Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. MOSHI S. KAKOSO – MWENYEKITI KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote niwashukuru sana wote waliounga mkono hoja ya kamati ya Bunge ya Miundombinu, kwa bahati nzuri kati ya wachangiaji wote hakuna aliyepina hoja ya kamati yetu tunawashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo mambo mengi ambayo yamechangiwa na Waheshimiwa wabunge, nimepata hoja za wachangiaji wapatao 10 wakiwemo mawaziri Mheshimiwa Prof. Mbarawa na Mheshimiwa Nape ambao wamekuja kutoa ufafanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wazungumzaji ambao wamechangia kuunga mkono hoja ya kamati yetu wamesisitiza juu ya umuhimu hasa wa kuunganisha barabara kati ya mkoa na mkoa ambazo zimetolewa hoja kutoka kwa waheshimiwa wabunge naamini haya yote yaliyokuwa yakichangiwa yalikuwa yakiunga mkono hoja ya kamati yetu, na msisitizo wetu bado tunaishauri Serikali kuweka mipango thabiti ya kuimarisha na kuunganisha miundombinu ya barabara hasa kwenye mikoa ile bado haijaunganishwa ikiwemo mkoa wa Morogoro dhidi ya mkoa wa Lindi, Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ipo mikoa mengine ambao inahitaji kuunganishwa ikiwemo Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Mara na Mkoa wa Arusha na Mkoa wa simiu, hiyo ni mipango ambayo tunaisistiza Serikali kuhakikisha wanaunganisha hiyo mikoa. Lakini wachangiaji wengine wamezungumzia juu ya ucheleweshaji wa GN ni mambo ambayo tumekuwa tukiishauri Serikali na hilo naamini wao kama Wizara husika watakuwa na mahusiano au kuwa na ukaribu na Wizara ya Fedha kuhakikisha wanalimaliza hili tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawapongeza sana waheshimiwa mawaziri kwa ufafanuzi ambao wameutoa. Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa amezungumzia suala la ujenzi wa reli. Lakini amezungumzia juu ya ushauri ambao umetolewa na kamati kwenye eneo la ushauri uliotolewa juu ya umuhimu sasa wa Serikali kuwachia viwanja vya ndege ambavyo vimekuwa vikijengwa na TANROADS sasa vianze kujengwa na mamlaka husika, ametoa ufafanuzi na amekubali maelekezo ya kamati, tunashukuru sana na tunawapongeza kwa uamuzi huo ambao kimsingi utakuja kuleta tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nape amezungumzia juu ya maalalamiko ya wananchi ambao wamekuwa wakilalamikia zaidi juu ya vifurushi ambavyo wanavitumia kabla havijakamilika wakiwa wamenunua vinakuwa vinatumika kinyume na matarajio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumzia jinsi utaratibu unavyotumika kwenye hizo bando zinavyotumika lakini kuna malalamiko yale ambayo wamekuwa wakilalamika wananchi juu ya makosa ya kimtandao ambayo kamati imeendelea kuishauri Wizara kuhakikisha wanawahusisha Wizara ya Mambo ya Ndani kwa maana ya Jeshi la Polisi ili waweze kutoa ushirikiano wa karibu kwa ajili ya kumaliza tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaamini sekta ya mawasiliano imefanya mapinduzi makubwa kupitia TCRA, ni kweli kabisa kwamba matatizo mengi ambayo yanajitokeza kwenye mitandao mengi yanaiangukia Wizara ya Mambo ya Ndani kushindwa kutoa ushirikiano kwa maana ya Jeshi la Polisi wanapobaini wanashindwa kutoa ushikiano wa karibu. Naamini Mheshimiwa Waziri wakikaa pamoja kama Serikali tatizo lile ambalo linajitokeza mara kwa mara linaweza likatoweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo ambayo tumeyapata kutoka kwa Waheshimiwa wabunge sisi kama kamati tutaendelea kuishauri Serikali na tunawapongeza kwa mchango wao wa mawazo makubwa, nirudie kuwashikuru sana wajumbe wa kamati ya Bunge ya Miundombinu kwa kazi kubwa ambayo mmeifanya naamini mchango wao umeonekana kwa kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.