Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, cha kwanza nikupongeze na nikutakie kila la kheri katika kutimiza wajibu wako na kutuongoza katika Bunge ukimsaidia Mheshimiwa Spika.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili niishukuru Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ushauri waliotupa na maoni waliyoyatoa. Nataka tu niwaahidi kwamba sisi kwetu maoni, ushauri na mapendekezo yao ni working tool, tutajitahidi ndani ya Serikali kuhakikisha yale ambayo ni kwa maslahi ya nchi tunayafanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni kweli, concerns za Waheshimiwa Wabunge zipo, na sisi kama Wizara na Serikali tunazitambua hasa kwenye eneo la umwagiliaji, pembejeo na gharama za pembejeo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la umwagiliaji, nilitaka tu niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na kuwaambia kwamba mapendekezo ya kuiwezesha Tume ya Umwagiliaji ni jambo ambalo halikwepeki. Tumeanza maongezi na wenzetu wa Wizara ya Fedha na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu tutapata fedha nyingi sana ambazo zitaenda Tume ya Umwagiliaji na tumekubaliana na Wizara ya Fedha, hivi sasa kuna miradi 19 ya umwagiliaji ambayo Tume ya Umwagiliaji imeshasaini na kupata wakandarasi, na tunaamini kwamba tutakapofika mwisho wa mwaka fedha zitatoka kwa ajili ya ku-facilitate hiyo miradi ambayo tumetangaza tender na kuwapa wakandarasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu eneo la ugani Wizara tayari sasa hivi imepatiwa fedha kwa ajili ya kuwapatia vitendea kazi Maafisa Ugani, na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu mwezi wa nne tutagawa pikipiki kwa ajili ya Maafisa Ugani, na sasa hivi tuko kwenye mazungumzo na Wizara ya Fedha kwa ajili ya kuwapatia Maafisa Ugani vitendea kazi. Mara ya kwanza allocation ilikuwa ni kwa ajili ya Maafisa Ugani 1,500 lakini tunaweza kufikia maafisa ugano wote 6,300 walioko nchini ili waweze kupatiwa vitendea kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kwamba tunabadili muundo wa Tume yetu ya Umwagiliaji ili kuhakikisha kwamba representation ya Tume ya Umwagiliaji itakuwepo mpaka katika Ofisi za Wilaya, kwa hiyo, itakuwa katika structure kama ilivyo TARURA na taasisi nyingine. Kwa hiyo kutakuwa na ma-engineer wa umwagiliaji katika ngazi ya Wilaya ili kuleta usimamizi wa karibu kwenye eneo la umwagiliaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo halikwepeki, nia kwamba tunatambua Watanzania wengi wako katika sekta ya kilimo. Sekta hii inatakiwa kufanyiwa mabadiliko ya kuwepo kwa sheria inayotu-guide, kwa hiyo tutaleta mabadiliko ya Sheria ya Ushirika, tutaleta Sheria Mpya ya Kilimo katika nchi yetu ambayo itatoa legal framework ya kuisimamia sekta kwenye masuala ya resources, financing na masuala yote yanayohusu mifumo ya kodi ili kuondoa matatizo tuliyo nayo katika sekta.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Arusha kwamba kuhusu subsector ya horticulture, kwamba tuko kwenye hatua za mwisho na Wizara ya Fedha na mashamba yale yatarudi na watawekeza Watanzania kwa priority na watapewa nafasi wawekezaji wa Kitanzania ili wawekeze katika subsector ya horticulture. Subsector ya horticulture ni sekta ambayo tunaipa jicho la karibu sisi kama Serikali kwa sababu ni sekta ambayo inakua na ni lazima tuendane na hali ya dunia inavyokwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie tu kuwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba tunashukuru kwa maoni na tahadhari zilizotolewa. Niwahakikishie tu kwamba sisi upande wa Serikali, suala la majadiliano juu ya kuifanya Wizara ya Kilimo ipate fedha ya kutosha yameshafika katika nafasi nzuri na Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo. Tunafanya mazungumzo na Wizara ya Fedha ili Wizara hii iweze kupata fedha inazostahili kwenda kuwahudumia wakulima wa nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kuhusu kilio cha mbolea na mwelekeo wa dunia unavyokwenda, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge hili litakuwa ni jambo la mwisho la kujadili katika nchi yetu. Ni lazima tu-subsidize kwenye inputs za kilimo, na huo ndio mwelekeo kwa sababu wakulima wetu ni wakulima wadogo; na hili tunalitengenezea legal framework na financing model ambayo tutakapoenda kutoa ruzuku basi ruzuku hiyo iweze kuwafikia wakulima, na tusifanye makosa ambayo tumekuwa nayo huko nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi nimalizie kuwashukuru Kamati, na niwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa maoni waliyoyatoa. Ahsanteni sana. (Makofi)