Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia mada iliyoko mezani hapo na nimshukuru Mungu kuweza kuwepo mjengoni mwaka huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiiti, nimepitia review ya mwaka 2014/2015, vilevile ya mwaka huu wa sasa ambao tunauzungumzia. Kimsingi, tumekuwa na malengo mengi ambayo hayapimiki na nina maana gani ninaposema hayapimiki? Unakuta kwa mfano, mapitio ya mwaka jana tumesema tuta-train walimu 460, lakini hatuambiwi katika ule mwaka ni wangapi wamekuwa trained. Kwa hiyo, tunashindwa kujua sasa, hawa waliokuwa trained ni wangapi na mmeshindwa wapi kwa wale ambao hatukufanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile hata ukipitia huu Mpango wa sasa hivi ambao Mheshimiwa Waziri ameuleta, bado tatizo liko pale pale, anazungumzia kusomesha vijana wengi kwa mkupuo katika fani mbalimbali, lakini hasemi anafundisha vijana wangapi, wa fani zipi na kwa mchanganuo upi. Kwa hiyo, napendekeza kwamba katika Mpango utakaoletwa yale malengo yawe bayana, yaweze kupimika kusudi tuweze kuisimamia Serikali kwa jinsi ambavyo inatenda kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Mpango umezungumzia suala la viwanda, tunataka Tanzania iwe nchi ya uchumi wa viwanda, lakini suala la rasilimali watu halijajitokeza bayana. Kwa sababu kama ni viwanda tutahitaji fani mbalimbali za kuweza kusukuma hili gurudumu la viwanda, lakini Serikali haijaleta mchanganuo wa fani zipi ambazo tutazihitaji kwa ajili ya huu uchumi wa viwanda.
Kwa hiyo, ni ushauri wangu Serikali ikachambue, ikaangalie kwa miaka kumi ijayo tunahitaji human capital gani, katika maeneo gani kusudi kila mwaka mpango wa mwaka unapoletwa hapa muweze kuainisha kwamba, mwaka huu Serikali itafanya hiki, mwaka wa kesho Serikali itafanya hiki, kusudi Bunge liweze kufuatilia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika Mpango huu ambao Mheshimiwa Waziri ameuwasilisha, kwa maoni yangu mimi kama Mbunge wa Chadema, vipaumbele ni vingi, wala havitatekelezeka. Kwa mfano, katika ukurasa wa 25, Ardhi na Makazi. Tumesema upimaji na utoaji hati miliki, naomba muangalie hivyo vipaumbele vya Ardhi, Nyumba na Makazi; hivi kwa mwaka huu hatuwezi kuvifanya, haviwezi kufanyika wala havipimiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, tunataka Serikali ije na mchanganuo. Kwa mfano, anasema watapima majiji na vijiji na miji mikubwa. Sasa Serikali ituambie katika majiji, miji na vijiji ni vingapi? Ni mji mmoja, ni miji miwili, ni vijiji kumi kusudi itakapokuja taarifa ya utekelezaji tujue kama kazi hiyo imefanyika au haijafanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumzia kuhusu rasilimali watu. Kama kweli tunataka kupata rasilimali watu ambayo itasaidia, Serikali katika kujenga uchumi huu, basi rasilimali watu hii iangaliwe tangu mwanzo. Waziri wa Elimu aangalie laboratories ngapi zinajengwa kwenye mashule, maana ndiko tunakochimbua wataalam ambao baadaye watakuja kusukuma huu uchumi wa kati ambao tunauzungumzia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye suala la kilimo. Serikali imesema kilimo ni uti wa mgongo, ni kweli, lakini je, Serikali inafanya nini kweli kusimamia kilimo? Kwa sababu lazima tukubali, kilimo nchi hii bado ni subsistence farming. Kwa hiyo, wakulima wanatakiwa kuangaliwa kwa jicho la karibu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Serikali haijazungumzia kuhusu Extension Officers. Extension Officers wanahitajika wengi na ingependeza kama Serikali ingekuja kuangalia ratio ya Extension Officer na wakulima, kama tunavyofanya ratio ya madaktari na wagonjwa, nesi na wagonjwa, kwa hiyo na Extension Officers ifanywe hivyo hivyo, kusudi muweze kufanikiwa katika kuinua kilimo ambacho pia kinatoa ajira kwa watu wengi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa ushauri kwa Serikali; Wizara ya Kilimo, SUA na Vyuo vya Kilimo na mkulima wafanye kazi kwa pamoja (tripartite). Watu wa ugani wawezeshwe kwa vifaa, wawezeshwe kwa pikipiki, waweze kwenda kutembelea wakulima na wawe na mafaili kama ya wagonjwa hospitali. Nchi nyingine ndivyo wanavyofanya, unakuta Afisa Ugani anawajua wakulima wake kwa jina na ana file analokwenda kuangalia wakulima wake na kujua matatizo yao. Naishauri Serikali ichukue mapendekezo hayo ili iweze kwenda kuyafanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la viwanda tunavyo viwanda vingi na vingi vimekufaa. Serikali inahitajika kuangalia viwanda katika maeneo mbalimbali, kwa mfano, Tanga kuna matunda mengi sana, kiwepo kiwanda pale Tanga cha ku-process matunda. Mahali kama Shinyanga kuna nyama nyingi, ng‟ombe wengi sana, kuna pamba nyingi sana, viwepo viwanda vya ku-process vitu hivi ili itoe ajira na kukuza uchumi wa nchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)