Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa pongezi kwa jitihada na matarajio makubwa ya nchi kuwa na Viwanda na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Watendaji wote walioteuliwa nae, kwa kasi yenye uchungu wa maendeleo ya wananchi wa Tanzania kwa kuwapatia ufumbuzi wa changamoto zinazowakabili.
Madhumuni ya kuanzisha SIDO ni kuwezesha kutoa ushauri na mafunzo kwa vijana wetu wajasiriamali kuboresha uwezo wa kujiajiri kwao. Lakini Mkoa wa Rukwa kuna mapungufu ambayo yamekwamisha utekelezaji wa ufanisi na wenye tija wa SIDO kwa vijana na wajasiriamali wetu.
Majengo yapo, mashine zilizokuwepo hazipo kwa sasa, ambazo zilitoa ajira na mafunzo kutokana na hali hiyo majengo yamepangishwa kwa wafanyabiashara wa mashine za kukoboa mpunga na kusaga unga. Naomba Serikali kufuatilia majengo hayo na kurejesha mashine zilizokuwepo ili kufufua SIDO madhumuni yake kwa vijana na wajasiriamali wengi wao ni kina Mama.
Mapungufu yafanyikayo SIDO-Rukwa, kwa namna watoavyo mafunzo kwa vijana wetu na wajasiriamali kwa kufanya mchango kutoka kwa washiriki hao ndiyo wafanye maandalizi ya mafunzo. Inakatisha tamaa na mafunzo hupatikana kwa wachache. Serikali ipange fungu maalum la kuendesha mafunzo kwani watalamu wapo bila ya kufanya hivyo watakuwa wanapata mishahara bure.
Serikali kuona umuhimu kwa Mkoa wa Rukwa kufufua SIDO kwa kuhakikisha majengo yake yanarejeshewa mashine zake na vijana, akina mama wajasiriamali waweze kufaidika na uwepo na SIDO Nchini
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Rukwa wapo vijana wa kutosha wanaomaliza elimu ya msingi na Sekondari wanakosa elimu ya kujiajiri, wanajishirikisha kwenye Ujasiriamali pasipo na uwelewa wa kuanzisha viwanda vidogo vidogo. Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wametenga eneo la kujenga chuo cha VETA lakini hakuna kinachoendelea. Ni vema Serikali ikaona umuhimu wa kujenga Chuo hiki kwa maslahi ya Mkoa wa Rukwa.
Mheshimiwa Waziri napenda kupata utaratibu na mikakati ya kufufua SIDO-Rukwa na ujenzi wa VETA-Rukwa katika kutukwamua huku pembezoni ambako hakuna hata viwanda vya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.