Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nami naomba nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kuchaguliwa na Wabunge kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye utekelezaji wa bajeti ambao umefanyika katika Wizara zetu tatu tunazozisimamia kuanzia mwezi Julai hadi Disemba mwaka huu wa fedha. Nianze kwa kuipongeza Serikali na Wizara ya Maji kwa kazi nzuri ambazo zinaendelea katika Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, sote tunakubaliana kama Wabunge kwamba Wizara ya Maji inafanya kazi nzuri na kuna miradi ya kutosha kabisa kwa kila Mbunge katika kila Jimbo, miradi inayogharamiwa na Serikali Kuu, Mfuko wa Maji na zile hela ambazo Mama yetu Rais Samia ametoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mfano katika pongezi zangu hizi kwamba kwenye bajeti ya maendeleo ya Wizara ya Maji Serikali ilikuwa imetenga shilingi 646,630,000,000 na katika pesa hizi Serikali imeshapeleka shilingi 413,950,671,097.95 ambayo ni sawa na asilimia 61. Kutokana na hili Mheshimiwa Juma Aweso na timu yake wanang’ara, wameendelea kung’ara kusema ukweli. Kwa hiyo, tunaipongea Serikali kwa kazi nzuri na kwa jinsi wanavyoisapoti hii Wizara ambayo tunaisimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tumeona kwamba kama Kamati kuna changamoto kwenye hii Wizara kidogo na ninaomba muichukulie seriously Waziri na watendaji wako, kwamba kwenye manunuzi kila kitu kinafanyika makao makuu na hizi Mamlaka za Maji na RUWASA kuna saa wanakwama kwamba, vifaa havifiki kwa wakati. Kwa hiyo, ni maoni yetu kama Kamati kwamba, hili lifanyiwe marekebisho ili ununuzi uende haraka na Waziri aendelee kuchapa kazi kama ambavyo anachapa pamoja na watendaji wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye Wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Wizara hizi kama Wizara, viongozi wa Wizara hizi wanajitahidi sana kutekeleza miradi mbalimbali, lakini wana changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa fedha kama ilivyokuwa kwa Wizara ya Maji; kwa mfano, katika bajeti ya maendeleo Tume ya Umwagiliaji imepangiwa shilingi bilioni 35 kama pesa za ndani na shilingi bilioni 11.5 kama pesa za maendeleo kwa pesa kutoka nje, lakini hadi mwezi Disemba, 2021 Tume hii ilikuwa imepokea shilingi milioni 349 tu ambayo ni 1% tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tuko serious tunakubaliana kwamba, Wabunge wote huku kila aliyekuwa anasimama alikuwa anasema kilimo, maji, umwagiliaji, lakini kweli kwa hii trend ya kutoa 1% kwa miezi sita tutafika kweli? Tutatekeleza vile vitu ambavyo tulikuwa tume-plan na tumewaahidi watu kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hapa tunaona kuna tatizo na tunaiomba Serikali iiangalie hii Wizara kwa jicho la huruma na wawape pesa, ili watengeneze miradi ya maji na mambo yaendelee.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika sekta ya uvuvi mambo ni yaleyale katika pesa za maendeleo zilizotengwa ambazo ni shilingi bilioni 99 wameshapokea shilingi bilioni tatu tu ambayo ni sawa na 5.1% katika sekta ya uvuvi. Katika sekta ya mifugo walitengewa shilingi bilioni 16.8 na wameshapokea shilingi 2.4 ambayo ni sawa na 14.6%.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hizi sekta ambazo zinaajiri wakulima wengi, wafugaji na wavuvi, sidhani kama tunazitendea haki. Kwa hiyo, ni mawazo ya kamati kwamba, pesa zilizopelekwa kutekeleza miradi ya aina mbalimbali ni ndogo na tukumbuke Rais alivyokuja kufungua Bunge letu, kutuhutubia hapa, alitoa ahadi kwamba, sekta hizi za uzalishaji kilimo, mifugo na uvuvi zitapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tutii lile agizo la Rais ili tufike mbele, bila hivyo ninaona tunakwenda ambako siko, tutahukumiwa na wale wapigakura.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo niseme tu naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)