Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Mariamu Ditopile Mzuzuri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa fursa hii. Nianze kwanza kuipongeza Kamati yangu ya Nishati na Madini chini ya Mwenyekiti wetu Mheshimiwa Dunstan Kitandula. Kwa kweli tumefanya kazi kubwa sana na tunashauriana na Serikali ili sekta yetu ya nishati na madini iweze kuwa na tija katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite kwenye ushauri ambao hasa ni endelevu. Kwa kweli shirika letu hili la TANESCO ni kubwa mno na nishati yetu hii ya umeme inahitaji mipango mikakati ambayo ni endelevu. Leo hii Taifa letu ambalo tayari tumeshaanza kuchochea uchumi wa viwanda tuna umeme wa Megawatt 1,600 na tunajiona kwamba tuna umeme wa kutosha na wa ziada, lakini ukienda duniani na kujifunza utaona tuko nyuma sana na tumechelewa kujipanga vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii nchi ya Afrika Kusini ambayo ina population ya watu takribani milioni 59.3 ina uwezo wa kuzalisha umeme Megawatt 52,000 na bado wananunua umeme kutoka nchi Jirani ya Msumbiji na Namibia. Kwa hiyo, ukiangalia Rule of Thumb, kwenye nchi ya Afrika Kusini moja tu, kwamba Megawatt 1,000 ni sawa sawa na watu milioni moja, huo nindiyo uwiano wa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi leo katika nchi yetu tuko takribani milioni 60 lakini tuna umeme ambao ni Megawatt 1,600 na tukiona namna tulivyojipanga ni kwamba 2025 tunategemea kuwa na Megawatt 5,000. Mwaka 2044 tunajipanga kuwa na Megawatt 18,000. Sasa tukajifunza kwa wenzetu na nchi hii ya Afrika Kusini, hivi tunavyoongea, wana hali mbaya ya umeme kuliko sisi. Leo South Africa wana mgao wa umeme na baadhi ya maeneo hakuna umeme kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia nature ya matatizo, tunafanana; uchakavu wa miundombinu na kutokufanya periodic maintenance ya hivi vituo vyetu vya kupooza. Kwa hiyo, naona kikubwa kwa shirika letu, napongeze sana uteuzi wa Mheshimiwa Waziri pamoja na MD wa TANESCO, tunaamini nyie ni vijana, basi hebu kaeni chini mtumie vipawa vyenu muweze ku-plan, kwa sababu Wagogo wanasema: “If you fail to plan, then you plan to fail.” Tunataka kwenda kwenye uchumi wa juu, wa viwanda, lazima tuwe na umeme toshelevu ili kuepuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jambo lingine la kuzuia, huko tunakoenda kwenye planning, ushauri wangu mwingine kuna kitu kinaitwa live line technology. Kwa sababu tumeona, walitutangazia siku kumi ili wafanye marekebisho kwenye vituo, lazima wakate umeme. Ila dunia ya sasa hivi, kuna kitu kinaitwa live line technology; ni mfumo unaoruhusu uendelee na ukarabati wa umeme bila ya kukata umeme. Huko ndiko dunia ilipo. Najua ni gharama, lakini ni bora utumuke leo kwa gharama kubwa lakini kuokoa hasara kubwa ambazo tunaweza kuzipata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naona ukitumia hii live line unaweza kubadilisha nguzo bila kukata umeme, unaweza ukaunganisha watu wapya bila kukata umeme, unaweza ukabadilisha vikombe bila kukata umeme, unaweza kubadilisha transformer bila kukata umeme, unaweza kufanya marekebisho na matengenezo kwenye vituo vya kupooza bila kukata umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hilo nalo tuliangalie. Ni uwekezaji mkubwa, lazima tuwafunze wataalamu wetu. Yapo mashirika binafsi hapa hawana tu uwezo wa kifedha, lakini TANESCO ikikaa nao kuona namna gani ya kuwawezesha ili tuingie na sisi kwenye utaalam huo, haya matatizo yataweza kuondoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nchini kwetu tuna tatizo kubwa la radi. Kuna baadhi ya maeneo yanakaa muda mrefu bila kupata umeme kwa sababu ya radi, lakini huko duniani kuna technology inaitwa comby Unit; kuna kifaa kinawekwa kwenye transformer…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MARIAM D. MZUZURI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja za Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. (Makofi)