Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri yafuatayo: kwanza, kutambua na kutangaza vivutio vya utalii tulivyonavyo kwenye maeneo mbalimbali. Mfano, Wilayani Ukerewe kuna mapango ya Handebezyo, jiwe linalocheza la Nyaburebeka (Ukara), beach ya Rubya na kadhalika, lakini bado havitangazwi kama inavyostahili na hatimaye viliingizie Taifa letu pesa na kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kuwekeza kwenye miundombinu inayozunguka vivutio vya utalii. Mfano, vivutio nilivyovitaja hapo juu kwa sababu ya kukosa uwekezaji na maeneo haya hayafikiki. Kwa, hiyo nashauri Wizara ishirikiane na Halmashauri kujenga barabara na njia za kufikia vivutio hivi hasa Wilayani Ukerewe ambako vivutio hivi havifikiki.