na wewe utaambiwa kama nillivyojibiwa mimi, kwamba sikupenda Mama Samia awe Rais au yeye awe Waziri. Ni hiyo tu.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mpina hiyo si taarifa, endelea.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan asiingizwe katika mambo haya, Rais wetu asiingizwe katika udhaifu wa utendaji wa baadhi ya Mawaziri, wamuache Rais wetu afanye kazi nzuri ya Watanzania. Udhaifu wa Waziri autetee mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuyasema haya, kwanini nataka tume teule ya Bunge iundwe? Kuchunguza suala hili la katika katika ya umeme na kuchelewa kwa mradi wa Mwalimu Nyerere, ziko sababu!

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2015 mapato ya TANESCO yalikuwa bilioni 72, tulisimamia yakapanda mpaka yakafikia bilioni 160 kwa mwezi, na sasa imewasilishwa mwaka 2021 mapato ya TANESCO yamefika trilioni 2.4. sababu za kushindwa kufanya ukarabati na matengenezo zinatoka wapi? Hawa hawa TANESCO walikuwa na madeni sugu yaliyofikia bilioni 272, yakasimamiwa yakapungua mpaka yakawa bilioni 49, sababu ya kushindwa kufanya matengenezo yanatoka wapi? TANESCO hawa wameweza kufanya kazi nzuri mpaka tukazima mitambo ya mafuta ya IPTL, AGRECO na Symbion ambayo yalikuwa yanagharimu bilioni 719 kwa mwaka; na sasa gharama hizo wameziokoa, sababu za kushindwa kufanya ukarabati wa mitambo inatoka wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu ilikuwa inafanyiwa ukarabati, tulikamilisha miradi mipya kutoka mwaka 2015 mpaka 2020, tumekamilisha miradi mipya iliyokuwa haijakamilishwa, tukaweza kupanua njia na kusafisha njia za usafirishaji wa umeme na mpaka tukasababisha vijiji ambavyo vilikuwa na umeme kutoka 2018 mpaka 10,312. Upanuzi huo wote umefanyika. Leo hii TANESCO sababu za katakata ya umeme zinatoka wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Bunge lako liambiwe ukweli, na kama miaka mitano, kama inavyozungumzwa, ni kama miaka sita kama inavyozungumzwa, kwamba ukarabati ulikuwa haufanyiki, kwa nini sasa umeme ulikuwa haukatiki? Kwa nini umeme ukatike leo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Watanzania waambiwe ukweli, majibu ya bla bla katika jambo hili hatuwezi kukubali katika Bunge hili. Ukikosa umeme kwenye Taifa; Mheshimiwa Rais wetu leo hii anahangaika sana kutafuta wawekezaji ndani na nje ya nchi, utamleta mwekezaji wa nani anayeambiwa kwamba Taifa halitakuwa na umeme mpaka uwe na trilioni mbili. Ina maana kwamba tusipopata umeme hauwezi kuwaka?...

NAIBU SPIKA: Ahsante.

MHE. LUHAGA J. MPINA: … na utaendelea kukatakata…

NAIBU SPIKA: Ahsante!

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge hili lisikubali, na tume teule ya Bunge iundwe, ichunguze jambo hili pamoja na lile…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)