Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. SAADA MANSOUR HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumshukuru Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na Mawaziri wote kwa ushirikiano wao leo wameweza kupunguza kodi ya asilimia sita kwenye mkopo ya elimu ya juu, maana wazazi tumepata nafuu kwa msaada huu tuliopewa kwa watoto wetu kutoka kwa huruma na mapenzi ya mama yetu Mama Samia.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia sisi Wabunge wote tumefarajika sana kuona Madiwani, Maafisa Tarafa na Watendaji wa Kata kwa kupewa posho kila mwezi kupitia kwenye account zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili suala la posho kwa watendaji wenzetu limetupa faraja sana sisi Wabunge maana kusema kweli walikuwa na hali ngumu sana ya utendaji wao wa majukumu yao wakati wao ndio wapo na wananchi muda mwingi kuliko sisi Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kuwakumbuka wastaafu kulipwa kwa wakati, kwani wastaafu wengine wanafariki wakati haki yake hajaipata, anakuja kulipwa mrithi yeye aliyetumikia ajira hajaigusa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kupunguza muda wa mikataba ya Jeshi la Polisi kutoka miaka 12 hadi miaka sita, hii tutafanya askari wetu waendelee kuilinda amani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia niaishukuru Serikali kwa kuamua sasa tozo ya viza ya wageni wanaoingia Zanzibar ibaki Zanzibar na Tanzania Bara ibaki Bara hii imepunguza kero za Muungano.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru viongozi wetu wote mama yetu kipenzi Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, Mheshimiwa Dkt. Hussein Mwinyi, Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Mheshimiwa Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba na Mawaziri wote kwa kazi nzuri ya kutuogoza na kulitumikia Taifa letu na wananchi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia naishukuru Serikali kwa kurejesha VAT kwenye bidhaa zinazonunuliwa Tanzania Bara na kutumika Tanzania Zanzibar. Pia naipongeza Serikali kwa kuondoa kero kwa vijana wetu waendesha pikipiki (bodaboda) kwa kupunguza faini ya makosa ya barabarani kutoka shilingi 30,000 hadi shilingi 10,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.