Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi nami jioni ya leo niweze kuchangia. Naomba nipongeze taarifa zote za Waheshimiwa Wenyeviti, ni taarifa njema kwa ajili ya maslahi mapana ya Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ya Bajeti, nimeshiriki katika kutoa michango na kwa siku ya leo nitaomba nitoe michango katika eneo moja tu. Ni ukweli usiopingika tumekuwa tukisema Bunge la Kumi na Mbili ni lazima liache legacy na litaacha legacy kwa kuhakikisha kwamba Serikali inasukumwa kwenda kuwekeza katika sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika pato la Taifa trilioni 163.88 sekta ya kilimo imekuwa ikichangia kwa trilioni 44.8 ambayo ni sawa na asilimia 26.9 ya pato la Taifa. Ni ukweli usiopingika kwamba Watanzania zaidi ya asilimia 66.3 nguvu yao yote iko kwenye kilimo. Kipekee naomba nipongeze Ubalozi wa Tanzania nchini China kwa kazi kubwa nzuri sana ambayo wamefanya katika kuhakikisha kwamba kunakuwa na mkataba kati ya Tanzania na China wa kuuza zao la soya. Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Balozi Kairuki, kazi njema sana anastahili kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika nchi ya Tanzania mikoa ambayo zao la soya linastawi ni pamoja na Mikoa ya Rukwa, Katavi, Mbeya, Songwe, Ruvuma, Mtwara, Lindi, Tanga na Kagera hasa Karagwe. Matumizi ya zao la soya ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, soya inatoa product nzuri sana ya maziwa ya unga pia inatoa mafuta mazuri sana first class, pia inatoa zao wanaita soya nyama kwa wale vegetarian ambao hawataki kutumia nyama, pia inatoa chakula kizuri sana kwa ajili ya mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kwa Serikali ni kwamba kwa ku-concentrate katika zao hili ambalo tayari tuna soko la uhakika nchini China, tuna soko la uhakika India na Ulaya, ni wakati muafaka wa kuhakikisha kwamba Serikali yetu inaenda kuwekeza kwenye kilimo kwa sababu manufaa ya kulima zao hili; moja, katika eneo ambalo umelima soya kama ambavyo ipo kwenye mazao ya mikunde ni kwamba inarutubisha ardhi na hivyo kupunguza matumizi ya mbolea za kemikali kwa asilimia hamsini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, majirani zetu siku ile Spika alisema siyo vizuri kuzitaja nchi jirani lakini katika mifano mizuri naomba mniruhusu niseme. Pamoja na kwamba Tanzania ndiyo ambao tuna mkataba na China na tumefanya kazi nzuri ya kusafirisha China, lakini ni ukweli usiopingika kwamba soya nyingi imekuwa ikipatikana kutoka nchi ya Zambia na Malawi, wakati Tanzania ndiyo tuna mkataba na China kuuza zao hili. Ifike wakati Serikali kuhakikisha kwamba inawekeza katika kupata mbegu bora ili hiyo mikoa ambayo nimeitaja ambayo zao hili linastawi na uhitaji kwa Mataifa ni mkubwa sana tuhakikishe kwamba zao hili linakuwepo nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika kwamba tumekuwa na tatizo kubwa sana la mafuta ya kula, tuki-concentrate katika zao moja tu la alizeti tukaachia soya tutakuwa hatufanyi vizuri. Naiomba Serikali na ni wakati muafaka, kwa fursa hii na mkataba ambao tumeingia na nchi ya China kwa miaka mitatu tuhakikishe kwamba dola nyingi zinaingia Tanzania kwa sababu tunauza tunapata forex, tunakuwa na soko la uhakika badala ya sisi kuendelea kuhangaika na zao la mahindi. Kama ambavyo nimesema inasaidia sana katika kurutubisha ardhi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachoomba Serikali kuhakikisha kwamba inakuwepo mbegu bora ambayo wenzetu wanazo. Kwa mfano, kwa nchi kama Zambia wana aina saba za mbegu, wana mbegu aina ya spike, wanayo mbegu aina ya safari, wanayo mbegu aina ya dina, Tanzania hatuna mbegu hata moja. Naomba kipekee nipongeze Wabunge ambao wamekuwa vinara akiwepo Mheshimiwa Msongozi amehangaika sana kutafuta mbegu ili kuweza ku- supply katika maeneo yake na Wabunge wengi ambao walikuwa na nia ya kuweza kusaidia maeneo yao, lakini kwa sababu hatuna mbegu Tanzania na tumekuwa tukikumbana na vikwazo vingi tungeweza kusaidia Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)