Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuchangia katika bajeti ya Serikali ya mwaka 2021/2022. Awali ya yote nimpongeze sana mama yetu Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuijenga nchi yetu na kuwaletea maendeleo watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika moja ya hotuba zake Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1962 alisema to build this country we have to make many changes. And to change it we must be willing to try what is new. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawapongeza sana Wizara ya Fedha wamekuja na mambo mengi mapya bajeti yetu kwa mwaka wa jana kutoka trilioni 34 sasa trilioni 36 hongereni sana. Lakini kuna mabadiliko mengi tumeyaona wamekuja na mapendekezo mengi mazuri na mimi naamiini kama Waingereza wanavyosema where there is a will there is a way. (Makof)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kazi yetu sisi Wabunge ni kuwachangia kuwaonyesha njia ni kuwashauri nimeona baadhi yetu wakiwa na wasiwasi naamini tunaenda kufanikisha bajeti hii na ninadhani yawezekana tukavuka hata lengo hili endapo Wizara itaenda kuwekeza vizuri katika mambo yafuatayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, moja Wizara ya Fedha tunaishauri sana nimeona katika bajeti hii bajeti kwa maana ya kiasi gani cha fedha kimetengwa katika research and development bado ni kidogo. Nimejaribu sana kuzisoma nchi za China, nchi za Taiwan, South Korea, nchi za Israel nchi hizi zinaenda kwa kasi kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini siri pekee ambayo wameifanya leo ukiangalia China kila mahali tunanunua vitu vyao kila kitu tunanunua China vitu vingi tunanunua China na uchumi wao unapaa sana lakini China kwa miaka 10 iliyopita kila mwaka katika bajeti yao wanatumia zaidi ya dola bilioni 380 katika research and development. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hatuwezi kufanya maajabu katika kuzalisha ajira nyingi kama uwekezaji wetu katika research and development bado ni kidogo. Taiwan, South Korea kila mwaka wanatumia Zaidi ya asilimia tatu ya GDP yao katika utafiti. Nchi ya Israel kila mwaka inatumia Zaidi ya asilimia nne katika research and development leo nchi ya Israel ni nchi ambayo inazalisha ajira nyingi pamoja na makampuni mengi ni ya pili baada ya Marekani na hiii ni kwa sababu ya uwekezaji mkubwa katika research and development.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tuna vijana wengi wanamaliza vyuo kuna watanzania wengi katika private sector wanahitaji kufanya vizuri lakini ni kwa sababu hatujawekeza sana katika research and development. Tax base yetu bado ndogo naamini tukiwekeza sana katika research and development tukawekeza kwa kiasi kikubwa investment spending yetu ikiwa kubwa katika research and development lazima tax base yetu itaongezeka. Kwa miaka hii na ijayo lazima pato letu litaongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili lazima hizi sekta tatu kilimo, viwanda na biashara ya huduma lazima tufanye uwekezaji mkubwa sana investment spending katika sekta hizi tatu itakuwa ni tiketi pekee ya kuiondoa Tanzania katika umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo kilimo chetu uwekezaji ni mdogo sana uwekezaji katika kutafuta masoko, uwekezaji katika kuwa-train wakulima, uwekezaji katika mitaji bado ni mdogo tunaiomba sana Wizara iangalie kila namna kupata fedha kwa ajili ya kuwekeza zaidi katika eneo hili la kilimo, viwanda pamoja na biashara ya huduma hasa ile ya utalii, na uwekezaji katika sekta hizi tatu utatutoa katika umaskini kwa sababu kubwa tatu sababu ya kwanza sekta hizi tatu zinaweza kuzalisha ajira nyingi sana na kwa sababu hiyo tutakuwa tumeongeza tax base kubwa sana katika nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili, sekta hizi tatu ndizo sekta zinazoweza kutusaidia kuongeza sana mauzo ya nje. Vilevile tukiwekeza vizuri kwenye sekta hizi tatu itatusaidia kuondoa sana inflation katika uchumi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba sana Wizara iwekeze sana katika viwanda, tutoe fedha za kutosha sana na tuweke mazingira mazuri na ya kutosha ku-support ukuaji wa viwanda ili tuongeze ajira kwa vijana wengi ambao sasa wamehitimu na wako willing kuweza kuchangia katika uchumi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie sekta ya miundombinu. Miundombinu inayo-support utalii bado. Inasikitisha sana kuna maeneo tuna potential kubwa ya utalii lakini bado miundombinu ya barabara pamoja na ya viwanja vya ndege ni shida. Leo ukienda upande wa Magharibi wa Serengeti watu wengi wanahitaji kuwekeza lakini bado ujenzi wa barabara unasuasua, tunaendelea kupoteza Pato kubwa la Taifa. Kwa hiyo niiombe sana Wizara twende na priorities watu hawashindwi kwa sababu hawana uwezo bali wakati mwingine tunashindwa kwa sababu ya vipaumbele visivyo sahihi. Tukiongeza uwekezaji katika sekta hizi ni lazima tutaongeza tax base yetu. Hivyo ni lazima mapato yetu yata-shoot tunaweza tukafikia huko mbele hata ku-double hii bajeti ya tirioni 36.

Mheshimiwa Naibu Spika, Rais katika hotuba yake Wizara mbalimbali zimeahidi mambo mengi makubwa; na sisi sote tumeona Waheshimiwa Wabunge waki-report changamoto nyingi zilizoko majimboni. Tunaweza kufikia hili kama tutaongeza tax base tukakusanya mapato makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tukiangalia sekta ya utalii utangazaji bado ni mdogo, investment yetu katika marketing ya tourism bado ni ndogo. Sasa niwaombe sana Wizara itafute namna ya kuongeza uwekezaji katika matangazo katika vivutio vyetu tulivyonavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuweza kufanikiwa sana katika tourism siyo function ya kuwa na rasilimali nyingi, kwa maana ya vivutio vingi ila ni function ya good marketing, na hii itatokana na uwekezaji mkubwa wa fedha katika eneo hili. Niiombe sana Wizara ya Fedha katika bajeti hii itafute kila namna inavyowezekana, kila mahali tunapoweza kupata fedha tuwekeze sana katika kuendeleza VETA pamoja na elimu ya ufundi nchini, hawa ndio wanaweza wakatusaidia katika kuzalisha ajira nyingi tukaongeza tax base na tukaweza kukusanya fedha nyingi.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, nashukuru sana, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)