Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia kwa kupongeza hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Ningependa kujua sababu ambazo zimefanya kiwanda cha Chai-DABAGA kutofanya kazi sasa ni miaka zaidi ya 15 wakati wananchi wanalazimishwa kulima chai, nitaomba ufafanuzi.
Ningependa nijue hadi sasa Serikali imejipanga vipi kuwawezesha wazawa zaidi kupunguza ukiritimba ili waweze kujenga viwanda vya matunda na nyanya katika sehemu za Ilula ambako nyanya nyingi zinapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Iringa kiwanda cha usagishaji cha N.M.C kilichopo Iringa Mjini kimekuwa kikifanya kazi kwa kusuasua. Ninaomba Mheshimiwa Waziri wewe mwenyewe ufike Iringa na utembelee Kiwanda cha Chai-DABAGA-Kilolo na Kiwanda cha usagishaji ili uone hali iliyopo pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Waziri na Wizara yake wawasaidie wananchi, wakulima kuona uwezekano wa kuleta sheria ambayo itamsaidia mkulima kuweza kuuza mazao yao sokoni na kwa kutumia mizani na siyo lumbesa. Tumeshuhudia hata viwanda vimekuwa vikinunua mazao ya wakulima kwa bei ndogo tena bila kutumia mizani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Waziri amtembelee Mtanzania Mzee Sallawa George aliyegundua jinsi ya kutengeneza Ulanzi na kuweka kwenye chupa bila kuharibika. Ninaomba Wizara yako imsaidie ili utaalamu wake usipotee. Wenzetu wa Kenya wanatengeneza juice ya Ulanzi, Bamboo Juice na mimi nitakuwa tayari kumuwezesha Mtanzania huyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.