Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia nzima inatafuta ahueni kwenye sekta ya utalii katika kipindi hiki cha Corona, lakini Tanzania tunaongeza tozo mfano kuanzia Julai, 2021 Park Fees zitaongezeka kwa 10 USD kwa Serengeti na Nyerere kipindi cha high season wakati Kenya, Uganda na Rwanda wamepunguza. TANAPA pia pamoja na uwekezaji ndani ya hifadhi kulipiwa Concession fee ya 50 USD bado wanaanzisha Land Base Rent ya 2000 USD kwa Seasonal Camps, Permanent Tented Camps 20,000 USD na Lodges 50,000 USD. Suala hili linaongeza gharama za utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA wana hifadhi 22 ila hifadhi zinazoweza kujiendesha ni hifadhi zisizozidi tano na ndiyo maana kila mara wanaongeza tozo na kuongeza mzigo kwa hifadhi kama Serengeti, Nyerere na KINAPA. Nashauri tozo hizi zisitishwe hadi Julai, 2022 ili kutoa ahueni kwenye sekta ya utalii kipindi cha corona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tozo kama ukikodisha gari ya utalii kwa kampuni nyingine pamoja na kulipa TRA pia inabidi ulipe 50 USD Wizara ya Maliasili na Utalii. Hii ni kuongeza gharama za kufanya biashara Tanzania. Nashauri tozo hii iangaliwe upya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu TDL, fedha hizi nashauri ziwekwe kwenye akaunti maalum na zifanye kazi iliyokusudiwa kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gharama za kupima Corona ni kubwa nchini Tanzania ambayo ni 100 USD wakati Kenya ni 30 USD Serikalini na 50 USD kwa Hospital binafsi. Gharama hizi ziangaliwe upya. Rapid test kote ni sawa kwa maana ya 25 USD.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Fedha ikae na bank na BOT ili kuangalia uwezekano wa kutoa ahueni kwa wadau wa utalii ambao walikopeshwa magari ya utalii na kushindwa kulipa kwa sababu ya Corona ili deni lao lisogezwe mbele bila penalty kama sehemu ya kutoa ahueni kwenye sekta ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawasilisha.