Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia bajeti hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kitabu chetu cha Quran mwanamke ametajwa mara tatu, mwanaume ametajwa mara moja, kwa nini sasa? Wengi tunamzungumza Mama Samia, tunampongeza kwa kazi nzuri alivyoanza, lakini mimi ninasema Mama Samia tumuombee dua usiku na mchana, huyu ni mama, huyu ni mwanamke. Nilisema Kitabu cha Quran mwanamke ametajwa mara tatu kwa sababu mama ndiye aliyebeba mimba, mama ni mlezi, mama ana upendo. Kwa hiyo, naomba Watanzania, Waheshimiwa Wabunge, tumuombee Mama Samia afanye kazi kwa kuwatendea haki Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumuombea dua Waziri na Naibu Waziri kwa kazi nzuri waliyoanza kufanya, Mwenyezi Mungu awape nguvu na afya kwa kuitekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mbunge niliyetokea Zanzibar. Bajeti imezungumza vizuri sana, lakini bado nitasema kuna mambo yanayotutanza Wabunge tunaotoka Zanzibar. Mimi leo nilileta gari langu karibuni na barua hii hapa. Barua hii nimepewa nije na gari langu kuishi nalo Tanzania Bara kwa mwaka mmoja, wakati mimi ni Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mkataba wangu nikiwa hai ni miaka mitano, leo nimepewa barua hii nikae na gari langu huku mwaka mmoja.

Je, tunamuuliza Mheshimiwa Waziri hii ni sheria au ni haki au ni nini? ama ni sisi tu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili niulizie kuhusu ma-agent kutoa gari Zanzibar kuja Tanzania Bara. Tuelezwe huyu agent ana mchango kwenye Serikali au ni nini? Tuelezwe kwa kweli imekuwa ni mateso ni maonevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi kwa wafanyabiashara wadogo-wadogo. Tunapenda sana wafanyabisahara wadogo-wadogo, vijana, akina mama na wazee, lakini vijana na wazee sasa hivi biashara zao wanafanyia katikati ya barabara, kwa kweli hii ni hatari maana hata Serikali inakuwa mapato inapoteza. Unakuta leo sado za nyanya zimepangwa barabarani, pana ujororo tu wa barabara tunaopita na magari, kwa hivyo naomba suala hili lishughulikiwe. Kwa kweli, wapangiwe nafasi, sehemu nzuri ya kufanya biashara zao wao wapate, lakini na Serikali ikusanye mapato vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira. Ilipopita bajeti Wabunge wengi tulizungumza kuhusu maliasili, kama hatukulisimamia suala la maliasili basi maliasili nafikiri baada ya muda mdogo itakuwa wanyama wetu wengi watapotea. Leo Mheshimiwa Mbunge anasimama anasema yeye tembo hana faida nae, ng’ombe ndiyo wana faida nao. Mimi naiomba Serikali lazima Wabunge wale waliopo pembeni mwa hifadhi wapewe elimu pia na wafugaji wapewe elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisema tembo hana faida kwa sababu tembo ni mnyama aliyeumbwa hifadhi yake ni kukaa kwenye hifadhi, hatembei, hata ukimfuata tembo unamfuata nyumbani kwake. Kwa hivyo, mtu yeyote anayemfuata mtu nyumbani kwake unakwenda kumtafuta ushari. Mimi nilikuwa naomba suala hili la hifadhi zetu lazima zilindwe, ziheshimiwe na sheria zifuatwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye utalii. Tunasema sana utalii ni wa nje tulikuwa tunautangaza, lakini sasa tutangaze utalii wa ndani. Nani atatangaza utalii wa ndani? Kutangaza utalii wa ndani ni wananchi wenyewe wa ndani. Tuna wasanii wazuri, vijana, warembo, hawa tuwape ubalozi watangaze utalii wetu wasitafute watu wengine wa nje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii. (Makofi)