Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili nichangie kwenye hoja iliyoko mezani ambayo imetokana na taarifa za Kamati zetu na nitakwenda kujikita kwenye taarifa iliyotokana na Kamati ya Miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia kidogo, nichukue nafasi hii kumshukuru sana Rais Samia kwa kuniamini na kuniteua kuwa Waziri kwenye kusimamia sekta hizi za Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Ahadi yangu kwake na kwa Watanzania kwamba sitamwangusha, nitatimiza wajibu wangu kama inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue pia nafasi hii kuipongeza Kamati ya Miundombinu chini ya Mwenyekiti wetu Mheshimiwa Kakoso na Wajumbe wote wa Kamati hii kwa kazi nzuri sana na ripoti nzuri waliyoiwasilisha mezani leo, wanafanya kazi nzuri sana. (makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nigusie mambo mawili makubwa. La kwanza, kumekuwa na malalamiko ya muda juu ya namna ambavyo bundles zetu zinatumika kwenye simu zetu. Kuna uwekezaji mkubwa sana umefanyika kwenye Taasisi yetu ya Kudhibiti Mawasiliano ya TCRA. Awamu ya Tano imefanya uwekezaji mkubwa, lakini Awamu ya Sita imefanya uwekezaji mkubwa sana, kiasi kwamba uwezo wao wa kufuatilia miamala hii mbalimbali umeongezeka sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya hizi bundle kwenye simu zetu. Hoja hii kwamba kuna bundle ambazo zinawekwa kwenye simu, zinatumika bila mtumiaji kuzitumia yamekuwepo haya malalamiko, yamefikishwa kwenye mamlaka husika na uchambuzi umefanyika. Matokeo ya uchambuzi yanaonesha, matokeo ya uchambuzi ambayo yamefanyika mpaka sasa yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa na matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa huitumii kuna baadhi ya applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu na zinatumia bundles ambazo umeziweka. Matokeo yake ukija ukiangalia unakuta bundle imetumika, wewe unaona hujaiutumia, lakini kuna applications zimeendelea na kwa sababu sasa ni simu za kisasa, wakati mwingine ujuzi wa kujua kwamba kuna applications zinaendelea imekuwa shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya pili; simu hizi za kisasa unaweza ukaweka bundle lako, ukawasha kuna kitu kinaitwa hotspot, kinachoruhusu mtu mwingine kutumia data uliyonayo bila kufunga, ukiweka password ni lazima umruhusu, usipoweka wapo watu wamelalamika simu zao zilipochunguzwa ikakutwa kuna watu wametumia kwa kujiunga wakatumia wifi wakatumia bundle zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa suluhisho ni nini? Tunayo mamlaka ya watumiaji ni Baraza la Watumiaji wa Huduma za Simu, wametengeneza application ambayo ipo kwenye majaribio ambayo ikianza kutumika itamsaidia mtumiaji wa simu awe anafuatilia matumizi ya bundle aliyoiweka na atakuwa na option sasa ya kuzima baadhi ya applications ambazo zinatumia mtandao wake. Kwa hiyo, kwa hapa tulipofika tunafanya majaribio ya application hiyo na ikishakuwa tayari watumiaji watapewa, wanatafuatilia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hili, tumejikita kwenye kutoa elimu ya matumizi ya hizi simu za kisasa ili watu wasijikute wanaingia kwenye gharama ambazo hazina sababu kwa kutokujua. Utafiti umeonesha shida kubwa ni kwenye matumizi badala ya wizi, mpaka sasa hatujakamata wizi.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, muda umekwisha?

MWENYEKITI: Muda umekwisha, lakini kwa sababu unaongelea bundle nakuongezea dakika moja. (Makofi)

WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Jambo hili limekuwa kubwa na kwa sababu limekuwa linazungumzwa kwa muda mrefu ni rahisi kudhani kuna wizi na tukawahukumu operators kwamba wanaiba, lakini Mamlaka ya Mawasiliano malalamiko yote ambayo mpaka sasa yamefikishwa kwenye mamlaka, hakuna lalamiko ambalo limethibitisha kuna wizi. Bado yanaendelea kupokelewa, lakini tunadhani njia mbili kubwa za kutumia; moja tutoe elimu ya matumizi ya simu za kisasa; lakini ya pili kubwa kuliko yote tutengeneze application ambayo imeshatengenezwa inafanyiwa majaribio. Huu utakuwa ni muarobaini kwa sababu itakwambia umetumiaje data yako, ni application gani umetumia zaidi na umetumia kwa wigo gani. Tunadhani hili litaondoa haya maneno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na nakushukuru kwa nafasi uliyonipa. (Makofi)