Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyoanza wenzangu naomba kuchukua fursa hii, kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma kwa kutujalia/kunipa fursa hii. Napenda kwanza kuipongeza sana Kamati yetu ya Miundombinu kwa ripoti nzuri na kubwa na sisi, kwenye Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ripoti hiyo tumeikubali na tunakwenda kuifanyia kazi kama walivyoelekeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nijikite kwenye ujenzi wa reli. Ujenzi wa reli unakwenda vizuri na mpaka sasa hivi ninavyoongea kipande cha Dar es Salaam mpaka Morogoro, chenye urefu wa kilomita 300 umefikia asilimia 95. Tarehe 18 Februari treni ya mwanzo ya umeme itaingia nchini na itafanya majaribio kwenye line ile, pamoja na kuwafundisha madereva wetu jinsi ya kuendesha treni ya umeme. Kipande cha pili cha kutoka Morogoro mpaka Makutupora chenye urefu wa kilometa 422 nacho kimefikia asilimia 81. Kipande cha tatu kutoka Mwanza Isaka chenye urefu wa kilometa 130 umefikia asilimia nnena kipande cha Makutupora mpaka Tabora yenye urefu wa kilomita 368, ambayo imegharimu takribani shilingi trilioni 4.4 tulisaini mbele ya Mheshimiwa Rais tarehe 28 mwezi Disemba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais na tayari ameshatupatia fedha kwa ajili ya kulipa advance payment/malipo ya awali kwa makandarasi hao. Mpaka hivi sasa tunavyoongea Serikali yetu imewekeza takribani shilingi trilioni 14.7 kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa. Kujenga reli ni jambo lingine lakini la msingi pia ni kuwa na miundombinu/vifaa vya kutumia reli hiyo. Wiki mbili zilizopita Serikali ilitoa kibali na tulisaini mkataba wa manunuzi, wa mabehewa 1,430 wenye gharama takribani Shilingi bilioni 301. Vile vile, tumesaini mikataba mingine kwa ajili ya vichwa vya treni vya umeme 17 EMU 10 na Simulator kwa takribani dola za Kimarekani 294.7. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi vichwa vya umeme pamoja na vifaa vingine tayari Serikali imeshaendelea kutoa takribani shilingi trilioni 1.2 tunawaambia watanzania kwamba, reli hii itakuwa ni reli ya kisasa na itakuwa na uwezo mkubwa na Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi tumejipanga vizuri mambo yatakuwa vizuri na itakuwa ni reli ya mfano ya kuigwa katika Bara la Afrika. Kwa upande wa viwanja vya ndege kweli tunakubaliana na Kamati kwamba, ipo haja sasa ujenzi wa viwanja vya ndege uhamishiwe kutoka TANROADS kupelekwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege. Hilo tunalifanyia kazi na tutalikamilisha hivi karibuni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Kamati yetu imeongea kwamba kuna changamoto kubwa ya mifumo ya TEHAMA pale bandari ni kweli, hilo tunalijua na tunaendelea kuhakikisha tunaiboresha ili sasa mapato yasiweze kupotea. Kila fedha inayoingia pale tuweze kuijua imekwenda wapi na imefanya nini. Kuhusu mizani kuna Mbunge mmoja ameongelea kuhusu mizani hili ni jambo kubwa na tunalijua na tumekuja na utaratibu mpya sasa wa kupunguza mizani. Kwa mfano, magari ya mafuta yanayotoka bandarini kwenda Kigali sasa yanapima kwenye mizani tatu tu na tunaendelea, nafikiri huko baada ya mwezi mmoja tunafanya utafiti tutapunguza na itakuwa inapima mizani moja tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nia yetu ni kuhakikisha kwamba tunaifungua Bandari ya Dar es Salaam na kila mtu aweze kutumia Bandari ya Dar es Salaam. Mwisho kuhusu mradi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (BRT) tayari tumefanya awamu ya kwanza (BRT I) tayari imekamilika. Tuko (BRT II) sasa inaendelea vizuri na hivi karibuni tutaanza kufungua baadhi ya maeneo na (BRT III) tutaanza kusaini wiki mbili zinazokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia 100. (Makofi)