Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, natoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia natoa pongezi kwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Hussem Ali Mwinyi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia kuhusu uvuvi wa bahari kuu. Mnamo mwaka 1980 kilikuwepo chuo kinachofundisha somo la fisheries, hili somo ni zuri sana kwa sababu wananchi wetu itapelekea kupata ajira na kupelekea kupunguza umaskini na kuwezesha viwanda katika uchumi wa bluu. Wananchi wa Tanzania ni wavuvi ambao wamekulia katika mazingira ya uvuvi ipo haja Tanzania kuwa na wataalamu wa uvuvi. Naomba kuishauri Serikali ya Tanzania kushiriki katika uchumi wa bluu kwa kufanya yafuatayo; kwanza kuweka mazingira mazuri ya kuwawezesha kupata vibali vya ajira ili itusaidie kupunguza umaskini kwa namna moja au nyingine. Pia naishauri Serikali iweze kuweka njia ya kuwafundisha vijana wetu na kufufua rasilimali zetu na kutumika. Kwa mfano kuweka ufugaji wa kaa/majongoo/samaki na kadhalika na pia tuweke vizimba kwa wingi vya mazao ya baharini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunanunua meli za uvuvi lakini hatujajiandaa na wataalamu wa uvuvi wa bluu. Pia kwa sasa naomba kuishauri Serikali kwamba Chuo cha Uvuvi kijengwe Zanzibar kwa sababu Zanzibar imezungukwa na bahari na mikoa yake yote ina pwani na mikoa ya nyanda za juu.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali inawasaidiaje vijana ili kuwawezesha na kuwashirikisha katika uchumi wa bluu? Naomba kuiomba Serikali tuweke mazingira mazuri ili kuwezesha wananchi kupata mitaji ili waweze kushiriki katika uchumi wa bluu na pia kupata pesa za kigeni, kupunguza umaskini na kukuza utalii wetu. Ahsante.