Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwanza kabisa nami nitoe shukrani nyingi sana kwa Serikali kwa kuweza kutoa fedha kwa kila jimbo kwa maana ya kupeleka fedha TARURA shilingi milioni 500 kwa kila jimbo hongereni sana na ninawashukuruni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa muda ni mdogo nitataja mambo kwa juu juu tu, ninachokiomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye upande wa Kilimo kuna mpango wa kilimo Agricultural Sector Development Programme, mpango huu ni mzuri sana umeelezea namna ya kuongeza uzalishaji, imeongelea namna ya kuweza kufanya processing kwa mazao yetu ya kilimo, ni namna gani ya kuweza kufanya packaging, namna gani ya kuuza na kufanya masuala yote ya environmental protection haya mambo ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wa Fedha habari tulizonazo sisi Wabunge na taarifa tulizonazo mpango huu hamuupi fedha, kama hamuupi fedha tutaendelea kupiga kelele siku zote hapa tunaongeza kilimo tuongeze kilimo, tuongeze uzalishaji kama ASDP Phase II hamuipi fedha tutakuwa tunaendelea kupiga mark time, naomba muwapelekee Wizara ya Kilimo fedha mpango huu uweze kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa utalii ongezeni matangazo, utalii wetu hautangazwi na kibaya zaidi, Waziri humu wa Utalii ulishawahi kusema vivutio tulivyonavyo sisi ni vingi hatuna haja ya kutangaza, tangazeni tunataka biashara ya utalii iongezeke katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, China ina 1.7 bilioni population ya watu wa China, mkitangazia watu wa China mkapeleka matangazo kwenye CCTV ya China 1.7 bilioni population wakisikia watu nusu ni milioni zaidi ya 800 watakuwa wamesikia habari hiyo, wakasikia na kuelewa nusu yao ni milioni 400 nusu yao wakaamua kuja kutembelea Tanzania ni milioni 200, nusu yao wakafanikiwa kufika Tanzania ni milioni 100, mkitangaza China tu tumeongeza idadi ya watalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo mnasema hakuna haja ya kuongeza kufanya matangazo ya utalii, nawashukuru Simba mmekwenda mbele, mmekwenda kwenye mashindano makubwa mmeandika visit Tanzania hiyo ni hatua nzuri endeleeni kutoa matangazo ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya elimu Mulugo ameongelea kuhusu mambo ya PPP nendeni kwenye PPP. Watoto wanaokwenda kumaliza darasa la saba ni wengi hatutaweza kuwa accommodate watoto kwenye madarasa tuliyonayo ya Sekondari muwa-involve private sector watusaidie na kazi ni nyepesi tu, kama mtoto anagharama tunamgharamia fedha inatoka BOT inakwenda kwenye shule za msingi na sekondari kuna gharama ya kila mtoto, gharama hiyo pelekeni kwenye shule ya Serikali na gharama hiyo hiyo wapeni watu binafsi wata-accommodate hawa watoto wawafundishe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa afya ndugu yangu hapa Mheshimiwa Shigongo kaongea vizuri kwenye preventive measures, preventive medicine, mama yangu hapa Mheshimiwa Dkt. Gwajima anakuja kuomba siku zote anaomba bajeti ya tiba, mishahara na kununua vifaa tiba pprevention haipo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Ofisi ya Waziri Mkuu isimamie suala la prevention kuna tatizo kubwa na non-communicable diseases limeongezeka sana bila utaratibu na uratibu wa Waziri Mkuu hatuwezi kufanikiwa wananchi wetu wanakwenda kupotea kwa sababu ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza, vyanzo vya vifo ni zaidi ya asilimia 36 tunapata vifo kutokana na non-communicable diseases. Ukiangalia ni magonjwa ya kisukari, magonjwa ya moyo na magonjwa ya kansa pamoja na ajali, tunaomba sana uratibu wa Waziri Mkuu katika kuhakikisha tunawanusuru Watanzania kutokana na majanga ya magonjwa yasiyokuwa kuambukiza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho bandari yetu ninasoma mipango ya uchumi siku zote. Upande wa bandari yetu ni kubwa ina uwezo wa kupakia tani nyingi sana kushusha na kupakia, lakini hatuna ujenzi wa meli kubwa ya kupeleka bidhaa abroad, kupeleka nje ya Tanzania. Tumekalia kuzungumzia bandari ujenzi wa meli, meli ndogo ndogo Ziwa Victoria, Ziwa Nyasa, Ziwa sijui Tanganyika, tuamue sasa kujenga na meli kubwa ya kupeleka bidhaa nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada kusema hayo naunga mkono hoja ahsante sana kwa kunipa nafasi (Makofi)