Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee nikushukuru sana kwa kunipa hii nafasi. Lakini nitumie nafasi hii vilevile kumpongeza sana Rais wetu, mama Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa sana ambayo anaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunatambua kwamba Corona ilikuwa ni janga kubwa lakini mama yetu amekuwa jasiri sasa hivi tuna chanjo Tanzania. Wote tunatambua kwamba Corona imeleta madhara mengi lakini mama yetu ame-fight akapata fedha za UVIKO kutoka IMF na sasa hivi tuna fedha za kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wote tunatambua kwamba Tanzania ilianza kusahaulika. Mama yetu sasa hivi anaifungua, sasa hivi Tanzania inajulikana nchi za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii vilevile kumpongeza sana ndugu yangu, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, pamoja na Naibu Waziri wake kwa kazi ambayo wanaifanya. Nikushukuru sana Waziri kwa kazi mnayoifanya na kuleta rasimu ya huu mpango. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ina mambo matatu ambayo ninapenda kuishauri Serikali. Jambo la kwanza, ninapenda kuishauri Serikali kwenye mfumo wa kukamilisha miradi mikubwa ya maji; la pili, ninapenda kuishauri Serikali kuhusu huduma za afya, hususan paradox iliyopo kati ya zahanati na vituo vya afya; jambo la tatu, ninapenda kuishauri Serikali kuhusu mfumo mzuri wa kutoa mikopo ya elimu ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais wetu, mama Samia Suluhu Hassan. Kwa upande wangu mimi Jimbo la Manyoni Mashariki nina mradi mkubwa sana wa maji wa Kintinku – Lusilile wa takribani bilioni 11, mpaka sasa tumepewa takribani bilioni tano. Na mwaka huu wamenitengea bilioni 2.4 na juzi hela za UVIKO ametupatia takribani milioni 500 kwa ajili ya kukamilisha huu mradi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la miradi ya maji nina hoja takribani tatu. Hoja ya kwanza ni kwamba tuna miradi mikubwa ya maji lakini tunatumia muda mrefu sana kuikamilisha. Nitatolea mfano mdogo wa mradi wangu wa Kintinku; mpaka sasa hivi tumesha-spend fifty percent ya bajeti ya eleven billion. Ile fifty percent imeshakaa zaidi ya miaka mitatu. Hiyo ni sunk cost, maana yake kuna wear and tear ambayo inaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kushauri kwenye hili. Cha kwanza, natamani kuona ni jinsi gani Wizara inaweza ikaja na modality mpya ya kuhakikisha kwamba tunakamilisha hii miradi ya maji kwa wakati. Ninapenda kumshauri Waziri mambo yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Nchi za Malaysia, Uturuki, hata Indonesia wanachofanya wameingia kwenye Public Private Partnership na manufacturers wa mabomba. Wanachofanya kwa sababu sisi tunajua kwamba tuna changamoto ya ku-raise hela kwa kutumia taxation, tunahitaji ku-tax ili tu-spend, kinachofanyika hapa, Serikali inaingia kwenye long-term agreement na manufacturers wa mabomba, then tunakuwa tunawalipa by installments.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo tutakuwa na uhakika kwamba tunaweza tukakamilisha utekelezaji wa hii miradi ya maji ambayo kwa kweli inaweza ikawa na impact kubwa sana. Na kwa kupitia hilo vilevile tunaweza tukaweka incentive. Tunaweka incentive vipi; incentive ya kwanza tunaweza tukawa-exempt hawa manufactures kwa sababu wana-import raw material kutoka nje, wawe na zero tax kwenye importation ya raw material. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hii vilevile ita-facilitate viwanda vyetu vya ndani vitakuwa, tutakuza ajira, lakini vilevile tutapunguza ile profit margin ambayo wanaweza wakai-set kwa sababu ya ile payment schedule ambayo tunaweza tukawa tunawalipa hawa manufacturers. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kwenye hili ni kwamba kama tutaenda na huu mfumo wa kutumia private sector waweze kuingia hiyo long-term agreement na Serikali, bado tunaweza tuka-opt kutumia ile force account kwa sababu tayari tutakuwa tuna uhakika wa kupata mabomba, tuna uhakika wa kupata fittings na tunaweza tukatumia force account ili kuhakikisha kwamba tunapunguza tatizo la kutokamilisha miradi kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri huu utaisaidia Serikali kukamilisha miradi mikubwa ya maji ukiwepo Mradi wa Kintinku – Lusilile ambao sasa hivi ni mradi wa zaidi ya miaka 15, bado tunasuasua kuukamilisha. Nina imani kabisa kwamba approach hii itakwenda kuisaidia Serikali.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kushauri upande wa afya. Mimi nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais. Sisi kwa upande wa Jimbo la Manyoni Mashariki kwanza ametupatia milioni 250 za fedha za tozo ambazo tunakwenda kukamilisha Kituo cha Afya cha Chibumagwa, lakini vilevile tunaanza ujenzi wa Kituo kipya cha Afya cha Sanza. Mbali ya hiyo, kwenye hela za UVIKO ametupatia takribani milioni 300, tunakwenda kujenga jengo la dharura. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mimi nina ishu kubwa mbili upande wa afya. Ishu ya kwanza Sera yetu ya Afya ilikuwa inasema kwamba kila kata tunahitaji kujenga kituo cha afya, lakini kila kijiji tunahitaji kuwa na zahanati. Kulingana na uwezo wa Serikali nadhani suala la kujenga kituo cha afya kila kata sasa hivi siyo wazo ambalo ni realistic. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri nini; la kwanza, mimi naomba nishauri kwamba hatuhitaji kujenga kituo cha afya kila kata, zaidi tunahitaji kujenga vituo vya afya vya kimkakati. Na hivi vituo vya afya viwe clustered ili Serikali iwe kwanza na uwezo wa kupeleka watumishi pale, lakini iwe na uwezo wa kupeleka vifaa, lakini vilevile tutakuwa na uwezo hata wa kusaidia…

MWENYEKITI: Kengele ya kwanza hiyo.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la zahanati; zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania wanaishi vijijini. Demand kubwa upande wa afya ipo kwenye zahanati kuliko iliyopo kwenye vituo vya afya. Vituo vya afya ni referral point, mtu akishindwa kwenye zahanati anakuwa referred kwenda kwenye kituo cha afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo najua utaratibu wa Serikali ni kwamba kila mwaka tunatenga takribani zahanati tatu kwa kila jimbo. Kwa upande wangu na maono yangu naona kwamba zahanati tatu kwa kila jimbo ni chache sana, na kwa sababu tunataka kuhakikisha tunafikisha huduma za afya karibu na wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni nini? Kwanza tunahitaji ku-invest zaidi kwenye zahanati tuongeze zahanati sasa kutoka tatu kwenda angalau sita kila jimbo kila mwaka, lakini kama nilivyoshauri kwamba tutakuwa na zile clustered health facilities ambazo sasa angalau kata tatu zitajengewa kituo cha afya kimoja ili ziwe referral points kwa ajili ya wale wanaotoka kwenye zahanati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la mikopo ya elimu ya juu. Katika wiki mbili hizi Wabunge wengi tumepokea simu nyingi sana za vijana wetu ambao wamekwenda vyuo vikuu, na katika hili niseme bado ule mfumo wetu wa means testing wa kuwachuja vijana ambao wana uhitaji mimi nauona bado una mapungufu makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hili niseme kwa sabbau gani; bado tunapata simu nyingi za vijana wetu ambao wanatoka kwenye maeneo yetu ambao tunajua kabisa ni watoto wa maskini lakini bado hawajapata mikopo. Na tatizo lililopo vilevile ule mfumo ni very bureaucratic, mtoto wa kijijini ambako mtandao haujafika anatakiwa a-upload, a-apply na aweke documents zote kwenye mfumo. Mimi nashauri mfumo huu ufanyiwe marekebisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ni marekebisho gani nashauri; kwanza nashauri tuachane na huu mfumo wa means testing. Na ningeshauri mambo matatu; la kwanza, tuje na mfumo wa category, tuwe na categories tano, category ya kwanza kwa wale wanafunzi waliosoma shule za Serikali form four na form six hawa ningeshauri wapewe mkopo asilimia 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, category ya pili ni wale wanafunzi waliosoma kidato cha nne…

MWENYEKITI: Kengele ya pili hiyo.

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, mimi nikushukuru sana na ninaunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)