Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nichukue nafasi hii kukupongeza kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kushika wadhifa huo na nikutakie kila la kheri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji napenda kujikita katika hoja ambayo inazungumzia dhana ya muunganiko pamoja na mwendelezo katika utoaji huduma ili kukuza uchumi. Lugha rahisi ni connectivity and linkages.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika sekta ndogo hiyo ya kilimo ya mazao ya bustani, maua, mbogamboga pamoja na matunda; kwanza ni sekta ambayo inakua kwa kasi, imeonekana ikikua kwa asilimia saba kulinganisha na kilimo chote kwa ujumla kikikua kwa asilimia nne, pia kinachotoa ajira nyingi kwa Watanzania na sasa inakadiriwa kwamba at least Watanzania milioni 6.5 katika mnyororo mzima wanashughulika na sekta hiyo ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuweka mkazo kwamba sekta hii ndogo ya maua, mbogamboga pamoja na matunda ni sekta ambayo ni logistic sensitive. Ninasema hivi kwa sababu tunahitaji usafirishaji kutoka kwa wazalishaji lakini je, ni wote katika mnyororo ule wanajua kwamba tuna- deal na perishable goods? Je, askari wetu barabarani wanajua kwamba hili ni kontena la maparachichi ambayo yanapaswa yafikie soko mapema? Je, tunapofika kwenye ports kuna handling facilities ambazo zitasaidia kutooza mapema kwa ajili ya bidhaa hizi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, unagundua kwamba kama hii ni emerging market kwa sasa, lakini je, watu wote katika mnyororo mzima unaotaka tutoe kutoka uzalishaji kufikisha bidhaa yetu sokoni ikiwa katika hali njema wana ufahamu huo? Je, pale Mamlaka ya Bandari tutachukua siku chache kuliko msafirishaji wa copper kwa sababu hizi ni perishable goods? Je, ufahamu huo upo? Je, kuna facilities za ku-handle kwa sababu hiki ni kitu ambacho kinahitaji uharaka?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tunahitaji kuwa na connectivity katika sekta hii kwa sababu tusipofanya hivyo tutagundua kwamba tija yake inaweza isionekane mapema na ndiyo maana huenda hata takwimu za nini tunapeleka nje ya nchi kutoka kwenye hii sekta ndogo imesababishwa na kutokuwa na facilities, lakini wakati mwingine pia kutokuwa na wadau wote kuhusishwa ili tuweze kufikia malengo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa msingi huo ninapenda kuiomba Serikali pamoja na Wizara husika kwamba tunapokuwa na kitu ambacho ni emerging market kama hii hapa ili tuweze kupata tija maana yake ni kwamba lazima tuwahusishe wadau wote wanaohusika, kwanza kuwapa elimu hiyo, lakini pia kuwapa tahadhari kwamba hebu tusifanye yale mazoea, maana yake ni kwamba tusije tukawa tunachelewesha bidhaa zetu hatimaye zikaoza au zikaharibika ubora kwa sababu tu watu fulani anadhani kwamba anapaswa kwenda kama ambavyo nafanya bidhaa nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii mara nyinge imetokea katika bandari zetu, lakini pia katika airports zetu japo ni kweli kwamba kuna improvement sana kuwepo na standard cold rooms katika airport zetu kwa ajili hiyo, nadhani kwamba bado kunahitaji kuwa na sensitivity juu ya jambo hili ili tuweze kupata tija. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu naelewa dakika zangu siyo nyingi niliamua niongelee jambo hili tu kwamba hebu sasa Serikali kwa maana ya Wizara ya Kilimo ijue kwamba wateja wake ni wengi sana, iwape elimu, iwape msukumo ili kwa pamoja kusiwe na vikwazo katika kufikia soko ambalo tunalihitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuliweka mkazo juu ya yale mashamba ya Arusha ambayo hayafanyi kazi kwa sasa, Serikali ifikie kuleta suluhisho la jambo hilo ili tuweze kupata tija. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana ninaunga mkono hoja. (Makofi)