Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nikupongeze kama mchangiaji aliyepita, na nimekuwa mtu wa pili kupata nafasi ya kuchangia toka uwe Naibu Spika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo ambayo ninataka nikukumbushe wewe mwenyewe kwa sababu tulikuwa kwenye Kamati moja na ulihudhuria kikao. Kumetokea malalamiko mengi sana kwenye suala la inflation. Nitatoa mfano mfupi nasi kwenye Kamati tulijadili, kwa mfano sasa hivi tumekuwa tukiongea kuhusu inflation kwenye nondo, kwenye sementi na vifaa vingine vya ujenzi. Examination gloves zimepanda kutoka shilingi 5,000 mpaka shilingi 18,000; paracetamol tablets kichupa chenye kukaa dawa 1,000 kimepanda kutoka shilingi 7,000 mpaka shilingi 22,000; Vitamin B Complex imepanda kutoka shilingi 5,000 mpaka shilingi 32,000. Naomba karatasi hizi nimpatie Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu yupo hapa meza yako impatie ili waweze kufanyia kazi waone namna ya kuwasaidia wananchi hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo ninataka niliseme hapa leo ni suala kubwa sana ambalo Kamati ya Viwanda na Biashara pia kwa kushirikiana na Kamati ya Bajeti tulileta pamoja mbele ya Mheshimiwa Spika aliyepita ilikuwa ni suala la ETS. Kwa masikitiko makubwa sana na kwa kutaka kuwasaidia Watanzania na sisi wenyewe kama Bunge, Bunge lako limedharauliwa nasi kama Wajumbe wa Kamati ya Viwanda na Biashara hatujaridhika, Serikali iliendelea mbele, wameingia mkataba na Kampuni ya SICPA tofauti na ushauri uliotolewa kwenye Kamati zile na hivi sasa wananchi wamekuwa kwenye sintofahamu kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, gharama za uendeshaji wa kampuni hii unazifahamu, katika akili ya kawaida kabisa kwa mfano, wakati huo walikuwa wanatoza mvinyo dola 20, sawa na shilingi 47,700 hata hivyo wanasema wamepunguza kutoka hiyo na sasa hivi wanatoza shilingi 42,000 wao ndiyo wanaliita punguzo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna kampuni ambazo zinaweza zikatoa huduma hiyo hiyo kwa shilingi mbili kwa maana ya dola sawa na shilingi 4,600 ndiyo maana ninakiomba Kiti chako kitoe maelekezo mahsusi kabisa ili tuweze kukaa sisi kama Wabunge tujadili jambo hili katika hatua ya dharura, tuweze kuwasaidia wananchi. Haiwezekani mtu mwenye akili ya kawaida aache kupata huduma kwa shilingi 4,600 ang’ang’anie kwenda kupata huduma ya shilingi 42,000; nini tunaficha nyuma ya mkataba wa SICPA na TRA na Serikali.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, karatasi ninazo hapa naomba na wewe uzipitie uone kama ninachokisema ni halali na kama hiki ninachokisema ninasingizia nitaomba Bunge lako liniwajibishe kwa sababu tunataka kuwasaidia wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, malengo ya kuwa na kampuni hii ilikuwa ni kutaka kuisaidia Serikali kufanya mahesabu ili TRA waweze kutoza kodi stahiki, lakini matokeo yake mzigo huu wote unahamishiwa kwa wanunuzi. Hakuna kitu chochote kinachopatikana kwa Serikali. Nilitoa mfano hapa Bungeni nikasema katika shilingi kumi ambayo inatozwa na mkandarasi anayefanya kazi ya kuhesabu, lakini mkandarasi huyu anailipa Serikali shilingi moja na senti nane kiasi kingine chote cha pesa kinachobakia kinakwenda kwake mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakuomba uelekeze, Bunge hili linadharauliwa sasa hivi, Kamati yetu ya Viwanda na Biashara imedhauriwa kwa sababu tulitoa ushauri mzuri kwa Serikali hata hivyo TRA wameendelea kuingia mkataba huu, tunataka tufahamu kama Kamati ni nani yupo nyuma ya mkataba SICPA na TRA. Kwa nini tuwapelekee wananchi mzigo mkubwa badala ya kuacha hili jambo likafanyika kama ambavyo Bunge tulishauri. Akili ya kawaida kabisa haiwezi kukubali; unakataa shilingi 4,600 unakimbilia shilingi 42,000 kwa manufaa ya nani? Nchi hii haipati shilingi moja kwa mkataba huu zaidi ya kodi inayotozwa pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, walichokifanya sasa hivi wametumia ujanja karatasi zipo hapa za TRA, wameacha kutoza kwa dola wame-convert zile pesa kwa shilingi halafu zinakwenda bado kutozwa na gharama hizi wale waendeshaji wanazileta tena kwa mlaji ambaye ni mwananchi wa kawaida na ndiyo sababu sasa bidhaa nyingi zinaweza kupata bei kwa sababu mwisho wa siku tozo hizi zinarudi kule. Sukari imepanda bei, chai kwa maana ya juice imepanda bei, soda zimepanda bei huko mtaani kwa sababu kubwa hizi na wenyewe walikuwa wakizileta kila mara.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeanza kuongea hili jambo kwa muda mrefu sana nataka sasa nitoe na mimi unisaidie kabisa, kuona kwa nini Serikali inataka kutuficha, nani yupo nyuma ya mkataba wa SICPA na TRA, kwa nini gharama hizi kubwa tunakwenda kuwahamishia wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba karatasi hizi zikufikie hapo, busara ikuongoze, uende kutusaidia na tunakuomba uje kwenye Kamati yetu ikikupendeza tutakueleza mengi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hiyo. (Makofi)