Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mchango mfupi wa mdomo, napenda nisisitize juu ya uwekezaji kwenye ardhi. Inakisiwa kuwa ifikapo mwaka 2050 dunia itakuwa na watu wapatao bilioni 9.7. Watu wote hawa watahitaji kula, hivyo watahitaji ardhi kwa ajili ya kilimo. Nchi yetu haina umakini wa kutosha namna tunavyowapa wageni ardhi. Wawekezaji wengi wanakuja tunawauzia ardhi kwa maana kuitumia kwa shughuli za kilimo kwa miaka 33, 66 au 99.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania kihistoria haina ardhi tupu. Aidha, itakuwa inamilikiwa na familia, koo fulani au Serikali za vijiji. Mara nyingi wakija hawa wawekezaji tunazichua ardhi hizi kutoka kwa watu wanaohodhi na kuwapa wawekezaji kwa bei ndogo sana na kwa kuwa maeneo ya uwekezaji kwenye ardhi yanazidi kupungua, tusipozingatia tutakuja kujikuta ardhi imekwisha na kundi kubwa vijijini litabaki bila ardhi na hii inaweza kuwa hatari kwa usalama na usitawi wa watu na Taifa lao.

Napendekeza itungwe sheria au miongozo ya kusaidia Watanzania wabaki na ardhi yao ila itambuliwe mahali ilipo, inamilikiwa na nani na kiasi gani na inafaa kwa kilimo cha mazao gani. Mwekezaji akija tumwambie ardhi ya uwekezaji ipo mfano Kalenga ni eka kadhaa inamilikiwa na kijiji au watu binafsi. Unakaribishwa kuwekeza ila ardhi sio yako ingawa unaruhusiwa kuwekeza mfano kwa miaka 40 lakini tutamiliki kwa hisa ardhi hiyo wewe mgeni chukua asilimia 80 kwa kuwa unaleta pesa na ujuzi na kijiji au mtu binafsi wachukue asilimia 20 ya mazao au faida inayotokana na mazao hayo. Jambo hili niliona muhimu sana, litavijengea uwezo vijiji vyetu na watu wetu, itaimarisha uchumi wa vijiji na watu wake. Nimeangalia muundo wa Dubai (Dubai Land for Equity). Alichotakiwa kuwa nacho Mdubai ni ardhi tu iliyopimwa. Wawekezaji walikwenda kutoka Ulaya, Marekani na kwingineko. Iwe hivyo kwenye ardhi yetu kwa faida ya nchi yetu na watu wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawasilisha.