Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kupata nafasi ya kuchangia kwa hizi dakika tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru na nikupongeze wewe lakini nitumie nafasi hii kuwashukuru sana Ofisi ya Msajili ya Hazina ambao sisi kama wajumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma tunafanya nao kazi kwa ukaribu sana na hata uzuri ripoti yako unayoiona na uliyoisikia leo ni kwa sababu ya wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianzie pale ambapo ameishia Mheshimiwa Malima jambo kubwa sana ambalo Serikali inabidi ilifanyie kazi kwa umakini mkubwa ni namna ya kuangalia mashirika haya ambayo tumeyapa nafasi ya kufanya kazi na usimamizi wake kwa namna moja au nyingine tunakuwa na miradi isiyokamilika kwa wakati na kwa mfano mzuri sana ni miradi ambayo iko kwenye shirika la nyumba la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna miradi imeanza muda mrefu lakini iko miradi ambayo imesha-takeoff sasa inakwenda vizuri. Lakini ni kwa nini miradi ambayo bado haijaanza kuchukuliwa hatua mpaka leo takriban miaka 10 haitakiwi kuanzishwa na kuendelezwa mpaka sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna miradi ya mfano pale Kawe wanaoishi Dar es Salaam watakuwa wanaijua 711 Kawe na ile Golden Premier Licence Kawe. Hapa kuna mbia lakini huyu mbia kila siku anaingilia hapa anatokea hapa niombe sana Serikali iingilie kati fedha zilizowekwa pale ni fedha za walipa kodi na kama tutaacha hivi tutakuwa tumetupa fedha na hatutakuwa hatuwasaidii watu wa National Housing. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaamini fedha zinazokuja wakati wa gawio ni moja ya chanzo kizuri sana cha mapato kama taasisi hizi zitafanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini la pili ni kuhusu kiwanda cha viuadudu kama tulivyoambiwa hapa na wenzangu waliopita kiwanda hiki ni mali ya Serikali kupitia NDC kwa asilimia 100. Serikali yetu inapata fedha nyingi sana kwenye mfuko kutoka mataifa na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kushughulikia malaria asilimia 98 fedha hizi zinashughulikia ugonjwa wa malaria na sisi tumepata bahati ya kuwa na kiwanda hapa ndani bahati mbaya sana asilimia hizi 98 ya fedha kutoka Global Fund hatuwezi kuzitumia kununua dawa kwenye kiwanda chetu cha viuadudu kwa sababu dawa hizi zinazozalishwa hazijaidhinishwa na ithibati ya WHO. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tuna dhamira ya dhati ya kupambana na ugonjwa wa malaria ni lazima tufike sehemu tukubali NDC, Serikali pamoja na hao ambao ni radio farm kutoka Cuba ambao ndiyo wenye hati miliki ya hivi viuadudu wakikaa pamoja shida ya hawa ni shilingi 6% itakayowafanya wao wawasaidie kwenye kiwanda hiki kupeleka WBHO waidhinishe ili dawa hizi zitakazokuwa zinatumika zikubalike kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo pale Uganda wameanzisha ujenzi wa kiwanda cha viuadudu kama hiki tulichonacho sisi hapa NDC. Hebu niambie kikikamilika dawa hizi tutauza wapi? Tutabaki kuhangaika na halmashauri zetu ambazo tumeshatoa maelekezo lukuki lakini hayazingatiwi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikuombe sana na niiombe sana Serikali hivi viwanda tunavyovianzisha kwa nia njema kama hatutakuwa na mpango mahususi wa kuwekeza nguvu na usimamizi mzuri nimesema hapa TR anafanya kazi nzuri sana lakini wakati mwingine kwa namna moja au nyingine anaweza akazidiwa asifikie malengo yake. Kwa sababu kama walivyosema akipia huku watu wanatokea huku ni kitu gani kinachoshindikana kiwanda hiki ithibati hii iende WHO ithibitishwe na dawa hizi katika asilimia 98 ya dawa tunazopata kutoka kwenye Global Fund zikija hapa tutakuwa tumevuka lengo la tumeokoa watanzania wengi sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)