Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. OMAR ALI OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na mimi kunipa fursa hii jioni hii kuweza kuchangia bajeti ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninamshukuru Mwenyezi Mungu Subhana wataala aliyetuwezesha jioni hii kutupa pumzi zake na nguvu zake tukaweza kubakia katika Bunge hili Tukufu, siyo kwa uwezo wetu siyo kwa ujanja wetu wala siyo rai isipokuwa ni uwezo wake yeye mwenyewe. Katika mchango wangu kwanza nataka nitoe kauli ya ndugu yetu mtunzi maarufu wa Kiswahili Shaaban Robert aliposema kwamba jibu linaposadifu swali shaka huondoka, hii ina maana ya kwamba nampongeza sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujibu maswali ya Watanzania moja kwa moja kwa matendo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hili kwa kweli hatuna budi tumpongeze sana na wala asichoke na asonge mbele kwani asie macho haambiwi tazama, katika mchango wangu pia nataka niweze kuangalia kwa ruhusa yako unipe nafasi ndogo niweze kutoa nukuu ya falsafa ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa Taifa hili la Tanzania. Marehemu mwalimu alisema siku moja katika nukuu yake ‘‘Njia pekee ambayo uongozi unaweza kutunzwa kama uongozi wa watu ni pale ambapo viongozi wanapokuwa na sababu ya kuogopa hukumu kwa watu’’.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina maana ya kwamba furaha ilitanda katika ukumbi huu wakati Waziri wetu Mama Ummy Waziri wa TAMISEMI alipozitaja Milioni 500 kwenda moja kwa moja kutatua tatizo la barabara zetu za vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli furaha ilitujaa katika nyonyo zetu na bado furaha ile tunaendelea kuwa nayo, lakini tulikuwa tunajiuliza sana sana maswali na ndiyo hapa majibu yalipokuja kwenye falsafa ya Mwalimu Nyerere kwamba Hukumu ya watu tunaiogopa, kwamba tunatakiwa tutende mema kwa watu ili kwamba hukumu hiyo isitujie kwetu sote, kutokana na hali hiyo basi tukawa tunajiuliza hizi milioni 500 kwa vile zinatoka Mfuko wa Hazina, na Mfuko wa Hazina ni wa Tanzania tukaona sasa furaha na sisi imeanza kutuingia, kwa hiyo Mheshimiwa Waziri nikupongeze sana pamoja na Naibu Waziri kwamba hili litaweza kutatua tatizo la Wazanzibar kwa kiwango kikubwa kwenye barabara zetu ambazo na sisi zinakero kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda Tumbatu barabara ni mbaya hazipitiki za vijijini, ukienda Mwera kwa Mheshimiwa Mwinyi nako ni vilevile ukija kwenye Jimbo langu mimi la Wete pia hukumu ni hiyo hiyo, ukienda kwenye Jimbo la Mfenesini nalo linalia, ukienda kwenye Majimbo mengine yote ya Zanzibar yanalia kilio hiki cha barabara ambazo hazipitiki. Kwa hiyo Mheshimiwa Waziri nakushukuru tena naendelea kukushukuru kwamba mfuko huu wa Hazina nao utakwenda kutibu lile donda tulilonalo kule Zanzibar, kwa heshima kubwa kabisa napenda kukushukuru sana pamoja na Naibu Waziri wako na Waziri wa TAMISEMI kwa kulitoa tangazo kwamba Majimbo yote kwa hiyo mimi ninaichukulia yote ni yote Tanzania ni moja itajibu maswali na swali hili litajibiwa na Watanzania wote, hasa ukilinganisha mfuko ni wa Hazina na Hazina ni ya Watanzani wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Nashukuru sana kwa kunipa fursa hii kuweza kuchangia, ahsante sana. (Makofi)