Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi sana na Waheshimiwa Wabunge, ila nikutakie mema kwenye kazi zako kama Naibu Spika wa Bunge letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii pia kuwashukuru sana Wajumbe wa Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji, kwa ushauri wao na maelekezo yao mengi ambayo sio kwenye taarifa hii tumeyasikia, lakini pia kila wakati tunapokutana nao wanatupa maelekezo, wanatupa mapendekezo, wanatupa maoni ambayo ni ya kujenga kwa kweli, wao hawakai kwenye mstari wa kukosoa tu kama Serikali, lakini pia wanaonesha changamoto tulizonazo, lakini pia na kutuonesha njia ya kutoka kwenye hizo changamoto. Namshukuru sana Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati na Makamu Mwenyekiti pamoja na Wajumbe wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa ambacho kimezungumzwa kwenye taaarifa ni upatikanaji wa fedha lakibi bajeti ya Wizara yetu ya Mifugo na Uvuvi. Nipende kukubaliana na maoni ya Kamati, kwamba inawezekana kweli hapa tunachangamoto kubwa lakini wote tumekwisha kusikia commitment ya Serikali kuhusiana na sekta hizi za uzalishaji, kilimo, mifugo, uvuvi, maliasili na sekta zinazozalisha. Tumemsikia Mheshimiwa Rais mwenyewe alipokuwa akihutubia Bunge kwamba tunataka kuangalia na kuona ni namna gani tunaziwezesha sekta hizi za uzalishaji ili ziweze kujikita sawasawa kwenye kuzalisha ajira, lakini kuzalisha mazao yale ambayo yanazalishwa na hizi sekta. Lakini pia Mheshimiwa Rais amerudia jambo hili tulipokuwa kwenye ziara pamoja naye Mkoa wa Mara kwamba sasa ni zamu ya kuziangalia sekta hizi za uzalishaji kuona ni kwa namna gani zinapewa kipatumbele kibajeti ili ziweze kuzalisha na kutoa mchango wake unaotakikana kwa Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara ya Mifugo na Uvuvi, pia tumekuwa na jitihada hizo tukisaidiana kwa karibu sana na Wizara ya Fedha na Mipango. Hivi karibuni tumekwisha kupeleka maandiko yetu yote mawili la mifugo pamoja na andiko la uvuvi kuonesha ni kwa namna gani tunataka pesa kwenye components mbalimbali ili tukipatiwa zile pesa tuweze kuzalisha kwa wingi, tuweze kuzalisha ajira zinazotakiwa, lakini sekta hizi ziweze kutoa mchango wake mkubwa ambao kwa kweli unategemewa na Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninaamini kama maandiko haya tuliyopeleka na tuliyoji-engage pamoja na Wizara ya Fedha yatakapopita, tunaamini mchango wa sekta yangu ya Mifugo na Uvuvi itaweza kutoa mchango wake unaotakiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna maeneo mengi ambayo nisingependa kuyataja hapa ambayo tumeyaainisha kwa upande wa mifugo, lakini pia hata upande wa uvuvi tumeainisha na baadae kukubaliana na hivi karibuni tu kuna dalili njema sana kuhusiana na malisho ya mifugo yetu, Serikali ya China iko tayari na imekwisha iko kwenye hatua za mwisho kutupatia dola za Kimarekani milioni tatu kwa ajili ya malisho ya mifugo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, huo ni mfano mmoja tu wa jambo ambalo tayari Wizara ya Fedha na sisi tumeji-engage pamoja na kwamba kuna dalili nzuri ya jambo hilo kutokea.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia bado kuna mambo yanayohusiana na mabwawa, bado kuna mambo yanahusiana na maji, na suala la maji pia bado tuna engage pamoja na Wizara ya Maji, kwa sababu na wenyewe wana fedha za maji, lakini sisi pia tunatafuta fedha za maji pamoja na kwamba tumeshauriwa na Bunge lako kwamba angalau kuwe na namna ya kupanga pamoja, lakini tunakaa pamoja na Wizara ya Maji ili kwamba miradi yetu ya maji iliyopo Wizara ya Mifugo na itakayokuwepo Wizara ya Maji isiweze kuingiliana au tusiweze kuiweka mahali pamoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Serikali iko na commitment ya kutosha kuhusiana jambo la kubajeti kuhusiana na sera hizi...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa muda wako umekwisha malizia malizia sekunde kumi.

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana, lakini nilihakikishie tu Bunge lako kwamba Serikali imekwisha kuona kwamba kuna haja ya kuongeza bajeti kwenye sekta hizi za uzalishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. (Makofi)