Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa nafasi ya kuchangia, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa zawadi hii ya uhai, kipekee kabisa niwashukuru sana Mawaziri wetu wa Wizara hii ya Mipango na Fedha kwa uwasilishaji mzuri wa bajeti yetu, lakini pia kwa kujibu kwa umakini na uweledi mkubwa Hoja za Wabunge, Mwenyezi Mungu aendelee kuwasimamia katika majukumu yenu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na vilevile nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati Mzee wangu Sillo kwa kazi nzuri aliyofanya ya kuitengeneza bajeti hii mpaka hapo ilipofikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kipekee kabisa na kwa dhati ya nafsi yangu nimpongeze Mwanamama jasiri, Mwanamama hodari Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa usikivu mkubwa alionao kuhakikisha kwamba anakwenda kuondoa shida na taabu kwa Watanzania. Kama jina lake linavyoitwa Samia kwamba ni msikivu, Mama yetu ameitendea haki Watanzania kwa kusikiliza vizuri kabisa hoja za Wabunge na kuzifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niliwahi kuchangia suala zima la kupunguza urasimu katika kodi za viwanja na mapango hili linakwenda kutekelezwa kwa kuhakikisha kwamba kodi za mapango yatalipwa kwa kupitia LUKU, niipongeze sana Wizara kwa usikivu huo nami nimeipokea kwa mikono miwili sana. Tahadhali moja ambayo naomba kuitoa wizara tafadhalini tujaribu kuangalia kwa wale ndugu zetu wanaofanya kazi ya biashara ya real estate isije kulipiwa kodi katika yale majengo ambayo kuna LUKU zaidi ya moja ndani lakini akaenda kulipa kodi moja kwa moja tutakuwa tumewabana wafanyabiashara wale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niipongeze sana kwa suala zima la kuhakikisha tunakwenda kuziboresha barabara za TARURA, hili ni jambo kubwa sana kwa uchumi wa Tanzania na kuhakikisha kwamba sekta ya ujenzi inakwenda kuongeza na kuchangia kwa kiwango kikubwa kwenye Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hoja hii ya kuongeza fedha katika mafuta ili tuweze kujenga barabara za TARURA, mimi naomba nichukue nafasi hii pia kuwatoa Watanzania wasiwasi. Watanzania wanafahamu kwamba unapoongeza fedha katika mafuta basi tunakwenda kuongeza mfumuko wa bei, kwa mujibu wa data za National Bureau of Statistics. Lakini Watanzania nawaomba tuwahakikishie kwamba, mama yetu mweledi mwenye upeo wa mbali ameangalia vizuri sana, kwa sababu factor muhimu katika kuhakikisha mfumuko wa bei ni suala zima la gharama za usafirishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapotoa nyanya zetu kutoka Iringa zinapokuja Dar es Salaam, msimu wa mvua barabara hazipitiki, hakika mfumuko wa bei utakuwa juu. Lakini tunapokwenda kuiangalia GDP ya taifa letu tunakwenda kuangalia uzalishwaji wote wa makampuni na watu binafsi. Kwa kilichofanyika hapa, in a long run tutaongeza per capital income ya Mtanzania na nchi yetu inakwenda kukua katika uchumi wa mbele wa taifa hili. Hongera sana mama yetu Samia Suluhu Hassan, hongera sana Mawaziri mliofanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya Watanzania wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine naomba nichangie kuhusu suala la uchukuzi. Sisi Watanzania tuko kwenye umoja wa East Africa na tuko kwenye umoja wa SADC lakini hatuko kwenye umoja wa COMESA. Sasa, kwa kuangalia Overload Control Act ya East Africa na Overload Control Act ya SADC tunapata confusion kidogo hapa. Wafanyabiashara wetu wanapolipa transit charge kwa kila kilomita 100 ndani ya Tanzania analipa dola 16,000. Lakini huyu huyu Mtanzania anapokwenda Kenya kwa mujibu wa East Africa anatakiwa alipe dola 10, lakini wanaotoka SADC na wanaotoka Uganda ndani ya ukanda ule wa East Africa wanalipa dola 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Serikali iende ikaliangalie hili ili kuhakikisha wafanyabiashara wetu nao wanakwenda kufanya biashara katika harmonizing way ili wanaokuja Tanzania nao waweze kufanya biashara kwa kutumia transit charge ya dola 10 badala ya 16. Kwa sababu wenzetu ambao wapo kwenye COMESA wana-take advantage ile ya kutukandamiza sisi. Wale wa SADC wanapokwenda Kenya wanalipa 10 lakini wanapokuja Tanzania wanalipa 16. It is obvious wata-run away from Tanzania na wataenda kukimbilia Kenya na Uganda. Kwa hiyo naomba hili uliangalie.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine naomba sana kuishauri Serikali. Tumepata mwarobaini wa barabara za vijijini kwa kutumia TARURA; lakini naomba niishauri Serikali kwa unyenyekevu mkubwa. Ni kwamba, barabara zetu kuu (trunk roads) na barabara zetu za regional roads pamoja na district roads thamani yake ni trilioni 21 za Tanzania. Thamani hii tusipoilea ipasavyo tutakuja kurudi nyuma na tutaanza kuzijenga barabara hizi upya. Naomba tuangalie namna nzuri ya kuhakikisha kwamba barabara hizi, trunk roads, regional roads na district roads zinafanyiwa periodic maintenance ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kwasababu gani, ukiangalia corridor ya TANZAM ambayo ni muhimu sana kwa sababu ndiyo inatuvutia wateja kutoka Malawi, Zambia pamoja na Lubumbashi – DRC. Corridor hii ni chakavu na imechoka sana, tunataka kuwaambia nini wafanyabiashara wanaopita katika njia hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, tuchukulieni mfano tu, kile kipande cha Chalinze – Mlandizi it is almost collapsed, lakini tukiangalia kutoka Dodoma mpaka Iyozi it is almost collapsed, ukiangalia Tunduma mpaka Igawa it is almost collapse. Sasa hii TANZAM corridor, ambayo ndiyo inatuletea wateja kwenda bandari ya Dar es Salaam, tunaiambiaje? Kwa hiyo, niishauri sana Serikali, kwa heshima na taadhima, despite ya njia nzuri tuliyoifanya upande wa TARURA, tuangalie namna ya kulea trillion 21 ya mtandao wa barabara za mikoa na barabara kuu pamoja na barabara za wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa data zilizopo, kwa mwaka wa fedha uliopita, barabara kuu na barabara za mikoa na barabara za wilaya zimefanyiwa periodic maintenance kwa asilimia 42 tu. Na ukienda barabara za wilaya ambazo zipo chini ya TARURA, zimefanyiwa maintenance kwa asilimia 28 tu, na asilimia 52 hazijafanyiwa periodic maintenance, kilichofanyika ni just sports improvements na wala hakuna over laying. Nini tunakwenda kufanya? Maana yake tutakuja kuanza afresh kama tusipoamua kutenga fedha kwa ajili ya maintenance ya barabara kuu, barabara za mikoa na barabara za wilaya. Ukiangalia hata barabara ya Kibiti-Lindi-Mtwara ambapo kuna mfanyakazi mkubwa kule Dangote; Dangote anatoa mizigo yake kuleta huku mjini, anakwendaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tuone namna ya kuhakikisha wafanyabiashara wetu wanapokuja Tanzania wanakuwa in a good way ya kufanya biashara na kuwa- attract zaidi ili waje kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba kuunga mkono hoja asilimia 100, nashukuru sana. (Makofi)