Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Naomba nianze na hoja ambayo iliwahi kuletwa hapa kwenye Bunge la Kumi na Mheshimiwa Margaret Sitta, baadaye ikapigwa danadana, sijui alikosa nguvu huyu, sasa nimekuja nimsaidie, tuongeze nguvu katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hoja Mheshimiwa Waziri wa Afya anaitangaza kwa nguvu zake zote; hoja ya fifty by fifty. Mheshimiwa Waziri, huwezi kufanikiwa hii hoja kama watoto wa kike wanaobeba mimba mashuleni waharuhusiwi kurudi kusoma. Utakwama tu! Utakwama mapema kwa sababu tunapofanya enrolment shuleni wanafunzi wa kike 50, wa kiume 50 au 40 kwa 40. Mwisho wa siku wale wasichana wako wanabeba mimba, wanaume wanabaki. Hiyo hamsini utapata wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekwenda Zambia, nimeisoma vizuri kweli! Kwa kweli kama Mheshimiwa Waziri yuko tayari, niende naye Zambia hata kwa nauli yangu. Twende ukaone kitu kinaitwa Return to School Policy. Sera ya Wanaopata Mimba Mashuleni, wananyonyesha miezi mitatu, wanarudi kusoma shuleni. Sisi hapa sijui tuna tatizo gani? Hii ndiyo tumeiona dhambi kubwa kuliko nyingine tunazozifanya. Watoto wa kike wanabeba mimba mashuleni, tunawaacha na hakuna anayefuatilia maisha yao ya baadaye! Hili nitaanza nalo mwaka huu na mpaka nitakapotoka humu, sitaliacha! (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Zambia tulipouliza, nini madhara? Yaani haliongezi kasi ya mimba? Walituambia kasi ya mimba imepungua kwa sababu wanaporudi they fill shy. Kwa hiyo, wale wenzao wana-learn through them, kwamba kumbe kubeba mimba ni tabu! Wanarudishwa mashuleni kwa lazima! Lazima urudi shule! Sasa wewe umerudi, ulishabeba mimba tena miezi kadhaa kabla ya kujifungua, ndiyo unaruhusiwa ukajifungue, wote wameiona pale shuleni inaonekana na unarudi wanajua umemaliza kunyonyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, na wenzao wanasema haiwezekani na wao yawakute hayo. Sisi hapa tunaona kwamba ndiyo tutakuwa tumewahamasisha sasa kwamba mambo ni bomba! Naomba tuone uchungu, akinamama mwone uchungu! Nanyi msingekuwa humu! Hao 400 ambao kwa mwaka wanabeba mimba, maisha yao ya baadaye yako wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani akina mama wengi wataniunga mkono, nami katika hili nitakuwa ambassador, tuokoe hiki kizazi kinachoteketea bila elimu. Mwisho wa siku watoto hawa ndiyo wanakuwa mitaani. Yaani umaskini unatengenezwa na sera zetu wenyewe. Wanakuwa maskini, wanaishia kuwa ombaomba, wanatupa watoto, kama vile watoto wale hawakuwa na haki ya kuja duniani. Naomba hili tuendelee nalo; Mheshimiwa Waziri atakapokuja atuambie, hawa watoto watarudi kusoma? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ambalo nilitaka nilizungumzie jioni ya leo ni viumbe ambavyo vipo hatarini kupotea nchini. Viumbe ambavyo viko hatarini kupotea nchini ni wanawake weusi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake weusi wanapotea Tanzania. Katika hotuba yake Mheshimiwa Waziri ameeleza ukurasa kama sabini na kidogo anavyopambana kudhibiti vipodozi visivyo salama kuingia nchini. Vile vipodozi vinaingia, halafu tunapambana kuvitafuta vilipokwenda kutumika. Badala ya kuzuia visiingie, tunasubiri viingie, kwanza, halafu tupambane na kuvitafuta vilipokwenda. Ni hatari kweli kweli! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Tunduma ukaambiwa tafuta mwanamke mweusi utapata shida! Kwa sababu ya Carolight zilizoko pale! Carolight ni vipodozi ambavyo ni vya hatari, vimepigwa marufuku na vinaendelea kuuzwa. Sasa Mheshimiwa Waziri atuambie, haya madhara wanawake wanayoyapata ya kansa za ngozi na vipodozi vinaendelea kutumika na mwisho wa siku wanawake wetu weusi wazuri wanapotea. Lazima tuchukue hatua juu ya hili! Hatuwezi kuliacha linaendelea tu; na vipodozi haramu. Unasikia zimechomwa tani na tani za vipodozi, vilipita wapi? TFDA wako wapi? Wanafanya kazi gani? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri atusaidie juu ya hilo, maana tutakuja kufikia hatua ya kutafuta mwanamke mweusi, unaenda kwenye Google ndio unamwona mwanamke mweusi wa kitanzania ni yupi na alikuwa anafananaje? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina hoja ndogo sana kwa wazee, Mheshimiwa Waziri atuambie kama pension kwa wazee ilishindikana, haya mambo tuyafute yaishe kuliko tubaki tunasema itakuja, itakuja. Wakati fulani tulisema tunatafuta umri wa wazee ni upi? Hivi mzee si anajulikana umri wake? Nchi hii hatujajua hata wazee ni wa umri gani? Retirement age Serikalini inajulikana 60, ukianza 60 hapo tayari wewe ni mzee. Kuna watu wame-extend wakasema twende 75. Sijui inakuwaje 75! Lengo lilikuwa ama wapungue wazee wasiwe wengi labda, tuweze kuwalipa vizuri; lakini miaka 60, huyo ni mzee. Hawa Wazee tuwape pension hata fedha kidogo, maisha yao ni magumu mno. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwelewe kwamba hawa wazee ndiyo wanaopiga kura vizuri. Yaani mngewapenda hawa, mambo yangekuwa mazuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, hoja ya wazee….