Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niunge mkono hoja kwa sababu Kamati hii ni yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo anafanya kazi vizuri na pia kwenye jimbo langu amenijengea madarasa 196. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nimshukuru na kumpongeza Mwenyekiti wetu wa Kamati kwa kuwasilisha taarifa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najikita kwenye eneo moja kulingana na dakika ambazo ni chache; eneo la watoto wanaopata mimba katika shule zetu za Sekondari na Msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naipongeza Serikali kwa jinsi ambavyo imeruhusu sasa watoto wale ambao wamepata ajali ya kupata mimba watarudi tena shuleni kusoma baada ya kuwa wanaendelea kunyonyesha. Hilo ni jambo jema na wananchi wamelifuarahia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hili isije kuonekana Serikali sasa imeruhusu mimba za shuleni. Hili ni jambo la kuangalia sana; kwamba kwanza kwenye familia zenyewe ambako hawa watoto ndiyo wanatoka, tuvunje ukimya, tuzungumze hili suala la mimba, tusiwafiche watoto wetu. Kama mwanaume utashindwa kuongea na kijana wako, basi tafuta namna ambavyo ujumbe utamfikia kijana wako, lakini kama huna uwezo wa kuongea na msichana basi tafuta hata shangazi aweze kuongea na huyu msichana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ni vizuri pia ije na mpango mwingine. Niliwahi kuzunguza wakati fulani kwenye semina nikasema Serikali ilete mtaala ambao utasababisha kufundishwa wale watoto wafikie hatua ya kujua kwamba mimba inapatikana wakati gani. Kwa sababu ile ni ajali. Ni ajali. Hakuna mtoto anayetegemea kupata mimba, hakuna. Anakwenda kusoma ilia pate elimu. Kwa nini anapata mimba; anapata mimba kwa sababu ni ajali. Na anapata mimba kwa sababu wakati mwingine hajui kwamba ile mimba anaipatapataje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa kuwa wale ni wanafunzi na wanasoma, basi wafikishwe kwenye eneo la kalenda, kwamba ukitaka kuthubutu kufanya jambo hilo, basi tarehe hii na hii usithubutu hicho kitendo. Kabisa. Kama mwenzangu aliyechangia aliposema kwamba…

T A A R I F A

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, taarifa.

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mzungumzaji kwamba kitendo cha ngono kwa mila na desturi za Mtanzania na kwa imani za dini zetu zote haipaswi mtoto kufundishwa namna ya kukifanya na kwamba kufanya hivyo ni sawa na kuhalalisha dhambi hiyo ya uzinzi. Ahsante. (Makofi)

MHE. NASHON W. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo lazima tulizungumze kwenye familia zetu lakini pia tulipeleke na shuleni. Bila kufanya hivyo Serikali itaonekana sasa kuruhusu hawa watoto waliopata mimba shuleni na warudi tena kusoma shuleni, itaonekana imehamasisha wanafunzi kupata hizo mimba. Naamini kabisa mimba zile zinapatikana kama vile ajali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niishauri Serikali; habari ya kukataa kufundisha somo hili tutakuwa tunajipotezea muda kwa sababu tunaposema kwamba kujamiiana ni dhambi, ni sawa ni dhambi, lakini lazima tufikie mahali kwamba no, usifanye ngono kipindi hiki na hiki, ndiyo. Tufike mahali hilo tuliseme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja tena. (Makofi)