Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia hoja iliyoko mbele yetu. Naomba nijielekeze kwenye eneo dogo tu ama eneo moja la michezo. Kwenye michezo changamoto kubwa tuliyonayo ni uwekezaji na uwezeshwaji hafifu wa makampuni ya taasisi za kiserikali kwenye michezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyikiti, nashauri mambo yafuatayo: Moja, Serikali ijaribu kushawishi makampuni na taasisi za kiserikali; kwenye fungu la Corporate Social Responsibility kwa kiasi kikubwa ielekezwe kwenye michezo. Mfano mzuri ni Geita Gold Mine, kwenye CSR yao wamewekeza kwenye upande wa Geita Football Club. Pia Kampuni ya Barrick imeweza kuwekeza kwenye timu ya Biashara United. Kwa hiyo, nashauri Serikali isukume makampuni hayo na taasisi za kiserikali ziweze kuelekeza CSR ziende kwenye michezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, Serikali itoe incentives kwa makampuni yote yanayowekeza kwenye michezo. Hii inafanywa sana na nchi nyingi zilizopiga hatua. Mfano, Serikali inaweza ikaamua makampuni yote yanayowekeza kwenye michezo, pale wanapokwenda kulipa Corporate Tax, basi lile fungu ambalo wamewekeza kwenye michezo lihesabiwe kwenye Corporate Tax. Hii italeta hamasa kwenye makampuni mengine yote kuweza kuwekeza kwenye mchezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa na machache tu. Naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)