Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru na niwapongeze sana watoa hoja wote wamewasilisha vizuri sana na mimi nilitaka nichangie katika hotuba ambayo, imewasilishwa na Kamati ya Bajeti na hususani nataka nijielekeze katika kipengele ambacho aligusia daraja la Tanzanite.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi wakazi wa Kigamboni tuna daraja linaitwa daraja la Nyerere ama kwa jina limezoeleka kama daraja la Kigamboni. Daraja hili limeanza kutumika tangu mwaka 2015 na limekuwa ni daraja pekee ndani ya nchi yetu ambalo linatozwa tozo kwa mwananchi kuvuka. Wananchi wa Kigamboni hawana mbadala ili mwananchi wa Kigamboni afike mjini aidha apite Ferry ambako anapanda pantoni, analipa tozo au inabidi apite darajani kwa mguu ama kwa wale ambao wana magari na vyombo vya usafiri lazima alipe tozo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, daladala moja ambayo inavuka pale inachajiwa kati ya shilingi 5,000 kwa kila trip ambayo inavuka pale zikiwa trip 10 za kwenda na kurudi hiyo ni shilingi 100,000. Kwa hiyo, wananchi wa Kigamboni wanakosa usafiri wa njia route ndefu ambazo wananchi wakazi wa maeneo mengine wanazipata. Mwananchi wa Kigamboni ili afike mjini anahitaji nauli tatu mpaka nne tofauti na wakazi wengine wa Jiji la Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wananchi wa Kigamboni wamenituma kuulizia wamesikia kauli ya Serikali kwamba daraja la Tanzanite litakuwa bure, wakati wakazi wa Kigamboni wao ambao wanajiita ni masikini wanatozwa tozo ili waweze kuvuka kwenda mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hawana mbadala kama walivyo wakazi wengine wa Oysterbay na Masaki ambao, wana barabara ya Salender sisi ukipita kwenye Kivuko na ukipita darajani ni lazima ulipie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Kigamboni wameniomba niwaulizie kwa niaba yao je, ni kwa nini tu peke yao ambao ni daraja pekee, ambao wanapaswa kulipia na wakati wananchi wa Kigamboni wanachangia katika ujenzi wa madaraja mengine. Hata kama hili daraja limejengwa kwa mkopo wa Wakorea na ninatambua kwamba daraja lile la Kigamboni limejengwa kwa mkopo kutoka NSSF. Kwa nini Serikali isilibebe kama inavyobeba mikopo ya madaraja mengine? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe Serikali ilichukulie suala hili kwa uzito unaostahili wananchi gharama za maisha/ wananchi wa Kigamboni ni, kubwa sana na wananchi wa Kigamboni hawana mbadala wa kwenda mjini zaidi ya kupitia kwenye Kivuko na kutumia daraja. Tofauti na wakazi wengine wa Masaki, Oysterbay ambao wana barabara mbadala ya kuweza kupita. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niombe kwamba Serikali itafakari kuondoa tozo katika daraja lile la Kigamboni Serikali ibebe mzigo wa deni lile la NSSF, ili na wananchi wa Kigamboni nao wapate nafuu ya gharama za maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru sana kwa kunipatia nafasi ya kuchangia. (Makofi)