Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii uliyonipatia. Vilevile nichukue nafasi hii nimshukuru Rais wetu, Mama Samia, pia nimshukuru Waziri wa Afya na Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitajikita kwenye magonjwa yasiyoambukizwa. Takwimu zinatuambia kuwa zaidi ya asilimia 40 ya Wabunge humu wamewahi kuvuta sigara, aidha kwa kukusudia au kwa kutokusudia. Vilevile kidunia takwimu inatuambia kwamba zaidi ya asilimia 70 ya vifo vinavyotokea duniani ni kwa sababu ya magonjwa yasiyoambukizwa. Kwa Tanzania, zaidi ya asilimia 40 ya vifo vinavyotokea vinasababishwa na magonjwa yasiyoambukizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivi? Tatizo la magonjwa sasa hivi ni kubwa saba. Wakati UKIMWI unaanza miaka ya 1980 tuliona ni janga kubwa sana la kitaifa, lakini naomba niseme kwamba sasa magonjwa yasiyo ya kuambikiza ikiwemo kansa, ugonjwa wa moyo pamoja na ugonjwa wa figo, ni hatari sana na ni janga la kitaifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikwambie burden ya magonjwa haya ya kuambukiza, nitatolea mfano mmoja tu kwenye ugonjwa wa figo. Wakati tunakwenda kupeleka wagonjwa wetu kutibiwa India kwa ajili ya dialysis na hususan kubadilishiwa figo tulikuwa tunatumia takribani milioni 60 kwa mgonjwa mmoja. Baada ya kuboresha huduma zetu za afya na tunamshukuru Rais, sasa hivi tunatumia takribani milioni 20, ambayo bado ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika wiki moja kuna session nne za kufanya dialysis, kusafisha figo kwa mgonjwa wa figo. Kila session moja inatumia si chini ya 200,000. Kwa hiyo, kwa wiki nzima mgonjwa wa figo anahitaji 800,000 ili afanyiwe usafishaji wa figo. Hili ni zoezi routine mpaka pale Mungu atakapomwita. Tatizo la magonjwa ya kuambikiza is a burden, ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kwamba bado takwimu, hata hii ninayoisema ya asilimia zaidi ya 40 bado iko under-reported. Kuna watu wengi sana wapo vijijini ambao wameathirika na magonjwa haya yasiyo ya kuambukizwa lakini hatujawatambua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ushauri wangu; natambua kwamba kuna initiatives mbalimbali zimechukuliwa kitaifa na kimataifa. Katika level ya kimataifa tuna Global Action Fund 2020/2025 ambayo lengo lake ni kupunguza magonjwa yasiyoambukiza kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2025. Katika ngazi ya Taifa tuna mkakati wetu wa kitaifa wa kupunguza haya magonjwa yasiyoambikiza. Tumeanzisha mwongozo wa kitaifa wa kufanya mazoezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mawili ya kushauri. La kwanza, naomba nimshauri Mheshimiwa Waziri wa Afya, tuboreshe na tuhuishe DHS2, mfumo wa kukusanya taarifa. Ule mfumo wa kukusanya taarifa una taarifa chache sana zinazoonesha watu wangapi wanaumwa magonjwa yasiyoambukizwa. Hiyo inasababisha tunatoa report ambazo ni under reported, tunaacha watu wengi sana ambao tungeweza kuwasaidia kupata huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, hili ni kwa upande wa Mheshimiwa Waziri Mkuu. Naishauri Serikali; suala la magonjwa yasiyoambikizwa ni multisectoral, ni suala mtambuka. Kuiachia Wizara ya Afya kushughulika na magonjwa yasiyoambukizwa inasababisha tunashindwa ku- deal na tatizo hili. Nishauri sasa, kwamba Mheshimiwa Waziri Mkuu alichukue hili ili liwe kwenye ofisi yake na tuanzishe tume kama tulivyoanzisha Tume ya UKIMWI ili tuweze kuratibu wadau wote ambao wanahusika katika kusaidia suala la kupambana na magonjwa yasiyoambukizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja, ahsante sana.