Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kwa mara nyingine ya pili nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kupata nafasi hiyo, nakutakia majukumu mema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nawapongeza sana Waheshimiwa Wabunge waliochangia hoja yetu ya Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji ambao yapata kama Wabunge tisa ambao wamechangia. Pia nawapongeza Mawaziri ambao wametoa ufafanuzi, Mheshimiwa Bashe, Mheshimiwa Ndaki bila kumsahau Mheshimiwa Aweso ambaye na yeye yuko kwenye Kamati yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sio lazima wote niwataje majina ila Mheshimiwa Profesa Muhongo, Mheshimiwa Profesa Manya, Mheshimiwa Profesa Patrick Ndakidemi, Mheshimiwa Kunti, Mheshimiwa Mwijage; na Mheshimiwa Polepole amepongeza na yeye kuwa mapendekezo yote yaliyopendekezwa na Kamati yaweze kuchukuliwa. Mheshimiwa Neema Lugangira na yeye kwa sababu usalama wa chakula ni mtambuka uko pia kwenye upande wa kilimo, kwa hiyo na yeye amechangia pamoja na Mheshimiwa Nusrat amesema ubunifu kwenye sayansi na hasa tunaposema kuwa ubunifu wa chakula, Mheshimiwa Gambo kwenye upande wa ajira ambao ni Ilani ya Chama cha Mapinduzi, pamoja na mambo ya maua tunashukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo yaliyoongelewa sana ni mengi ya kuhusu Tume ya Umwagiliaji, mambo ya pembejeo na mambo mengine yote yaliyoongelewa. Nawashukuru Waheshimiwa Mawaziri kama mmekubali kuwa mtachukua ushauri wetu na mapendekezo yetu na tumekuwa pamoja, naamini tutaendelea vizuri kama tulivyokuwa tunaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba taarifa yetu yote iweze kuungwa mkono na mapendekezo yote pamoja na Wabunge wote waliomo humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja ya Kamati. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante, toa hoja.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KILIMO, MIFUGO NA MAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.