Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kuweza kunipa fursa hii ya kuchangia katika hoja ya leo. Sambamba na hilo, natumia fursa hii kumpongeza sana Waziri na Naibu wake pamoja na Kamati zao zote kwa kubwa wanazozifanya. Hakika Watanzania tunajivunia kuwa nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika kulifanya Taifa hili la Tanzania kuwa au kufikia hatua ya kukamilisha ufuataji wa misingi ya Utawala Bora, Haki, Usawa wa Kijinsia katika uwajibikaji, ni lazima tuhakikishe kwamba wananchi wa Taifa hili wananufaika na rasilimali zao sambamba na kutekelezewa mahitaji yao na Serikali yao wanayoitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna masikitiko makubwa mno kwa wastaafu wetu. Wafanyakazi wa Taifa hili wanakuwa na wasiwasi mkubwa sana juu ya mafao yao mara baada ya kustaafu kazi zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa mfano mmoja. Kuna watu wamestaafu kazi toka mwaka 2003, hadi hii leo tunapozungumza bado hawajapatiwa mafao yao ya kustaafu kazi hiyo. Mimi Jimboni kwangu kuna mfano mzuri, kuna watu mwaka 2004 walipewa hadi cheque za kwenda kuchukua malipo yao lakini kufika kule katika Taasisi inayohusika mtu anaambiwa jina la mwisho limekosewa. Kwa mfano, naitwa Simai Hassan Ali, limeandikwa Simai Hassan Ally, ile Y ya mwisho tu. Kitendo cha kurekebisha cheque hiyo mpaka hii leo tuna miaka si chini ya 18 bado kurekebisha cheque haijarekebishwa. Kitendo ambacho kinakuwa kinaleta manung’uniko na masikitiko makubwa kwa wastaafu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo ningependa kuzungumzia suala zima la watu wanaohusika na mitandao. Kuna mapato makubwa sana ambayo Serikali hii tunayaacha. Ni lazima Wizara ya Fedha ipitie tena VAT, lazima wapiti tena hao watu wanaohusika na wanaofanya masuala ya miamala ya kifedha mtandaoni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna vyanzo vingi sana na kuna pesa nyingi sana ambazo sisi tunazipoteza pindi kama tutazisimamia fedha hizo basi tuna uwezo wa kupata hata madawati ya kushughulikia shule zote za nchi hii. Tuna uwezo wa kuendeleza miundombinu mingi tuliyokuwa nayo. Kiukweli kabisa, watoa huduma hizi za kifedha kupitia mitandao kusema ukweli kodi wanayolipa ni tofauti sana na faida wanayoipata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nisingependa kuizungumzia faida yao lakini tuangalie ule uhalisia wa kile ambacho wanakipata kupitia Taifa hili na kile tunachowalipisha sisi. Sisi tunahitaji Bodi kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu. Sambamba na hilo, tunaelewa kwamba Wizara ya Fedha ndiyo Wizara inayosimamia uchumi wa nchi hii chini ya usimamizi wa BoT. Wakati huo huo, BoT ndiyo mhusika mkuu wa thamani ya fedha wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kitu cha kusikitisha BoT wakati inapoweka vigezo vya kiuchumi wanapenda sana kuangalia upande mmoja tu wa Tanzania Bara, hawaangalii sana vile vigezo vinavyotumika kule Tanzania Visiwani. Kwa mfano, Tanzania Bara wanatoa kipaumbele kwenye masuala ya kilimo, mazao kama vile karanga, korosho lakini Tanzania Visiwani tuna mazao ya kimkakati kabisa ambayo ni pekee kabisa. Ukiangalia tuna uzalishaji mkubwa wa karafuu, tuna uzalishaji wa mwani, tuna utalii lakini sasa wakati ambapo hatuvipi tija kupitia BoT, hatuvi-promote vitu hivi kusema ukweli inakuwa inaleta ukakasi na masikitiko makubwa kwa upande wa pili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima tuelewe sisi sote ni nchi moja lakini tuna mifumo miwili. Licha ya kwamba tuna mifumo hiyo miwili tofauti, ila pesa yetu na uchumi wetu unakuwa unasimamiwa na BoT, BoT ni kitu ambacho kinasimamia maslahi ya pande hizi zote mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa katika kusimamia hilo, kama ntakuwa sikosei ni lazima sasa imefikia wakati Wizara ya Fedha ije isimamie vizuri ule mradi unaoitwa JSFC (Joint Sterling Financial Committee) kitu ambacho kinakuwa kinajumuisha taasisi zote za kifedha baina ya Tanzania visiwani na Tanzania Bara. Tutakuwa tunapata ule uwajibikaji wa pamoja na kuondoa malalamiko kwa upande mwingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo ningependa sana nizungumzie suala la microfinance na BoT. Tanzania tuna malalamiko makubwa kwa vijana wetu kwa kukosa ajira lakini kusema kweli matangazo mengine na maagizo mengine yanapokuwa yanatoka wananchi wanakuwa wanaa msikitiko makubwa mno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuchukulie mfano kitendo cha BoT, kwa upande mmoja inawezekana walikuwa sahihi lakini upande mwingine kuzuia haya masuala ya Bureau de Change na kutoa agizo kwamba masuala ya ubadilishaji fedha lazima yafanyike katika Taasisi za Kibenki za Serikali inakuwa ni mtihani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, kuna sehemu nyingine tuna uwezo wa kuzikosesha uchumi wake mkubwa katika halmashauri kwa mfano Halmashauri za Arusha na Visiwa vya Zanzibar. Tunategemea sana mapato yetu kupitia hii Sekta ya Utalii lakini sasa tunapokuwa tunapoziruhusu hizi benki chache kuweza kutoa huduma hizi za ubadilishaji wa fedha inakuwa inaleta ukakasi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Serikali yetu sisi kuna siku za kazi na siku zisizokuwa za kazi. Kwa mfano, siku ya Jumapili hakuna kazi. Sasa inakuwa ngumu kwa mtalii anapokuja hapa kumwambia kwamba anataka kwenda kubadili pesa, kumwambia leo Jumapili hakuna kazi. Kwa maana hiyo, siku hiyo mtalii itabidi alale na njaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo ningependa nizungumzie issue za siri za Kibenki kwa wawekezaji. Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kwa wawekezaji wanaokuja kuwekeza hapa kwamba, Taarifa zao za Kibenki mara nyingi zinakuwa wazi. Serikali mara nyingi kupitia hizi Taasisi za Kibenki wanakuwa wanaziiingilia ndani hizi taarifa za wawekezaji hawa kitu ambacho kinakuwa kinaivunjia sifa na hadhi nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haitakuwa kitu cha busara kwa akaunti za wawekezaji wakubwa, wafanyabiashara maarufu kwamba hata muuza dagaa ana uwezo wa kukuambia akaunti ya mwekezaji fulani ina kiasi gani. Hii inakuwa sio kitu kizuri. Lazima tuwe na utaratibu wa kuhifadhi siri za benki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna nchi kama vile Dubai, Uswiss, wao hata kama Serikali basi inapokwenda kudai documents kwa masuala ya makampuni makubwa yanayowekeza katika nchi ile inakuwa ni shida kupewa kwa sababu wameingia makubaliano na makubaliano hayo ni ya kimkataba yanaongozwa na siri. Maana yake ni kuwa Benki ni issue ya siri kwa kuzingatia tu kwamba pesa hizo zinazokuwa zimo humo zitatumika kwa maslahi ya Taifa na kwa utaratibu ambao haukiuki misingi ya nchi husika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo kuna tatizo jingine hapa. Imefikia hatua kwamba Tanzania kweli tunataka mpaato ya nchi yetu kwa ajili ya kuongeza mishahara kwa wafanyakazi…

SPIKA: (Kicheko)

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.