Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba Waheshimiwa Wabunge wanipongeze kwani katika Bunge hili la 2015-2020, mimi ni Mbunge wa kwanza kupeleka ambulance ya kisasa Jimboni kwa kutumia gharama zangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kufika hapa mpaka leo hii maana huko nje magazeti yote Mlinga, Mlinga, kamtu kenyewe hata kwenye mkono hakaenei. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali yangu ya Wilaya Mheshimiwa Waziri ina shida sana. Japokuwa mimi Mbunge nimejitahidi nimepeleka ambulance lakini kuna upungufu mkubwa wa vifaa tiba, hata mashine ya kufulia hakuna, watumishi hakuna, wapo wachache mno. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba katika bajeti yako unikumbuke.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa Idara ya Maendeleo ya Jamii hakuna watumishi wa kutosha, hakuna vitendea kazi, wako maofisa hata pikipiki hawana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba unikumbuke katika bajeti yako hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, limeongelewa suala la NHIF. Waheshimiwa Wabunge ni-declare interest mimi nilikuwa Compliance Officer - NHIF. Nafahamu shida zilizopo katika shirika hili lakini hata hivyo nashukuru viongozi waliopo wamejitahidi. Kuna suala la mashirika ya umma kukataa kwenda kujiunga na NHIF na kusababisha huu mfuko ufe. Kama sisi Wabunge tumejiunga na NHIF, haya mashirika yana nini mpaka washindwe kwenda kujiunga na NHIF? Mheshimiwa Waziri na Waheshimiwa Wabunge niwape siri moja, hii mifuko binafsi ya insurance ina mikono ya wakubwa.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: TCRA hawataki kujiunga na NHIF kwa nini? EWURA hawataki kujiunga na NHIF kwa nini? Kama sisi Wabunge tumeweza kujiunga kwa nini wao wasijiunge? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nikiwa Compliance Officer nilishawahi kwenda TRA kuonana na Mkurugenzi Mkuu ili wafanyakazi wa TRA wajiunge na NHIF. Jibu alilonipa, haki ya Mungu ni kwa sababu ilikuwa ofisini kwake lakini angekuwa ofisini kwangu asingetoka. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na bahati nzuri ameshatumbuliwa jipu, aliniambia sisi pesa sio tatizo maana nilimwambia NHIF mnachangia kidogo mnapata matibabu mengu, wigo wa matibabu ni mpana. Halafu pia sheria inataka mashirika ya umma yajiunge na NHIF. Akaniambia sisi hela kwetu sio shida, nikamuangalia kimoyomoyo nikasema hizi fedha za kwako?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba Mheshimiwa Waziri afuatilie hilo, mashirika mengi ya umma hawataki kujiunga na NHIF kwa sababu wanapewa ten percent wanapokwenda kujiunga na mashirika binafsi ya insurance. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kinanisikitisha sana nacho ni ubakaji wa wazee, sijui Wizara hii mnaliangaliaje suala hili. Kuna mikoa ubakaji wa wazee umeshamiri. Huwa najiuliza shida ni nini au wanawake wa maeneo ya huko wagumu kuelewa somo mpaka hawa watu wanaenda kubaka wazee? Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri naomba mfanye utafiti mgundue ni nini kinachosababisha tatizo hili. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utulivu Waheshimiwa Wabunge, nimepata tuhuma nyingi sana jamani. Nimeitwa teja, jamani Waheshimiwa Wabunge hebu mnitazame, teja anaweza akawa anashinda amevaa suti zimenyooka namna hii? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwamba ukiniita mbilikimo nitachukia kwa sababu ukweli mimi ni mbilikimo na kila nitakapokuona nitakuchukia lakini ukiniita teja siwezi kuchukia kwa sababu sio ukweli na ukweli huwa unauma, kwa hiyo siwezi kuchukia. Nimepata vitisho vingi, lakini naamini Serikali yangu ipo. Kama wanajeshi walienda kuwakomboa wananchi wa Kongo wakaisambaratisha M23 watashindwa kunilinda mimi tena Mbunge? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Waheshimiwa Wabunge wamefurahi lakini naomba mnisaidie kumwambia Waziri wa Ujenzi, naomba Daraja la Kilombero liishe mwaka huu. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo sina mengi, naomba kumalizia kwa kusema naomba uje ukitembelee Kituo changu cha Afya cha Lupilo. Sitaki kuongelea hapa lakini naomba uje ukitembelee kituo changu cha afya uone jinsi kilivyo, hakifananii kufanya matibabu ya binadamu, sisemi lakini naomba tuondoke wote uende ukajionee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo sina mengi, ndio hayo tu.