Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, mambo machache muhimu naomba yazingatiwe kama ifuatavyo; kwanza bajeti ya kilimo iongezwe kwani kiasi cha fedha kilichotengwa kwa sasa hakiwezi kukidhi kuleta mageuzi kwenye kilimo.

Vilevile mpango mkakati wa kuongeza uzalishaji wa alizeti katika mikoa ya Singida, Dodoma na Simiyu uliozinduliwa Singida hivi karibuni na Waziri Mkuu utekelezwe kwa vitendo na uwe endelevu, isiwe ni jambo la mwaka huu kwa sababu ya upungufu wa mafuta, lakini liwe endelevu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili ni kuhusu posho za Madiwani; naipongeza sana Serikali kwa utaratibu iliopendekeza wa kuwalipa Madiwani kupitia Serikali Kuu na moja kwa moja kwenye akaunti zao. Ushauri ni kwamba ni vyema kiwango wanacholipwa kiongezeke kutoka shilingi 350,000 hadi shilingi milioni moja au 700,000 kwa mwezi kwani Diwani ndio msimamizi wa miradi yote ya maendeleo inayokwenda kwenye kata yake ambayo ni ya mamilioni ya fedha, kumuacha Diwani akilia njaa huku anasimamia miradi mikubwa ya maendeleo haileti picha nzuri. Anaweza kushawishika kuhujumu au kuingia kwenye upigaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Diwani ndio msimamizi wa wataalam wote kwenye kata yake. Anahitajika awe vizuri kiuchumi ili aweze kuifanya kazi hii kwa ukamilifu. Pia Diwani ndio anaishi na jamii, matatizo yote yanaelekezwa kwake, akiwa na posho ya milioni moja ataweza kusaidia jamii na kuisemea ipasavyo Serikali hapo kwenye eneo lake.

Mheshimiwa Naibu Spika, shilingi laki moja kwa Maafisa Tarafa; napongeza sana hatua hii ya Serikali kuwapatia shilingi laki moja Maafisa Tarafa kila mwezi. Hata hivyo kumejitokeza manyanyaso kutoka kwa ma-DAS wakisema kuwa sasa watasitisha kuwapa posho za mafuta ya pikipiki na matengenezo (OC) kati ya shilingi 50,000 hadi shilingi 250,000 au mafuta ya petroli lita 50 walizokuwa wanawapatia Maafisa Tarafa hapo awali.

Naomba katika majibu ya Waziri alitolee ufafanuzi jambo hili na kukemea kauli na matendo wanayoanza kuoneshwa na ma-DAS dhidi ya Maafisa Tarafa kuwa watasitisha kutoa zile walizokuwa wanawapa. Naomba hii ifahamike na itajwe na Waziri kuwa ni ku-top up ile posho waliyokuwa wanapewa ili kuboresha utendaji kazi wao. Jambo hili limejitokeza kwa Wilaya ya Singida ambapo Maafisa Tarafa wameanza kutishiwa/kuacha kupewa posho/ oc waliyokuwa wanapewa hapo awali.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa uwasilishaji na jinsi anavyoendelea ku-fit katika nafasi yake.