Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushuru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kutoa mchango wangu, nimebahatika kuwa Mbunge hii ni term yangu ya pili kwa maana ni mara yangu kuwa Mbunge katika Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishiriki kupitisha bajeti zote za Serikali kwa Bunge lililopita ninaomba niwe honest kwa mara yangu ya kwanza toka nimekuwa Mbunge nimeshuhudia bajeti iliyobeba dhima halisi ya wale waliotutuma kwa maana walipa kodi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara ya kwanza, kama Mbunge nimeshuhudia kiwango kikubwa sana cha kasi ya upelekaji wa fedha za miradi ya maendeleo katika halmashauri zetu. Ninaomba niseme kwa dhati ya moyo wangu na Kiongozi Mkuu wa shughuli za Serikali kipenzi chetu Waziri Mkuu Kassim Majaliwa yumo humu ndani. Mheshimiwa Waziri wa Fedha wewe na Naibu wako Mheshimiwa Eng. Masauni mmewatendea haki sana walipa kodi na wananchi waliotutuma katika Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu yetu Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa alikuwa Singida ndani ya siku moja mbili zilizopita, na nitaka nilisema hili Mheshimiwa Waziri Mkuu nanijuwa na huko hapa na ninajua Mheshimiwa Gulamali atatulia niseme wema wa Waziri Mkuu aliyeuonyesha kwa watu wa Singida akiwa ameambatana na Waziri wa Kilimo na Naibu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu wananchi wa Singida wanakupongeza kwa jambo kubwa moja, ulipokwenda Singida kwa agenda ya zao la Alizeti ambalo ni zao la Serikali la kimkakati, ulitumia zaidi ya masaa nane ukiwa umekaa kwenye meza ukisikiliza hoja za wananchi wetu na walipa kodi wetu mmoja baada ya mwingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu usikivu wako wananchi wametutumia meseji na ushahidi tunao wanasema hawajapata kuona kiongozi wa kiserikali, wa nafasi kubwa kama Waziri Mkuu anaweza kukaa na akatulia kwa masaa zaidi ya nane akisikiliza michango ya wananchi tena wananchi wengine ambao hawana hata uelewa mpana wa mambo ya kimkakati ya kiuchumi, lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu uliwasikiliza wananchi wa Singida wakatoa mawazo yao wakatoa wanataka direction gani katika production ya sunflower katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niungane na wananchi wa Mkoa wa Singida kusema kabisa kwa dhati ya moyo wangu kama kuna karama za kiuongozi Mungu anazitoa, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, Waziri wetu Mkuu umepewa karama kubwa sana ya kiuongozi karama ya kuwa na unyenyekevu wa hali ya juu ya kujishusha to the ground na kuwasikiliza walipa kodi. Umetupa somo kubwa sana sisi vijana tunaokuwa katika uongozi ahsante sana kiongozi wetu Mungu akubariki sana kaka yangu. (Makofi/ Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la Alizeti ni zao ambalo Serikali ya Awamu ya Sita na niwapongeze sana Mawaziri wa Wizara hizi mbili ni zao ambalo wameamua kwa dhati kulifanya kuwa zao la kimkakati na ninataka nitoe takwimu zifuatazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tuna make seventy eight percent ya market share ya uzalishaji wa mafuta ya Alizeti katika ukanda wa East Africa na baadhi ya nchi za maziwa makuu ikiwemo Zambia, pamoja na Kongo. Asilimia 78 ya market monopoly Tanzania tumeikamata, nchi inayotufuata kwa mbali sana ni Uganda kidogo, wakifuatiwa na Rwanda ambazo production yao ni karibia tani kama 4,000 kwa mwaka mzima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kukisema na ninaomba kabisa Waziri Wizara ya Fedha na Naibu mnisikilize, hili mkiweza kulichukuwa wazo langu nina imani kabisa mtakwenda kuifanya Tanzania inakwenda kuwa another giant katika kuliteka soko la Afrika kwa sababu anayeongoza ni South Africa ambaye amekamata 48, 46 percent ya production ya mafuta haya katika ukanda mzima wa Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri naomba unisikilize ushauri wangu tumeweka incentive kwa wale tunawaita strategic investors katika sekta ya sunflower production. Kwa Mkoa wa Singida strategic investor tunaye huyu mmoja katika kile kiwanda kikubwa cha uzalishaji, viwanda vingine huyu yeye amepewa zero VAT kwa maana ni muwekezaji mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nilipe Bunge lako taarifa katika zao hili la Alizeti takwimu zimeshasomwa na hapa Bungeni namna gani Serikali na Taifa tunatumia a lot of forexes kuagiza mafuta kuja ndani ya nchi. Na wakati mwingine mafuta haya uenda yanakuwa hata hayana ubora ule tunaoukusudia. Tanzania tukiamua kwa mipango thabiti na tumepata Waziri wa Fedha naomba nikiri msikivu sana anayefikika kwa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu na kiongozi wetu Mkuu wa Serikali yupo hapa Bungeni, ushauri wangu ninaomba Wizara ya Kilimo Wizara ya Biashara na Masoko sijui na vitu gani ninaomba kwa dhati ya moyo wangu chukueni ushauri huu. Nendeni mkaangalie wale wazalishaji wadogo wa mafuta katika Mkoa wa Singida na mikoa jirani, wazalishaji wale mkienda kuwaangalia wawezesheni wapate mashine za kisasa katika kuhakikisha ya kwamba ukamuaji wa mafuta unakidhi tija kwa sababu mashine nyingi wanazotumia hazina ubora wa kimataifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkiweza kulifanya hili Mheshimiwa Waziri pamoja na Wizara ya Viwanda na hii chachu mliyokuja nayo ya kuleta mbegu za kisasa katika zao la Alizeti nataka niwaambie kwa idadi ya wakulima tulionao wa Alizeti kwa Mkoa wa Singida peke yake Mkuu wa Mkoa amekuja na takwimu kwenye kikao cha Mkuu wa Mkoa Singida peke yake kwa wakulima wetu tunauwezo wa ku- cover production ya nchi nzima ya Alizeti na tukabusti uchumi wa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mheshimiwa Bashe ushauri wangu ninawaomba kwa kuwatumia wakulima hawa ambao umeamua kuwekeza kwao, nataka niwaambie Singida tunayo ardhi ya kutosha yenye rutuba, tuna watu akina baba wenye uwezo wa kufanya kazi tuko tayari tukiwezeshwa na Serikali kuhakikisha tunazalisha tuweze kupiga hatua katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ninalotaka kuliongelea juzi nimetembelea Kisarawe nimetembelea Wilaya ya Mkuranga anapotoka kaka yangu na Waziri mahiri kabisa kijana Mheshimiwa Ulega usipokuwa makini unaweza ukafikiri hili Taifa watu wanafanya ngonjera hili Taifa linapiga hatua this country is moving nchi hii inapiga hatua kubwa ya kimaendeleo ya kiuchumi, tumekwenda pale kwenye kiwanda tukiwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye Kamati ya Sheria na Katiba tumejionea uzalishaji wa gypsum kwenye kiwanda kile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazungumza kiwanda kile ambacho kipo kwenye nchi yetu ya Tanzania kime- capture market ya nchi saba Afrika Kenya, Zambia Malawa Msumbiji mpaka Zimbambwe wanauza gypsum. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu Mheshimiwa Waziri kiwanda kile cha kimkakati kina changamoto moja kubwa na nilizungumza hapa Bunge lililopita kuhusiana na mifugo watu wengine wakaniona na attack personality za watu leo Serikali mmefanya research ushauri niliutoa yale matozo yote ya kwenye nyama mmeyafuta wananchi kule wanapiga makofi production ya nchi itaongezeka ninawapongeza sana Mheshimiwa Waziri na Wizara ya Mifugo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsanteni sana Mheshimiwa Waziri Mkuu wamefanya kazi matozo niliyoyasema hapa Bungeni wamefanya utafiti wamejiridhisha leo nimesoma ripoti ya Waziri wamefuta zile tozo ninawapongeza sana Wizara ya Fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokiomba nendeni mkakitembelee kile kiwanda Wizara ya Fedha mimi kila jambo nikilizungumza hapa ninazungumza kwa maslahi ya Taifa langu siweki maslahi yangu ninazungumza maslahi ya nchi mtu achukie apende asipende nimeiweka Tanzania yangu mbele kwa maslahi ya vizazi vinavyokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu nendeni mkakitembelee kiwanda kile cha Mkuranga wale watu wana changamoto moja Mheshimiwa Waziri karatasi wanazozitumia katika ku-cover ile gypsum haipatikana Tanzania karatasi ile inakuwa imported kutoka nje ya nchi na inapekelekea cost of production inakuwa kubwa inasababisha bidhaa inakuwa na bei kubwa na ninataka nikuambie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda kile wakati wana ki-acquire kilikuwa na uwezo wa kuzalisha milioni 4 waka- expand uzalishaji mpaka milioni 15 na actual production ni milioni nane wameweza kuliteka soko lote la Afrika na Mheshimiwa Waziri Mkuu nilifanya upelelezi kutaka kujua resources tulizonazo zinazoweza kukifanya kiwanda hichi ku- sustain tumeambiwa ma-gypsum powder tuliyonayo yanaweza yakazalisha gypsum kwa zaidi ya miaka 40 na yapo yakutosha kwenye Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuomba Waziri wa Fedha wewe na naibu wako fanyeni utafiti wa kitaalam tumieni vyombo vyetu vya kiserikali nendeni mkawasaidie mwekezaji huyu ajira aliyoitoa nilipoona sikuamini kama niko Tanzania, sikuamini kama niko kwenye nchi hii ya Tanzania, msaidieni mwekezaji huyu aweze kupata nafuu ya kodi kwenye hii kodi moja ya makaratasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnaona hilo haliwezekani pelekeni fedha kwenye kiwanda chetu cha kuzalisha karatasi nunueni mitambo izalishe karatasi wapate market ya kuuza kwa mwekezaji huyu mtakuwa mmesaidia na mtakuwa mmeliongezea nguvu Taifa katika kuzalisha kodi wanayolipa wale watu na production wanayofanya nimekwenda kulala usingizi hata…

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa!

T A A R I F A

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge anavyozungumzia suala la kiwanda kinachozalisha karatasi nchini ni Mgololo kiwanda kile kile nimefika pale na nimeona uzalishaji wa kiwanda na kina changamoto ya masoko ya ndani ahsante.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kingu malizia washa mic umalizie muda wako.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaipokea kwanza taarifa lakini aina ya karatasi ninazozizungumzia za gypsum sio karatasi kama hizi ni karatasi ni industrial paper zinazotumika kwenye gypsum. Ambazo mwekezaji huyo anatumia fedha nyingi kuzi-import Mheshimiwa Waziri Mkuu kaka yangu kama tunaweza tuone fedha kwenye kiwanda kile kilete mitambo ya kisasa kizalishe karatasi kwa sababu soko tayari lipo unless otherwise mpeni msamaha wa kodi mwekezaji huyu anayeleta ajira kwenye Taifa letu na kusababisha TRA kukusanya kodi ya kutosha katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. (Makofi)