Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

Hon. Kassim Majaliwa Majaliwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ruangwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu kwamba nimesikiliza mjadala unaogusa maeneo ya Ngorongoro na Loliondo juu ya mahitaji makubwa ya uhifadhi wa maeneo haya kwa maslahi ya Taifa. Ni kweli upo mgongano mkubwa unaotokana na sheria tulizonazo, lakini pia matakwa binafsi ya mtu mmoja mmoja.

Mheshimiwa Spika, vile vile Mheshimiwa Rais ametoa maelekezo ya kukutana na ndugu zetu waliopo pale. Kazi hiyo tumeshaianza. Jumapili iliyopita nilianza na kazi hiyo nikakutana na Uongozi wa Mkoa wa Arusha, nimewasikiliza, nimekutana na Wizara pale Arusha, nimewasikiliza na sasa hatua iliyobaki ni kwenda Ngorongoro. Nitafanya mikutano na wananchi wa eneo la Ngorongoro, nitafanya mikutano na wananchi wa eneo la Loliondo ambako pia mwaka 2017/ 2018 tulifanya mikutano mingi sana kueleweshana juu ya jambo hili.

Mheshimiwa Spika, haya yote na mjadala unaoendelea hapa Bungeni wapo ambao wanaelewa mazingira yaliyopo kule, lakini wapo Wabunge ambao hawajui mazingira yaliyopo pale. Huku tukiwa tunazungumza na wananchi kule, naiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kufanya semina siku moja kwa Wabunge wote ili Wizara iwaambie kuna nini kule Ngorongoro? Nini kilikuwepo awali na ni hali gani ambayo ipo sasa? Hii itasaidia tuwe na uelewa wa pamoja hata haya mapendekezo ya Mheshimiwa Waziri ya kutaka kuja kubadilisha sheria, mnaweza kuunga mkono au kutokuunga mkono baada ya kujua nini kinaendelea kule? Hatua hii ndiyo itawezesha kuendesha zoezi hili kwa amani kabisa kadri itakavyokuwa imeamriwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiyo ndiyo njia sahihi ambayo pia niliona nipate muda huu niweze kutoa maelekezo kwa Wizara na pia Wabunge mpate kuelewa jambo hili. Tutakwenda kwa wananchi; tumeanza kwa hatua hizo ambazo nimezieleza, tumzungumza na Wizara, tumezungumza na Mkoa ambao unasimamia jambo hili ambapo pia TAWA, TANAPA pamoja na Ngorongoro walikuwepo, na hao sasa nawataka kupitia Wizara waje hapa Bungeni wawaelimishe Wabunge, mjue mazingira yaliyopo pale. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ili kumaliza jambo hili, kwa kadri ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais ya kutatua tatizo hili bila kuwa na mgongano kati ya wananchi walipo pale na maamuzi ambayo yanaweza kufikiwa, lazima tukae pamoja ili tuweze kumaliza.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa na hayo tu. (Makofi)