Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekitti, ahsante kwa kunipa fursa hii niweze kuchangia Bajeti ya Serikali. Nimeisoma vizuri bajeti hii, jambo moja ambalo naweza kuwaambia Watanzania pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwamba Tanzania tuna bahati kubwa sana. Tumepata Rais msikivu amesikia vilio vya Wabunge, amekaa na Mawaziri wake, vitu vyao vingi wametuwekea kwenye bajeti yetu, tunawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze pia Mawaziri, nimpongeze Mheshimiwa Mwigulu Nchemba kaka yangu Waziri wa Fedha pamoja na Naibu wake kaka yangu Masauni, kwa kweli wamekuwa ni wasikivu na wanyenyekevu. Wamechukua mambo yetu humu Bungeni wameenda kukaa na Amiri Jeshi Mkuu, Rais mwanamke mwenye kuandika historia ya kwanza Tanzania kwamba ni Rais mwanamke na kuleta bajeti nzuri ambayo mimi mwenyewe ikiwa ni bajeti yangu ya 11 toka nikiwa Mbunge nimeiona ni bajeti ya kipekee, nawapongeza sana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti hii imepanua wigo wa kodi, lakini imetuletea kodi za kisayansi, kodi ambazo hazimuumizi moja kwa moja mwananchi, kodi ambazo mwananchi anazilipa bila kuzisikia. Yote hii ni dhamira ya Rais wetu mwanamke ya kuleta mageuzi ya maendeleo ndani ya nchi yetu ya Tanzania. Tunampongeza sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna nchi isiyolipa kodi, dunia nzima tunalipa kodi ila inategemea ni kodi za aina gani ambazo wananchi wako watazimudu. Nitoe mfano kama kodi iliyoandikwa kwenye bajeti yetu ya property tax, nimesikia kuna watu wanaiongelea kodi hii, wakisema kwamba kodi hii italeta mkanganyiko baina ya mwenye nyumba na mpangaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ina watalaam, nyumba zetu zina hati za nyumba, kwa mfano nyumba imeandikwa Munde ndiyo mwenye nyumba, kwa hiyo watalaam hawa wataenda kufanya katika zile LUKU kama kuna LUKU tatu au nne, wataangalia nyumba hii hati ya nyumba ni ya nani, kama ni ya Munde house rent ya huyo property tax rent itafidiwa kwenye LUKU ya mwenye nyumba. Kwa hiyo niwatoe wasiwasi Watanzania pamoja na Waheshimiwa Wabunge waliokuwa wanadhania kwamba huu ni mkanganyiko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kama ikitokea kwa bahati mbaya mpangaji amekatwa property tax rent risiti itaandikwa kuna property tax rent ya Sh.3000 au Sh.2000, siku wana-renew mkataba wao wataiweka mezani kwamba nilichangia LUKU Sh.20,000, kwa hiyo wakati una-renew mkataba nitakatwa hiyo 20,000 kwenye mkataba wangu. Kwa hiyo niwaombe Watanzania na Waheshimiwa Wabunge tuzipokee kodi za kisayansi za Amiri Jeshi Mkuu mama yetu Samia Suluhu, hazitamuumiza mwananchi, unakatwa elfu moja moja, hutaisikia kama kuna kodi, lakini Serikali itakusanya mapato mengi na hatimaye kutekeleza yale mambo yote tuliyokuwa tunayataka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji trilioni 36 ili kutekeleza mambo yetu. Ni lazima tulipe kodi Watanzania, hatuwezi kuwa na nchi ambayo hailipi kodi, lakini kodi hizi ni nzuri na za kisayansi. Tuache propaganda ya kuzalisha maneno kwamba ukiamka asubuhi simu yako inakatwa Sh.200, simu yako inakatwa shilingi 50 siyo kweli, ukiweka voucher, ukiweka muda wa maongezo wapo watakaokatwa shilingi 10 ambayo kwa mwezi ni shilingi 300 kwa kuweka muda wa wapo watakaokatwa shilingi 20 ambayo kwa mwezi ni Sh.600 kwa kuweka muda wa maongezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale watumiaji wakubwa wa juu wanaotumia shilingi 100,000 mpaka shilingi 200,000 labda Wakuu wa Taasisi ndiyo watakatwa shilingi 200 kwa siku watakayoweka muda wa maongezi. Akiweka muda shilingi 800 tu. Kwa hiyo jamani kodi hii haina tatizo twendeni tukalipe kodi, tukahamasishe Watanzania, Mheshimiwa Rais apate pesa aweze kuleta maendeleo kwenye nchi yetu, twendeni tukamuunge mkono Amiri Jeshi Mkuu wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais amejipambanua kwamba yeye ni Rais mpenda haki na mimi nawathibitishia Watanzania na Wabunge, Mheshimiwa Rais ni mpenda haki, mimi najua Mheshimiwa Rais ni mpenda haki. Pia amekuwa na slogan zake, anapenda kusema kwamba kazi iendelee na zege hailali, twendeni tukakusanye kodi, Mheshimiwa Rais afanye kazi iendelee na zege hailali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepata Amiri Jeshi msikivu, mchapakazi, mwanamama wa kwanza Tanzania, naamini ndani ya miaka yake kumi ya uongozi wake wa urais mpaka 2030 atakuwa kafanya kazi kubwa na ataacha legacy kubwa ya maendeleo kwa jinsi hapa alivyotuonyesha ukusanyaji wake wa kodi, najua pesa zitapatikana na malengo yake yatakwenda kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema bajeti hii ni ya wananchi na bajeti hii imegusa watu, Mheshimiwa Rais ameenda kugusa watu wa chini kabisa kama bodaboda, walikuwa wanalalamika muda wote bodaboda, wanalalamika wapunguziwe faini muda wote, lakini Mheshimiwa Rais Samia ameenda kuwapunguzia kodi bodaboda wetu, faini kutoka shilingi 30,000 mpaka shilingi 10,000 kwa kweli vijana hawa walikuwa wanaumia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais amesikia kilio cha muda mrefu cha Madiwani wetu kulipwa na central government posho zao. Leo tunaenda kuwalipa Madiwani wetu kutokea central government. Malipo kwa Serikali za Mitaa, mimi Madiwani wangu wamekaa miezi sita hawajalipwa posho zao, naamini sasa watakuwa wanapata kwa wakati muafaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka tupate uhuru, hakuna awamu iliyowahi kulipa posho ya madaraka ya Mtendaji wa Kata na Katibu Tarafa, ni awamu hii ya Rais mwanamke Mheshimiwa Mama Samia Suluhu. Nani kama mama?

MBUGE FULANI: Hakuna!

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa watu ndio wanaosimamia maendeleo yetu, wanasimamia utekelezaji wa ilani kule chini, Mheshimiwa Rais amewaona na ninaamini kazi itakuwa nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Mheshimiwa Rais ameenda kumaliza kero ya ukamilishaji wa maboma ambayo ilikuwa inakera kwenye majimbo yetu. Tuliwahamasisha wananchi wakajenga maboma, lakini yalikuwa yamebakia wazi na wakaona kama nguvu zao zimekwenda bure. Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu amekwenda kumaliza kero ya maboma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais amekwenda kuandika historia kwa kujenga shule za watoto wa kike za mabweni kila mkoa, tena za sayansi ili kupata wanasayansi wazuri wanawake. Vile vile Mheshimiwa Rais ametuwekea pesa za TARURA. Ameongeza Mfuko wa TARURA kwa shilingi mia mia kwenye lita ya mafuta ili tutokane na kero kubwa ya barabara kwenye vijiji vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisikia kuna Mbunge mmoja analalamika kwamba tukipandishwa shilingi 100 vitu vitapanda bei. Hivi kero ya barabara inayoua magari yetu, inayoshindwa kusafirisha na shilingi 100, kipi bora? Tuache kuwa walalamishi. Naipongeza sana Wizara ya Fedha, nampongeza sana Waziri aliyepo madarakani na Naibu Waziri wake kwa kazi nzuri, lakini Mheshimiwa Mama Samia Suluhu amefanya mambo mengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nirudi kwa Mheshimiwa Waziri wa Fedha, namwomba sana, watakapokuwa wanakusanya hizi fedha, hizi fedha ni kwa ajili ya maendeleo. Tunaomba azi-ringfence ziwe kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania, zisiwe kwa ajili ya kulipana posho. Kazi maalum shilingi milioni 400 kwenye pesa hizi za kodi ya Watanzania.

Namuomba sana Mheshimiwa Waziri na Wizara yake ya Fedha, pesa hizi wazipeleke zikafanye kazi ya kuwakomboa Watanzania kama Mheshimiwa Rais Samia alivyodhamiria na siyo kwa ajili ya kulipana posho kwa kazi maalum. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli tunamwomba sana Mheshimiwa Waziri sana na Naibu Waziri wasimamie hilo kwa watendaji wao. Pamoja na Katibu Mkuu kama yupo humu, hizi sio pesa za posho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza tena na tena Mheshimiwa Rais wetu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu, kwa kweli...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Munde bado dakika zako.

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa suala zima la TARURA. TARURA kulikuwa na kero kubwa. Waheshimiwa Wabunge humu walikuwa wanalalamika wakiisema TARURA, lakini ilikuwa haina fedha za kuweza kufanya kazi kukidhi mahitaji yaliyopo kwenye majimbo yetu.

Hata hivyo, kwa maono makubwa ya Mheshimiwa Rais pamoja na Wizara yake ya fedha nikimaanisha Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu wa Wizara hii, wameliona hili, wameamua kuongeza pesa kwa ajili ya kuongezea mfuko huu. Wameanza kwa kupeleka shilingi milioni 500 kila jimbo hili kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niwahakikishie Watanzania, tumepata Rais mzoefu, mchapakazi, tunakwenda kufanya kazi kwa bidii, tunakwenda kuandika historia, mpaka ikifika mwaka 2030 ambapo Mheshimiwa Mama Samia anakabidhi kijiti, ninaamini atakuwa ameacha legacy kubwa sana ndani ya nchi ya Tanzania. Ahsante sana. (Makofi)