Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja ya hotuba ya Waziri wa Maliasili na Utalii kwa kumpongeza sana Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni yangu kwa Wizara, naomba utalii wa ndani uimarishwe kwa kufanya promotion au ku-promote utalii wa ndani na hasa kuimarisha cultural heritages site zetu. Watalii wa ndani waje waone Makumbusho zetu na maeneo mentioned ya urithi wa Utamaduni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu mwingine, Serikali sasa ijipange kuhakikisha wanaanzisha Plantation Museums ambazo zitasaidia watoto wetu kujifunza. Tunakoelekea, wanafunzi wa mijini hawatakuwa na sehemu ya kujifunza kwa vitendo na kwa kuona uhalisia wa mazao mbalimbali

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.