Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kuandaa hotuba nzuri sana yenye kuleta matumaini. Nawashukuruni sana na nawapa pongezi sana kwa kazi nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwa niaba ya Mkoa wangu wa Simiyu na Wilaya yangu ya Maswa napenda niwapongeze Naibu Waziri pamoja na Waziri kwa kutembelea katika Hospitali ya Wilaya ya Maswa. Kulikuwa kuna majengo mapya ya OPD na theater, nawashukuru jengo la OPD limeanza kufanya kazi baada ya kukamilika kwa muda mrefu, lakini lilikuwa halijaanza kufanya kazi. Kwa sasa wananchi wa Maswa wanapata huduma kupitia OPD mpya, nawashukuruni sana kwa hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda tu kuendelea kusema kwamba changamoto imebaki kwenye theater. Theater zimejengwa kubwa na nzuri, lakini hazina vifaa, madaktari ni wachache, tunaomba muendelee kuweka juhudi zenu basi theater ya pale Maswa ambayo ni theater kubwa na ya kisasa ianze kufanya kazi hasa tukizingatia kwamba Hospitali ya Wilaya ya Maswa ni tegemeo katika Mkoa wa Simiyu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu lingine katika Wilaya yangu hiyo ya Maswa ni kwamba hospitali hiyo basi ikiwezekana muipandishe hadhi kwa sababu ni hospitali ambayo ina vifaa vingi vya kutosha lakini haijapandishwa hadhi. Ki-capacity ni kubwa, tunaomba basi muangalie uwezekano wa kutuletea madaktari na vifaa vya kutosha ili iweze kutoa huduma zaidi katika Mkoa wetu wa Simiyu. Wagonjwa wengi wanaondoka katika Wilaya yetu ya Maswa na Mkoa wa Simiyu wanapokuwa referred katika Hospitali ya Rufaa wanakwenda Bugando. Ni mwendo mrefu, ni kilometa zaidi ya 120 wanakwenda kupata huduma kule. Basi naomba muweze kutusaidia hospitali hiyo muipandishe hadhi ili wananchi wangu wa Maswa waweze kupata huduma nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba vilevile nijadili bajeti. Bajeti ya Wizara ya Afya kwa kweli mimi bado inanisikitisha kwani ni ndogo. Kuna upungufu kweli wa shilingi bilioni 18 ukilinganisha na bajeti ya mwaka jana lakini kinachonipa moyo ni kwamba utekelezaji wa bajeti ya mwaka jana ulikuwa ni asilimia isiyofika 40 lakini nina hakika chini ya utawala wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli zimewekwa ceiling mpya, hizo ceiling mpya za kila Wizara nina hakika utekelezaji unaweza kwenda asilimia zaidi ya 80, hapo ndipo ninapopata matumaini makubwa. Tunaomba tushirikiane na Serikali hii tuweze kuhakikisha kwamba pesa zinakusanywa na utekelezaji wa kupeleka pesa katika Wizara ya Afya uwe wa kutosha na mambo yaweze kwenda vizuri kama ilivyopangwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wizara hii ya Afya kuna matatizo ya wazabuni. Kwa mfano, Chuo cha Uganga Wilaya ya Maswa, toka mwaka 2010 wazabuni wame-supply pale vyakula na bidhaa mbalimbali lakini hawajalipwa pesa zao. Kuna deni la shilingi milioni 270 na wazabuni wako 15, wengine wametaifishiwa mali zao na benki kwa sababu hawajalipwa pesa zao na benki zinawadai, kwa kweli wamebaki hohehahe kisa wamefanya biashara na Wizara ya Afya. Mimi nafikiri kufanya biashara na Wizara ya Afya siyo dhambi, ni vizuri mkawajali hawa watu mkawalipa madeni hayo. Pia sehemu zingine zote nchini wazabuni walipwe ili waweze kurudi kwenye kufanya biashara zao. Tunashirikiana na watu binafsi basi tusiwa-discourage kwa kutowalipa madeni hayo. Naomba mfanye juhudi ya kutosha muweze kuwalipa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine katika Wizara hii ni MSD. Nakubaliana kabisa na pande zote mbili ya Upinzani pamoja na Kamati ya Maendeleo ya Jamii, MSD wapelekewe pesa zao on time ili waweze kununua dawa na ku-supply. Kwa sababu tutaendelea kuwalaumu wakati kumbe Serikali na yenyewe inahusika kutokupeleka pesa zao kwa muda unaostahili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba niongelee kuhusu malipo ya madaktari. Madaktari wetu wanafanya kazi nzuri sana, wanapata shida kwa sababu wanafanya kazi, wanakwenda kwenye call zao lakini pesa haziji on time. Madaktari wengine wanadai pesa nyingi hawajalipwa mpaka leo.
Naomba Wizara iangalie uwezekano kwa mwaka huu wa fedha 2016/2017 muwalipe madaktari hawa. Madaktari hawa kwa kweli wanafanya kazi kubwa lakini malipo ni madogo, tushirikiane, tushikamane Mheshimiwa Waziri muwalipe madaktari pesa zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitaka kuwa frustrated nchi hii soma udaktari. Unasoma sana, unafanya kazi sana lakini malipo ni kidogo. Watu waliosoma mambo mengine unawakuta wanafanya vizuri tu na mambo yao ni mazuri, ukisoma udaktari inakuwa kama vile ni dhambi. Na-declare interest na mimi nilipitia huko huko, kwa kweli naomba muilee hii fani kwa sababu ni muhimu, ni fani ambayo huduma yake tunahitaji watu wote, kila mmoja hapa ni mgonjwa mtarajiwa na anakabiliwa na maradhi. Tunaomba mboreshe huduma za afya na muanzie kwa madaktari. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuzungumzia suala kuhusu mafunzo ya wafanyakazi, muongeze idadi za vyuo na kozi mbalimbali ambazo zinaweza ku-produce wafanyakazi wengi wa Wizara ya Afya. Mmepunguza tatizo kutoka asilimia 58 la upungufu wa wafanyakazi wa afya mpaka asilimia 51, bado haitoshi. Tunataka twende kwenye asilimia ndogo ya upungufu wa madaktari na wafanyakazi wa Wizara ya Afya. Tunaomba huduma iweze kuboreshwa na huwezi kuboresha huduma bila kuwa na wafanyakazi wengi wa kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naungana na ushauri wa Kamati kwamba Wizara hii ikiwezekana itenganishwe na TAMISEMI kwa sababu kunakuwa sasa na mlolongo ambao hauendi sawa. Unakuta madaktari walioajiriwa na Serikali Kuu na madaktari walioajiriwa na TAMISEMI wanagongana katika maslahi yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mfano mmoja japo siyo mzuri madaktari waligoma walikuwa wanataka mafao yao yalipwe na walikuwa wanataka walipwe stahili zao za kutosha, waligoma kutoa huduma ili kuisukuma Serikali ilete huduma. Hata hivyo, unapogoma wakati wafanyakazi au madaktari walioajiriwa na TAMISEMI wanaendelea na kazi ile impact ya kugoma inakuwa haipo, Serikali haiwasikilizi, mwisho wa siku Serikali inawagonganisha, inaonekana kama madaktari wanayumba au wanapishana. Wanayumba na kupishana kwa sababu wameajiriwa na waajiri wawili tofauti, huyu kaajiriwa na Serikali Kuu mwingine kaajiriwa na TAMISEMI. Wanapoungana pamoja kudai maslahi yao ya kutosha inashindikana kwa sababu wanakuwa na waajiri wawili tofauti.
Kwa hiyo, naomba hii Wizara ya Afya ishughulikie masuala yote ya afya pamoja na wafanyakazi wote wa afya kuanzia juu hadi ngazi ya chini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda vilevile kuongelea suala la huduma za afya. Mheshimiwa Waziri kwa kweli huduma za afya ni duni nchini kwetu. Ukitaka kujua nchi imeendelea ni pale unapopiga simu ya emergency uone muda wa waganga au gari la paramedical linavyokuja kutoa huduma. Ukienda nchi zilizoendelea ukipiga simu kuna dharura ni dakika tano tu hata haziishi unakuta huduma tayari imeshafika mlangoni. Nchini kwetu ni saa hata 24 unaweza ukapiga huduma haijafika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mfano mmoja wa ajali zinazotokea barabarani. Ikitokea ajali sasa hivi wanaokufa pale pale on the spot ni wachache sana wengi wa wanaokufa ni wale wanaokosa huduma ya afya. Mtu anapata bleeding kwa muda mrefu, anakata roho kwa sababu hakupata huduma ya afya ya haraka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri umefika wakati sasa Wizara iangalie uwezekano wa kuwa na unit inayoshughulikia emergency case. Tunapoteza wananchi wengi kwa sababu ya kukosa huduma ya haraka ya afya yaani huduma ya kwanza. Unapopata ajali labda upasuke kichwa au kifua hapo ndiyo unakufa on the spot lakini wengi wa wanaokufa ni kwa sababu wanakosa huduma ya mwanzo. Tunaomba hili suala Mheshimiwa ulitizame kwa kina ili uweze kulitafutia ufumbuzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuunga mkono hoja, ahsante sana.