Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia Wizara hii adhimu. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa wetu Rais kwa kazi nzuri anazoendelea kuzifanya. Nasema anazoendelea kuzifanya maana ni kazi ambazo alikaa kama vile Mungu alivyokaa na utatu wake mtakatifu wakaumba wanadamu na mambo yote duniani na yeye alikaa na utatu wake na Mheshimiwa wetu Hayati wakapanga mipango yote hii iliyokuwepo na miradi yote hii inayoendelea, kwa hiyo ni vitu ambavyo anaendelea navyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa wale ambao wanadhani na wanauliza ngoja tusubiri Mama atafanya nini? Wanapaswa kujua kwamba, hata haya yanayoendelea yeye ndiye aliyekaa pia na kuyapanga na Hayati na anaendelea kuyatekeleza. Sasa tunapaswa kum-support na kumpa nguvu ili kusudi aendelee kufanya mengi mazuri baada ya kuyamaliza haya waliyoanza nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa wetu Waziri mtani wangu Mwigulu Nchemba kwa kukalia kiti hiki cha fedha. Kwa kweli, naamini kabisa fedha yetu iko mikono salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwenye suala la umeme. Kipindi kilichopita tulikuwa tuna vijiji 12,312 ambavyo vilikuwa havina umeme, lakini Mama kwa mapenzi mazuri na Tanzania yetu ameona kwa mwaka huu vijiji 10,317 vyote vipate umeme. Basi kwa maana hiyo ninaamini kabisa kwa kasi hiyo, kipindi kijacho, bajeti ijayo basi hata hivi vijiji vilivyobaki 2,005 naamini kabisa vyote vitapatiwa umeme kiasi kwamba, hata Mkoa wangu wa Mara utapata umeme Mkoa mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kwa wasambaza umeme. Umeme upo, umeme umetolewa, lakini sasa kasi ya usambazaji ni ndogo. Ukiingia ndani kule vijijini unawakuta watu hawajasambaziwa umeme, kwa hiyo umeme unabaki tu kuwa jina kwamba tuna umeme. Kwa hiyo, mimi niwaombe sana Ndugu zangu wasambazaji wa umeme wafuatilie sana susla la kusambaza ili kusudi wasaidie vijiji vyote na maeneo yote yapate umeme ili kuleta pato zuri kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye suala la miradi ya maji. Ninamshukuru sana Mheshimiwa wangu Rais kwa kuweka miradi na kuendelea kujenga au kutekeleza miradi mizuri ya maji ya kimkakati. Kwa kweli, Mungu ambariki sana kwa sababu miradi ya maji yote ikitekelezeka, akimtua ndoo mama kichwani atakuwa ameponya ndoa za wanawake asilimia 98 ambazo zilikuwa zinavunjika kwa ajili ya kufuata maji mbali au umbali mrefu. Wanawake wengine walikuwa wanachoka sana wanashindwa kutekeleza majukumu yao ya ndoa, lakini pia wanawake wengine walikuwa wanaenda kwenye maji mbali sana, wanapokuwa wameenda mbali wanachelewa kurudi nyumbani kwa hiyo, inawaletea conflict ndani ya familia zao, suala ambalo Mama yetu naamini kabisa yeye kama Mama sasa ameona kwamba, alimalize kabisa ili kusudi liende vizuri kwa hiyo, mimi niseme Mungu ambariki sana.. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kwa Watanzania, niwaombe Watanzania wenzagu tumuunge Mama mkono, tum-support Mama, tuwe na umoja na ushirikiano, asitokee mtu mwingine wa nchi nyingine akaibeza Tanzania na wewe ukakubali. Mtu yeyote anayembeza Mama amelibeza Taifa la Tanzania. Mtu anayebeza Taifa la Tanzania amekubeza wewe Mtanzania.

Kwa hiyo, mimi niseme umoja wetu ndio ushindi wetu ili malengo yetu yatimie tufikie malengo yetu, tufikie uchumi wa kati na ikiwezekana tufikie uchumi wa juu zaidi, kama tunavyoona kasi ya Mama ni kubwa sana sio kama watu wengine wa huko nje walivyokuwa wanategemea na wachache waliokuwa wana nia mbaya na Tanzania walivyokuwa wanategemea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mama anaenda kwa kasi ya ajabu, Mama anapiga kazi, Mama yuko vizuri kwa sababu, wao wenyewe ni mashahidi na mashuhuda. Walidhani kwamba, miradi iliyokuwa imeanzishwa kipindi cha Hayati, kipindi kilichopita kwamba, italala, mama amesema miradi yote itatekelezwa. Na ikishatekelezwa atafanya mengine makubwa zaidi ambayo tumeshaona sasa hivi mama anaendelea kufanya mambo makubwa zaidi hata yale ambayo watu hawakutegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaombe sana Watanzania tuwe wamoja, tulilinde Taifa letu kwa nguvu zote. Niwaombe sana watu wetu wa dini zote bila kujali ni dini ya aina gani, watu wa imani zote, kila siku kukicha, asubuhi, mchana na jioni tuliombee Taifa letu la Tanzania ili tufikie malengo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti hii imeongelea vizuri sana kwenye suala la wachimbaji wa madini lakini la wawekezaji kwa ujumla wa Tanzania. Ombi langu, niombe sana kuna watu ambao waliathirika katika mgodi wa North Mara kule kwetu Tarime kipindi kilichopita, kwanza kabisa maeneo yao walipoyatoa walitarajia at least watabadilisha kidogo maisha, lakini waliheshimu sana Serikali yao kwamba wanapotoa yale maeneo na wao watahifadhiwa vizuri, naishukuru sana Serikali yetu kwamba walisikiliza vizuri na baadhi yao walipewa fidia lakini hawajapewa fidia wote, mpaka leo kuna wengine wameingia umaskini kwa kile kinachoitwa uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti hii imeongelea vizuri sana kwenye suala la wachimbaji wa madini, na wawekezaji kwa ujumla Watanzania. Ombi langu niombe sana, kuna watu ambao waliathirika katika mgodi wa North Mara kule kwetu Tarime kipindi kilichopita kwanza kabisa; maeneo yao walipoyatoa walitarajia at least watabadilisha kidogo Maisha. Lakini waliheshimu sana Serikali yao kwamba wanapotoa yale maeneo na wao watahifadhiwa vizuri. Naishukuru sana Serikali yetu kwamba walisikiliza vizuri na baadhi yao walipewa fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hawajapewa fidia wote mpaka leo kuna wengine wameingia umaskini kwa kile kinachoitwa uwekezaji, unapokuwa uwekezaji Tanzania basi mawaziri wetu, waangalie hili suala la wawekezaji, waangalie watanzania wanashida gani, na uhitaji gani ili hawa Watanzania walipwe fidia zao kutokana na mali zao walizozitoa. Siyo watoe wao eneo halafu wabaki kuwa maskini kila siku wanalia siyo jambo zuri hata kwa Mwenyezi Mungu Tanzania tunahitaji baraka. Kwa hiyo, niombe sana kwa wale waliobaki watu wa Tarime Mheshimiwa Waziri ufuatilie hili suala ili wakalipwe maeneo yao na wao waifaidi mali yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nikuombe sana Mheshimiwa Waziri au Waheshimiwa Mawaziri katika wawekezaji wanaokuja Tanzania ninaimani kabisa mnajitahidi sana. Kuna jambo moja naona kama tunafeli hivi inapokuwa kuna uwekezaji mkubwa mahali basi maeneo hayo yang’ae yatakate kutokana na uwekezaji ule siyo tu watu wanawekeza kuna madini sisi tunaonekana kwenye madini. Lakini Mheshimiwa Agnes nikitoka kule Tarime vumbi limeshanipiga mpaka basi. Eti! Mpaka tusubirie bajeti ya Serikali! Kwani wale wawekezaji jamani! Si wangetutengenezea hata lami kidogo hata kuonyesha wamechukua fedha kutoka kwetu, kuchukua pesa kwetu maana yake ni kwamba wanapopata mali kutoka kwetu wanakwenda kuuza wanapata fedha nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, basi wanapopata pesa nyingi na sisi wanaotuacha pale angalau basi tunukie nukie na sisi ile dhahabu siyo tu tuna barabara mbaya maji, hatuna sisi tunaitwa tu tuna wawekezaji jamani hili suala niombe sana mawaziri wetu mkae karibu na hawa wawekezaji muwaambie ukweli kwamba faida wanazofaidika nazo kutokana na nchi yetu ya Tanzania na wao pia watufaidishe.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana kengele ya pili imeshagonga Mheshimiwa.

MHE. AGNES M. MARWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naunga mkono hoja. (Makofi)