Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba leo tena niendelee kuishauri Serikali kwa jambo lake zuri sana la kuweka tozo ya shilingi 100 kwenye mafuta, naomba Serikali iende mbali zaidi kwa kuiwekea wigo fedha hizi ili ziwe kwa ajili ya TARURA tu yaani ziwe ring fenced kama ilivyo kwa fedha za mafuta hata zile za miamala ya simu nazo zielekezwe moja kwa moja (RUASA) maji vijijini na zile za line za simu zielekezwe moja kwa moja maji mijini, kuliko ilivyo sasa fedha hizi zote ziko tu hewani hazijawa ring fenced, hivyo kufanya rahisi kutumika nje ya makusudio.