Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumshukuru Mungu, lakini nikushukuru pia wewe kwa kunipatia nafasi ya kuchangia jioni hii. Nianze kwanza kwa kuwapongeza Wenyeviti wote wa Kamati hizi mbili kwa mawasilisho mazuri. Nianze moja kwa moja kwa kwenda kwenye point.

Mheshimiwa mwenyekiti, leo nitajikita hasa hasa kwenye mambo mawili. Jambo langu la kwanza ni kwenye utengaji wa asilimia 10 kwa ajili vijana, wanawake na wenye ulemavu. Ni ukweli usiopingika kabisa hili suala la utengaji wa hizi fedha asilimia 10 liko kisheria. Hata hivyo, tunaona katika baadhi ya halmashauri nyingi utengwaji wa hizi fedha hauendi na unakwenda kwa kusuasua mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inajitokeza pale ambapo tunaona kuna baadhi ya vikundi vingi sana vya akinamama, vikundi vya vijana lakini vya wenye ulemavu kila siku wanakwenda kule halmashauri kufuatilia hawapati, kina mama wanasumbuka mno na isitoshe kuna baadhi wanatoka mbali mno. Imagine kama mimi halmashauri yangu ipo mbali na jimbo langu, kwa hiyo kila siku wanagharamika kwenda halmashauri kufuatilia lakini hawapati majibu. Hii inatokana na ukweli kwamba hivi vikundi vingi vinavyopewa hizi fedha ni vikundi vya watu binafsi. Watu wengi wanaopewa hivi vikundi either ni viongozi wa vyama, lakini vikundi vingi ukivichunguza hivi wamiliki wa hivi vikundi ni watumishi wa halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sasa, nataka nitoe ushauri ili takwa la hizi fedha ziwalenge walengwa kabisa. Moja ya ombi tunaiomba Serikali kwanza iwe na database, kila halmashauri ituambie ni vikundi vingapi vimeomba, lakini ni vikundi vingapi vimepatiwa fedha na ni vikundi vingapi vimerejesha hizo fedha, tunataka tuzione.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia uwepo na ufuatiliaji; hawa Maafisa Ustawi wa Jamii na Maafisa Maendeleo hawafiki kule kwenye vile vikundi matokeo yake kuna vikundi hewa vingi mno. Kwa hiyo, kuwepo na model ya ufuatilia ili tuvijue vikundi halisi ni vipi? Kwa sababu kama hawa wananchi ambao tunaishi nao vijana na akinamama hawapati, hivi vikundi vinavyopata ni vya wapi? Ina maana kuna vikundi hewa vingi ambavyo vinamilikiwa na watu. Kwa hiyo, uwepo huo wa ufuatiliaji na data zijulikane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni uendeshaji wa masoko yetu na kuungua kwa masoko. Masoko yetu kwa sasa tunapata taarifa kila siku yameungua, yameungua, yameungua, lakini hatuambiwi nini chanzo cha kuungua masoko haya. Hata huvyo, tunajua kabisa haya masoko yamegharimu fedha nyingi sana katika ujenzi wake. Tukiangalia tu mfano wa Soko la Ndungai, lile soko ni miongoni mwa masoko yaliyogharimu fedha nyingi sana, lakini haya masoko hata uzalishaji wake kiukweli hauleweki na pamoja na kwamba yanatumia gharama kubwa lakini bado yanaungua kila siku. Kwa hiyo, niiombe Serikali kwanza ije na mpango, pamoja na kwamba inayajenga lakini yawe na mpango wa kuya-rescue haya masoko yetu kwa ajili ya matumizi ya baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeiomba Serikali pamoja na kwamba inayajenga haya majengo, tunaambiwa tuweke fire extinguishers kila sehemu zinasaidia nini zile fire extinguisher wakati kila siku yale masoko yanaungua. Ningeshauri kila masoko basi ziwekwe zile fire detectors ili angalau hata kama kuna viashiria vya moto viweze kutoa ashirio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine hapo hapo kwenye masoko, ningeweza kushauri Serikali kama inaweza inapofanya usajili wa hawa wafanyabiashara basi iweze kuweka na takwa la lazima la kila mfanyabiashara aweze kuwa na bima ya biashara. Hii bima ya biashara itawasaidia pale inapotokea majanga ya aina mbalimbali mfano pale inatokea moto. Tunaona wafanyabiashara wanawekeza mitaji yao mingi sana, wanakopa kwenye mabenki na sehemu mbalimbali ili kuendesha biashara zao. Linapotokea suala la moto soko limeungua, wanaambiwa tu mabenki wawaongezee muda wa kulipa so what? Wakati watu wameshaweka mitaji yao na imepotea, kwa hiyo nafikiria suala la bima litakuwa ni mkombozi kwa hawa wananchi ili waweze kufanya biashara vizuri, lakini wawe na uhakika wa kulinda mitaji yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, nimpongeze sana Mheshimiwa Rais ameweza sasa kutuletea miundombinu ya elimu, maji na afya. Tumeona kwenye suala la UVIKO tumeletewa madarasa mengi sana, vituo vya afya lakini na kwenye miradi ya maji. Hata hivyo, huwezi kuwa unaongeza tu kitu bila ya kuangalia population, tumeongeza madarasa ya kutosha well and good lakini je, hawa watumishi ambao watakwenda kufanya kazi kule wapo wapi? Niiombe sasa Serikali pamoja na juhudi hizi nzuri inazozifanya lakini iende sambamba na kuongeza watumishi katika hii miradi ambayo imeianzisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)