Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nishukuru kwa kupata fursa ya kuchangia. Nina mambo machache na ningeomba Bunge hili tumsaidie Waziri na Naibu wake na Katibu Mkuu ili mwaka kesho wakija watuambie wamepunguza vifo vya akinamama kwa kiwango gani. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, takwimu zipo na ukitazama vifo vya akinamama vinachangiwa na nini? Moja ni access to health services, wao kutopata huduma nayo ni moja kati ya sababu kubwa inayowachangia kupatikana kwa vifo vya akinamama. Kwa takwimu tunapoteza akinamama 42 kwa siku kama nchi. Kwa hiyo, nilichokuwa nataka niombe ni nini?
Mheshimiwa Spika, nataka niombe Bunge hili tupitishe, tuitake Wizara ya Fedha impatie Waziri wa Afya shilingi bilioni 7.5 mwaka huu ili akinamama wajawazito wote wakatiwe Bima ya Afya ya National Health Insurance Fund. Kutokana na takwimu za nchi yetu, kwa wastani akinamama wanaojifungua kwa mwaka ni average ya akinamama milioni moja na laki mbili, maximum milioni moja na laki tano. Wakipata Bima ya Afya ya average ya shilingi 50,400 ni sawasawa na shilingi bilioni 7.5. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Waziri wa Afya aidhinishiwe fedha hizo, Waziri wa Fedha akatafute fedha hizo popote ili akinamama hawa nchi nzima kwa sababu mama anakwenda kliniki, akienda kliniki anakuwa registered, anakatiwa bima ya afya, baada ya miezi tisa anakwenda kujifungua bila kwenda na gloves, wembe wala kitu chochote na tui-task bima ya afya kuweza kulifanya jambo hili. Hii itakuwa ni njia moja ya kutatua tatizo au kupunguza vifo vya akinamama kwa sababu kila mama mjamzito atakuwa amepata haki ya kuleta kiumbe duniani bila matatizo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu sisi sote Wabunge tunafahamu ugumu wa maisha wa watu wetu, nataka nitolee mfano Nzega. Leo theatre iliyoko katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega na nimshukuru Waziri na Katibu Mkuu, katika theatre tatu zilizojengwa na ADB katika Wilaya ya Nzega, theatre iliyoko katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega imefunguliwa, bado theatre ya ndugu yangu Kigwangalla iliyoko katika Kata ya Lusu haijafunguliwa na theatre iliyoko Itogo kwa Mheshimiwa Selemani Zedi haijafunguliwa. Kumtoa mama Bukene kumleta Nzega ni kilometa zaidi ya 50 ili aweze kuja kupata huduma. Kwanza anaingia gharama ya usafiri, lakini bado akifika hospitalini anatakiwa aende na zile accessories ili aweze kupata hiyo huduma.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tukiwapatia bima akinamama nchi nzima, kwanza tutakuwa tumetekeleza ahadi na ilani ya chama chetu, tulisema akinamama wajawazito watapata huduma ya afya bure. Kwa hiyo, tuwakatie bima na ningeomba Waheshimiwa Wabunge tuungane pamoja kuitaka Serikali impatie Mheshimiwa Ummy shilingi bilioni 7.5 ili mwaka huu akinamama wajawazito wote nchi nzima, wakatiwe bima ya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, jambo la pili, sera ya afya inasimamiwa na Wizara ya Afya. Hili tatizo wewe umelisema katika lugha nzuri tu kwamba suala la afya ni TAMISEMI na nini; ni sahihi kabisa na ndugu yangu Sugu ameligusia, tutazame, D by D ambayo kama nchi tumei-adopt, kwenye Sekta ya Afya na ikija Wizara ya Elimu na nikipata fursa nitaongea, is it practical? Ningeomba Bunge hili kwa mwaka huu, tumtake Waziri wa afya, akabidhiwe hospitali zote zilizoko katika mikoa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nasema hivyo kwa sababu hii sekta ya afya katika nchi yetu inasimamiwa na Wizara ya Afya, on the other hand TAMISEMI, on the other hand Utumishi, Wizara tatu zinasimamia sekta moja, hatutopata efficiency. Kwa hiyo, ningeomba Bunge hili kwa mwaka huu wa fedha tumkabidhi Waziri wa Afya hospitali zote za Mikoa, siyo tu za Rufaa za Mikoa zote, kila Mkoa ukiwa na hospitali ya mkoa na kama mkoa hauna hospitali ya Mkoa, hospitali moja itambuliwe kuwa ni hospitali ya mkoa, akabidhiwe Waziri wa Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hii itatusaidia mambo yafuatayo; itatusaidia suala la usimamizi wa sera, itatusaidia katika usimamizi wa sekta ya afya katika hospitali ile, itasimamia ugharamiaji na uendeshaji, TAMISEMI tumwachie jukumu la ku-develop infrastructure peke yake. Kwa sababu haina mantiki, anayesimamia sera, hata tukienda Nzega pale mimi na Mheshimiwa Kigwangalla, hana mamlaka ya kumsimamia Afisa yeyote katika Hospitali ya Wilaya. Mfano, siku nne zilizopita katika Hospitali ya Wilaya ya Nzega hakuna umeme, Daktari hayupo, wagonjwa wamejaa OPD. Kwa hiyo, inabidi mimi ama Kigwangalla amtafute Mkurugenzi, bwana watu wako hawapo kazini na hakuna umeme, lakini Waziri hana mamlaka na yule Daktari aliyeko pale na huyu ndiye anasimamia afya.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ningeomba kwa mwaka huu tuwakabidhi Wizara ya Afya Hospitali za Mikoa, bajeti ya mwaka kesho, Wizara ya Afya ije ichukue hospitali zote za Wilaya ziwe chini ya Wizara ya Afya, kwa sababu wao ndio wanasimamia sera na wao ndiyo tutawawajibisha juu ya ubovu wa afya katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wenzangu, kama Bunge tuchukue jukumu la kutoa leadership katika nchi hii juu ya suala la D by D. D by D is not practical kwenye sekta ya afya, is not practical kwenye sekta ya elimu. Leo hii nataka nitolee mfano watoto wa form four wakifeli tunasema Wizara ya Elimu ime-perform hovyo, lakini hana mamlaka, hasimamii uendeshaji wala ugharamiaji, ndiyo hivyo hivyo kwenye Wizara ya Afya, Waziri wa Afya anasimamia sera tu. Kwa hiyo anatengeneza sera pale, anaiangalia ofisini kwake, mimi ni mjumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii, nataka niwaambie for my little experience, katika sekta mismanaged katika nchi hii ni sekta mbili, afya na elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niseme kama Mbunge wa Chama cha Mapinduzi na nataka nikupe mfano, wazee wa miaka 60 watoto chini ya umri wa miaka mitano, magonjwa sugu yasiyotibika, kwa maana ya kisukari, pressure na UKIMWI na mengine mama wajawazito hawa wote kisera wanatakiwa wapate huduma bora na huduma bure. Ukienda leo kufanya tathimini katika hospitali zetu hawa wana-constitute 70% ya wagonjwa wanaokwenda hospitali, lakini central government hai-subsidize fedha kwenye hospitali hizo. Kwa sababu tumesema kisera wapate huduma bure, lakini watakwenda pale, matokeo yake ataandikishiwa cheti, atafika pale, hatopata huduma, ataambiwa nenda dukani kalete gloves. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ningeomba ili mwaka kesho tuingie kwenye rekodi ya nchi hii, Wabunge wa Chama cha Mapinduzi na Wabunge wa Kambi ya Upinzani, tuungane kumsaidia mwaka huu Mheshimiwa Ummy na Mheshimiwa Kigwangalla, wawaondolee matatizo mama mjamzito katika nchi hii kwa kumpatia bima ya afya. It is doable, naamini Serikali inaweza na ni ahadi yetu kama Chama cha Mapinduzi, tuliwapa Watanzania kwamba mama mjamzito atapata huduma bure na bora. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na mwisho namwomba Waziri pale Nzega, sisi tumejenga OPD mpya, Mheshimiwa Kigwangalla anajua tumeishia njiani, kwa sababu imekuja amri ya maabara na madawati hatuna fedha…
SPIKA: Ahsante sana.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Tunaomba mtusaidie, ahsanteni.