Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba mimi ni Mbunge wa Kambi ya Wachache lakini pia pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amekuwa ni mpinzani wangu kwa term mbili mfululizo Jimboni kwangu Iramba Magharibi na nikiri kwamba tulitifuana kwelikweli, lakini ninaomba nikiri kwamba na bila kigugumizi kwamba bajeti hii ni miongoni mwa bajeti ambazo ni bora sana ambazo tumewahi kuwa nazo katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii ni bora kwa sababu inakwenda kutua mzigo wananchi wetu, tumeona tozo nyingi zimefutwa, kodi, ushuru mbalimbali zimefutwa kama ambavyo zimeonekana kwenye ukurasa wa 28 na 31 wa kitabu cha bajeti. Kwa kusema hivyo ni wazi kwamba kama Serikali inaweza kuwapunguzia mzigo mkubwa wananchi wa tozo hizi, inatakiwa kugombezwa au kupongezwa, inatakiwa kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizi yapo mambo ambayo lazima tushauri, nchi yoyote ambayo inaweza ikaonesha ina uwezo wa kujiendesha na kujisimamia kiashiria kikubwa kabisa ni kwenye mapato yake ya ndani, ukiangalia kwa mujibu wa sura ya bajeti yetu utaona kwamba tunatarajia kukusanya trilioni 26.03 mapato ya ndani, ukiangalia matumizi ya kawaida tunatarajia kuwa na trilioni 23 point something, sasa ukichukuwa mapato ya ndani ukatoa matumizi ya kawaida unabaki na trilioni three point something.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tusingekuwa na mikopo na misaada ya kibajeti ni wazi kwamba tulikuwa tunakwenda kutumia trilioni tatu kwa ajili ya miradi ya maendeleo jambo ambalo siyo zuri sana. Mwaka wa Fedha 2021/2022 Serikali inatarajia kukusanya trilioni 36.33 na ukiangalia katika bajeti yetu tunategemea, bajeti yetu inategema takribani asilimia 30 ya mikopo ya kibiashara na misaada kutoka nje na ndani lakini kwa mazingira kama haya na ninaomba hapa Mheshimiwa Waziri anisikilize vizuri kwa mazingira kama haya nina ombi ni vema vyanzo vyote ambavyo zimewekwa kwenye Finance Bill, ambavyo vimetengwa kuwa mahsusi kwa ajili ya kuchangia miradi ya maendeleo, vyanzo hivi viwekewe zuio kuwepo na akaunti ambayo itakuwa ni special kwa ajili ya kutunza vyanzo hivi, kwa mfano tozo ya lane za simu, miamala ya fedha, petrol na tozo nyingine, fedha hizi zipewe akaunti maalum.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili nalisema kwa sababu tusipofanya hivyo tutajikuta tunaingia kwenye mtego mbaya sana wa kukusanya tozo hizi tukapeleka kwenye mfuko wa Serikali halafu zikapangiwa matumizi mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hili Mheshimiwa Waziri you must be very smart kwa sababu mwisho wa siku utakuja kubeba mzigo ambao utashindwa kuutua, kama tunaona kuna kazi kuweka kwenye akaunti special basi tunaweza tukazipeleka Serikali Kuu lakini tukaweka kwenye special reserve fund kwa ajili ya matumizi ya kutelekeza miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwenye akaunti hii ambayo itatengezwa kwa ajili ya kutunza fedha hizi, basi CAG apewe mamlaka kamili ya kuweza kukagua na kupitia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba fedha ambazo zimekusudiwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zinakwenda kuliko kusudiwa, na hii itawapa confidence hata wananchi ambao wanakatwa tozo hizi, kwenye lane za simu na maeneo mengine kwamba watakuwa wanaona moja kwa moja wanachangia fedha na inakwenda kutekeleza miradi ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nina hoja yangu nyingine ambayo ningemuomba Mheshimiwa Waziri wakati wa hitimisho, basi ajaribu kutoa ufafanuzi zaidi kwenye tozo hizi, kumekuwa kuna ukakasi na kupindishapindisha na kutokuwa na uelewa wa tozo ambazo zimesoma kwenye bajeti hii. Ukweli ni kwamba bado tozo hizi hajizaeleweka vizuri na nina wasiwasi mkubwa kwamba kuna uwezekano mkubwa wananchi wakaingia kwenye mtafaruku wa namna mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano kwenye hii tozo ya hawa watu wa bodaboda, ukiangalia kwamba Serikali kwenye bajeti imeeleza kwamba imeshusha kutoka elfu thelathini mpaka shililngi elfu kumi, lakini ukiangalia faini hii hiyo shilingi elfu kumi ambayo imeshushwa ni kosa moja, kuna hatari kubwa ya traffic kupambana na bodaboda kwa sababu bodaboda wanaamini kwamba ni kwa makosa yote kama ambavyo ilikuwa awali kwa shilingi elfu thelathini, kwa hiyo ni vizuri vitu hivi mkavitolea ufafanuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haraka nimalizie na hoja nyingine ambayo inahusiana na namna ya matumizi tumejikita sana kujadili namna ya kutumia fedha, ningependa sasa hivi nijaribu kuelezea kwamba ni namna gani bora tunaweza tukakusanya fedha na tukadhibiti mapato, wote tunajua kwamba Serikali yetu inamiliki shares kwenye makampuni mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo makampuni ambayo Serikali ina total ownership lakini yapo makampuni ambayo Serikali inamiliki kwa asilimia Fulani, lakini kumekuwa kuna tabia ya makampuni haya kuwa yanatoa taarifa ambazo siyo sahihi kwenye mitaji yake, kwenye gawio Serikalini, lakini hata kwenye faida inayoingiza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haikagui, Serikali haina mamlaka ya kukagua makampuni haya kwa sababu ya sheria ambayo inamzuia CAG kukagua makampuni ambayo Serikali inamiliki less than 50 percent. Nina mapendekezo ninaomba Mheshimiwa Waziri Mwigulu Nchemba mnaweza mkapeleka shares zile ambazo Serikali inamiliki less than 50 percent, mkazipeleka kwenye stock market mkizipeleka kwenye stock market automatically share hizi makampuni haya yatafanyiwa ukaguzi na zile fedha zitakuwa wazi kwa sababu kule kwenye stock market wanafanya scrutiny ya hali ya juu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo tutakuwa tuna nafasi ya kujua kile ambacho tumeingiza kina uhalali kiasi gani. Pia nina pendekezo lingine tunaweza tukabadilisha sheria yetu tukampa mamlaka CAG akafanya ukaguzi hata kwenye makampuni yote ambayo Serikali inamiliki less than 50 percent bila kujali shares zetu ziko kiasi gani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo la mwisho ambalo ni muhimu sana ni muhimu tunaweza tukaunda PIC (Public Investimate Company) ambayo kampuni hii itakuwa ni kampuni inayomiliki hisa ambazo Serikali inamiliki minority shares, tukiwa na hii kampuni, itatusaidia kuhakikisha kwamba hesabu zote zinakuwa wazi, zitalazimika kukaguliwa kwa sababu inakuwa ni kampuni tanzu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nakushukuru sana. (Makofi)