Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushkuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia bajeti hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhi Hassan, Kwa kazi nzuri sana anayoifanya. Pili nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu wake pamoja na wataalamu wote wa fedha kwa kazi nzuri wanayoifanya, hongereni sana. Kwa kweli nimeipita hii bajeti yote nzima nimeiona kweli bajeti nzuri sana, ambayo kila mmoja anaisifia na kila mmoja hata kule nje wanaisifia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hapa niweze kuongelea kuhusu mambo ya kilimo. Kila mmoja anaelewa kuwa kilimo inaajiri asilimia 65 ya wananchi, pia kilimo 100% ya chakula kinachotolewa na kinachozalishwa kinaliwa na sisi wananchi kwa 100% wanazalisha hichi chakula. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo licha ya hayo yote imetengewa bajeti kidogo, kwa mwaka huu wa bajeti ya 2021/2022 imetengewa kiasi cha fedha ya bilioni 294.2 ambayo hii ni kidogo sana. Kilimo inamambo mengi, kilimo ina umwagiliaji, kilimo ina mambo ya mbegu, kilimo ina utafiti, kilimo ina kupima udongo, kilimo ina mambo kweli mengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba mambo yote ambayo yametengwa kwenye bajeti hii iweze kutolewa, kusema kuwa ni ndogo kwa upande wa nchi zinazoendelea, kufuatana na Azimio la Malabo ilitupendekeza kuwa, bajeti ya kilimo iwe angalau asilima kumi ya bajeti nzima ya Taifa. Sisi bajeti yetu iko chini ya asilimia moja, unaweza ukaiona kuwa kweli tunakazana na kilimo hatuwezi kuwalaumu Mawaziri ni sisi wenyewe, nilikuwa nashauri kuwa Mheshimiwa Waziri unanisikia kuwa safari ijayo mwaka wa bajeti unakuja 2022/2023, hii bajeti ya kilimo kama kweli tunataka kupunguza umasikini iweze kuongezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuongelea ni kuhusu mikopo ya elimu ya juu, mikopo ya elimu ya juu wote tunafahamu, wote wabunge tunajua, kuwa Watoto wa vyuo vikuu huwa wanatusumbua huko vijijini na mjini, wengi wamedahiliwa na wamepata vyuo na hawakuweza kupata mikopo, kwa hiyo bado wapo vijijini wako huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru naipongeza Serikali kwa kuweza kutenga bilioni 500, ambayo itaweza kwenda kwenye mikopo ya elimu ya juu. Saa nashauri hawa wanafunzi ambao walidahiliwa na wakapata vyuo na wakakosa mikopo, wawe wa kwanza kuwapa kipaombele kuona je, kama watawe kuomba wanaweza wakamit requirement ya kupata hii mikopo.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lengine ambalo naongelea ni ukusanyaji wa mapato, nashukuru kwa kupunguza ushuru wa mashine za kukusanyia mapato. Jambo muhimu ambayo inabidi tuangalie na wote tunajua watu hawadai risiti na watu hawatoi risiti, na ukienda anaweza akakwambia nikupe risiti feki, na wewe kama unataka vitu vya rahsi unakubali pia nilikuwa naomba tutoe elimu kuhusu ukusanyaji wa mapato ndio tunaweza kuendeleza nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naongelea kuhusu lishe, miaka mingi lishe huko nyuma ilikuwa ni kwa Wizara ya Kilimo, na kwenye Wizara ya Kilimo ilikuwa inaenda vizuri sana, kiasi kinamama walikuwa wanafundishwa vizuri hata kupika uji, wanafundishwa lishe vizuri sana, hakuna mtu aliyeongelea kuhusu lishe humu ndani. Jambo ninalo omba bajeti ya lishe iweze kuangaliwa, na ikiwezekana lishe itolewe huko kwenye Wizara ya Afya iweze kwenda kwenye Wizara ya Kilimo kama zamani, au iweze kwenda TAMISEMI ambavyo inaweza ikaratibu vizuri mambo ya lishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa elimu imetolewa asilimia tatu ya bajeti tu ambayo haitoshi, kwa hiyo, nilikuwa nashauri kuwa iweze kutengewa zaidi ya asilimia tatu…

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema Lugangira taafira.

T A A R I F A

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nashukuru, ningependa kummpa taarifa mzuingumzaji kwamba, Chama cha Mapinduzi tayari kimeona umuhimu wa suala la lishe kuwa kwenye sekta ya kilimo, na kwenye ilani yake ile lengo la kushusha hali ya udumavu kutoka asilimia 32 mpaka asilimia 24 imewekwa chini ya sekta ya kilimo. Kwa hiyo, kilichobaki ni Serikali na yenyewe kufanya kama hivyo, ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Ishengoma unaipokea hiyo taarifa.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naipokea kwa mikono miwili, halafu kuongezea hapo hata wale maafisa lishe wanafundiswa na vyuo vya kilimo, kuanzia kwenye cheti mpaka kwenye Chuo Kikuu cha Sokoine wanafundisha hadi lishe. Inakuwaje inaratibiwa na afya?

Naomba sana afya iungane kama idara nyengine lakini mratibu mkubwa aweze kuwa ni kilimo. Pia tuweze kutunga sera na sheria ambayo inaweza kuwabana watu wa halmashauri, kutenga hiyo elfu moja kwa kila mtoto chini ya miaka mitano kusudi iweze kuratibu mambo ya lishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu TARURA, watu wengi wameongelea lakini na mimi nashukuru kwa shilingi milioni mia tano ambazo zinatolewa kila Jimbo kusudi kutengeneza barabara zetu za TARURA. Ukweli barabara ni mbaya zinaweza zikaenda vizuri, halafu napongeza kuwa kwa ushuru ambao utakuwa ni shilingi 100 kwa kila lita ya diesel na kila lita ya petroli ambazo hizi fedha zitakwenda kutengeneza barabara za TARURA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye mafuta. Naishukuru na kuipongeza Serikali kwa kupunguza ushuru na kwa kuongeza ushuru wa mafuta yanayotoka nje ili kusudi kulinda viwanda na kulima mbegu zinazozalisha mafuta ndani ya nchi yetu. Hii hapa nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye juzi kule Singida alizindua kampeni ya kilimo cha alizeti na kilimo cha alizeti ndugu zangu Wabunge mnapotoka hapa nendeni kwenye Majimbo yenu, hamasisheni kilimo cha alizeti ili kusudi tuweze kuondokana na kuagiza mafuta kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu pia kwa kuhamasisha kilimo cha michikichi ambayo na yenyewe inazalisha mafuta ya mawese.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naomba kuongelea ni kuhusu kilimo cha umwagiliaji. Vifaa vya umwagiliaji ukweli ni ghali hasa ukileta kwenye mipira ile ya matone ya maji. Mheshimiwa Waziri, angalia kama kuna VAT kwenye vifaa hivi vya umwagiliaji VAT iweze kutolewa kusudi tuweze kumwagilia kwa urahisi mambo yetu ya mboga mboga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hapa napongeza kwa kutoa ushuru hasa cold chain au chumba cha baridi. Hii itasaidia kwa ukulima wa bustani, wakulima wa bustani kwa sababu wataweza kulima mbogamboga na matunda na wanaweza wakaweka kwenye chumba cha ubaridi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ni nzuri sana kwa sababu inaendeleza kilimo cha bustani ambacho ni rahisi sana kwa kumtoa mkulima kwenye umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaunga hoja na hayo yote niliyoyaongea naomba yachukuliwe. Ahsante sana. (Makofi)