Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

Hon. Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Viwango vya Afya ya Mimea, Wanyama na Usalama wa Chakula

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nitazungumza kwa kifupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza natoa shukrani sana kwa Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji, kwa sababu wakati wa kuwasilisha kwa kweli walitukalisha chini kweli kweli, walichambua Itifaki kwa undani kweli kweli, waliuliza maswali mengi sana, walitaka tuwahakikishie kila kitu na maslahi ya nchi yetu yapo wapi, tunashukuru tulielewana nasi kwa upande wetu tunachukua ushauri wao wote nita- highlight baadhi ya vitu ambavyo wamevizungumza hapa. (Makofi

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hesabu zangu za haraka haraka tumekuwa na wachangiaji 16 na wote wameunga mkono hoja na wametoa ushauri ambao ni muhimu sana kwetu kuuchukua. Sasa niweke kwa muhtasari mambo makubwa nitajaribu ku- highlight vitu vichache sidhani kama nitahitaji muda wote ambao umewekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kama kila mtu alivyosema Itifaki hii ni muhimu sana kwetu. Kwanza kwa sababu inatuwezesha sisi kufanya biashara, kuuza nje hapa tunazungumza changamoto ya soko, changamoto kubwa ya soko la mahindi, changamoto kubwa ya soko la mchele na tunazungumzia mboga mboga, na tuliona hapa karibuni tatizo la watu kutoa tafsiri kuhusu usalama wa mahindi yetu. Kuwa na itifaki kama hii kama walivyosema baadhi ya Wabunge, ambayo inatupa vigezo ambavyo vinapimika na vya uwazi za kuhakikisha kwamba hatudanganyani kama nia ya kuzuia biashara yetu isifanyike kutatusaidia sisi kuendelea kutumia soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki vizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hakika na nadhani wamezungumza baadhi ya Wabunge hapa, sisi ndiyo wauzaji wakubwa wa mazao ya chakula katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo, sisi kwa hakika ndiyo tunastahili zaidi kuisimamia Itifaki hii ili uweze kuwa na mafanikio kwa hiyo hilo ni moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili; hii Itifaki nayo inatuhakikishia usalama wa vile vinavyoingia hapa nchini kwetu, kwa sababu ni vigezo vya kuhakikisha usalama wa vitu vinavyoingia. Kwa hiyo, kwa kusaini hivi na kudhibiti kwamba nchi jirani kwenye Jumuiya hii haziingizi vitu ambavyo vikivuka kwanye mpaka vinakuja kuumiza afya ya watu wetu, tunakuwa tunajilinda na tunalinda watu wetu, kwa hiyo ni Itifaki ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuwa na Itifaki hii inatukumbusha kuendelea kuboresha ubora na usalama wa bidhaa zetu kwa sababu bado tunahitaji masoko ya Ulaya, na kote kuna SPS, kinachozuia sana kuingia masoko ya Ulaya Marekani kwa sababu viwango vyao viko juu sana, walau tunajiwekea viwango sasa hivi vya kwenda mbele na kuhakikisha kwamba baadaye tunaweza tukaongeza ubora wetu na kuuza nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa na la muhumu ni kwamba tayari Tanzania ni signatory ni member wa WTO, na Itifaki ya namna ipo katika agreement ambazo tunazo kwenye WTO. WTO ndiyo inasema nchi mkiwa pamoja na mazingira yanayofanana mnaweza mka- customize na ku-localize agreement ambayo tayari iko WTO. Kwa hiyo, hata kama tusinge saini Itifaki hii bado tunabanwa na itifaki WTO ambayo sisi ni member.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulichofanya sasa ni kuhakikisha kwamba tunazungumza na wenzetu, kwa mfano tu, kwenye Itifaki inasema lazima tubadilishane taarifa kwamba ni taasisi gani huko Tanzania itakuwa inahakiki usalama na taasisi gani ya Kenya, taasisi gani ya Uganda, na kadhalika. Kwa hiyo, hata mfanyabiashara anakuwa na uhakika nasi tunakuwa na uhakika unapotaka kuuza bidhaa zako katika nchi hizo unapitia upande gani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Itifaki imechukua miaka minane na sehemu mojawapo ni kwa sababu kulikuwa na mjadala mrefu na kila mtu na kila taasisi imetaka kujihakikishia na baada ya pale ikaonekana umuhimu wa kutunga sheria ambayo ilitungwa mwaka jana ya afya ya mimea kuhakikisha baadaye tutakaporidhia hii tutakuwa tumeajiandaa vizuri. Sisi kwa upande wa kilimo tunaita, sheria ambayo tulitunga mwaka jana ambayo inaitwa Plant Health No. 4, 2020 ambayo imeanzisha taasisi inaitwa Tanzania Plant Health and Pesticides Authority (TPHPA), ambayo ni Taasisi muhimu kwa ajili ya shughuli za SPS.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzetu wa upande wa Mifugo na Uvuvi tayari walikuwa na sheria nyingi ambazo ametueleza Naibu Waziri hapa kwa ajili ya shughuli hizo hizo. Kwa hiyo, baada ya kuchukua miaka minane sasa hivi tunajua kabisa tumejiandaa vizuri sana na kila taasisi na kila mdau aliyekuwa na shaka ana uhakika kwamba tumezingatia maslahi na msimamo wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya mambo ambayo yamezungumzwa na Kamati yetu ni kwamba lazima tujenge uwezo na ni kweli, wa maabara yetu na kuongeza uwezo wa kupima kwa haraka, tunakubali. Jambo kubwa ambalo pengine baadhi ya watu wanalitilia shaka ni juu ya suala la GMO, humu ndani Itifaki haisemi kwamba tutaruhusu bidhaa za GMO, kilichosemwa ni kwamba tutakaa chini na kuweka utaratibu na sheria na masimamo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu GMO.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuna msimamo wetu na tunapokwenda kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki hakuna kinachopita bila kukubaliana wote. Tanzania hatuna sababu na hatuna nia ya kutetereka kuhusu msimamo wetu wa GMO.

Kwa hiyo, tutakapokaa mezani kuweka msimamo, msimamo wa Tanzania lazima tuhakikishe kwamba ndiyo msimamo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo hakuna sababu ya kuwa na wasiwasi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, suala jingine ni kuwa kulikuwa na wasiwasi baadhi ya watu walihisi kwamba kwa sababu ukisoma inasema hii ni kwa ajili ya kutujengea mkakati wa pamoja ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao vilevile utatuongoza sisi kushughulika na Jumuiya nyingine, baadhi ya watu wakadhani kwamba maana yake kwamba ni kushughulika na EPA. Ukweli ni kwamba unapokuwa na Trade Block, mnapokubaliana taratibu zenu, zile taratibu zinatumika vilevile ninyi kufanya biashara na nchi nyingine na blocks nyingine bila kujali EPA. Kwa hiyo, watu walikuwa na wasiwasi kwamba ni EPA lakini siyo kabisa haina uhusiano wa namna yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vyovyote vile standard za SPS za Ulaya ni kubwa kweli ndiyo maana tunapata shida sana kuuza vyakula vyetu katika Jumuiya ile ya Ulaya. Kwa hiyo ingekuwa tunafanya hivyo kwa sababu ya EPA hizi standard wala sisi wengine tusingeziweza katika nchi za East Africa Community. Kwa hiyo, watu wengi wameliona hilo, taasisi mbalimbali zimeona na zimeridhika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo mengine ambayo tumeambiwa hapa kwenye kujenga uwezo tunakubali sana, mimi nadhani yote tu kwa sababu discussion yote ilikuwa ni positive. Kwa hiyo, ninapenda kuchukua muda huu kutoa shukrani nyingi sana kwa Kamati inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, ametuongoza vizuri sana, na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Almas Maige na Wajumbe wote wa Kamati, kwa sababu product hii ni pamoja na mchujo na majibizano na scrutiny niliyofanya na Kamati na ninashukuru wamekuwa wa kwanza kuanza kuelezea msimamo wa Serikali, nawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.