Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuchangia katika bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Awali ya yote nawapongeza sana Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya na Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri nawashukuru kwa ushirikiano mzuri wanaonipatia kila mara tunapokuwa na changamoto, lakini pia nawapongeza wameanza vizuri, kasi yao ni nzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza pia, Dkt. Kijazi kwa kazi nzuri, wananchi wa Serengeti wanatambua kazi yake pia. Nampongeza Mhifadhi Mkuu wa Serengeti National Park, Ndugu yetu Mwishawa anafanya kazi nzuri. Nadhani wote wamesikia hifadhi ile sasa imekuwa ya kwanza mara mbili mfululizo katika kuwa hifadhi bora Afrika, nawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka siku moja Dkt. Bashiru alishauri Bunge hili ni vizuri likaweka record kuwa limeweza kusaidia ku-transform kilimo. Nishauri pia katika nchi yetu maeneo mawili pekee ambayo tunaweza tuka-compete kiuchumi ni kilimo na utalii tu, kwa sababu tunazo rasilimali nyingi sana katika eneo hili la utalii. Kwa hiyo niombe Serikali kwa safari hii tuwekeze sana katika utalii. Wabunge wenzangu wengi wamechangia kuwa bado performance yetu si nzuri uki-compare na rasilimali tulizonazo, lakini nikiangalia si kwamba kwa sababu Wizara haifanyi kazi, hawatendi kazi, no naangalia ni how much tuna-invest katika sekta hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Wizara sasa ijielekeze core business yake iwe ni biashara ya utalii, siyo kwenye uhifadhi tu na tutoe fedha nyingi tu invest sana katika marketing. Marketing ina mambo mengi sana, ina watu wanaofanya kazi, product zetu, service delivery, miundombinu na vitu vingi sana. Kwa hiyo tujielekeze huko tunaweza tuka-transform sekta hii na kuifanya nchi yetu ifanye vizuri kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la pili, ningeomba Wizara hii pamoja na jitihada nzuri wanazozifanya, sasa waongeze kasi kwenye kutatua matatizo au migogoro iliyopo kati ya hifadhi pamoja na wananchi. Simba na tembo wameendelea kuua sana wananchi katika Jimbo langu la Serengeti. Najua jitihada zipo, lakini naomba ziongezwe na niombe sana Wizara hii ni vizuri sasa wale askari wa wanyamapori wa-shift focus yao, pengine wasikae kule ndani ya hifadhi, zamani wananchi walikuwa hawana awareness, sasa hivi hawaendi kuwinda.

Mheshimiwa Naibu Spika, niombe sasa wale askari hata wangewajengea nyumba waishi huku vijijini, wapewe pia magari ili kwamba tembo anapoingia wawe huko, kuwapigia wale watu simu usiku ni ngumu. Sasa hivi ninapoongea ukienda Kata za Issenye, Natta, Nagusi ukienda Ikoma, Machochwe, kule Merenga, watu wanakaa usiku kucha wakilinda tembo wasiingie na wakati huo hawana silaha wala hawana magari. Kwa hiyo, niiombe sana Wizara, waende sasa wawahamishe wale askari, sasa hivi watu hawawindi, wakae huku ili waweze kutusaidia kufukuza tembo wakati wa usiku.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna tatizo la mipaka, kuna vijiji saba mpaka sasa mipaka ile haijawa solved. Niombe sana mipaka ile waende kutatua hili tatizo, ni la muda mrefu na wananchi walifungua kesi, wakashinda. Niombe vile Vijiji vya Mbirikiri, Bonchugu, Sedeco viweze kusaidiwa ili viweze kuondokana na tatizo hili, limekuwa ni la muda mrefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia suala hili la kutaifisha mifugo mbona toka wameendelea kutaifisha bado watu wanaingiza tu. Kwa hiyo unaweza ukaona kuwa, hii sheria haiwezi ku-work, ni vizuri sasa suala hili la uhifadhi tuwashirikishe sana wananchi. Tuwashirikishe kwa kiwango kikubwa, nafikiri tunaweza tukatatua tatizo hili na likaisha kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu, niiombe Wizara hii iangalie namna ya kuongeza namna ya wananchi kufaidika zaidi na utalii. Hapa nishauri eneo moja tu, hizi hoteli za kitalii ni vizuri sasa Wizara itafute namna ya kuboresha sera, zijengwe katika vijiji vya jirani ili wananchi waweze ku-trade kwa urahisi na hoteli hizi, lakini pia uwepo wa hoteli hizi katika vijiji vinavyozunguka hifadhi itaongeza ile spirit ya kuhifadhi hifadhi zetu pamoja na ku-change ile mind set yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe sana Wizara tuende kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika kuona tunatengeneza miundombinu mizuri kule ndani ya hifadhi na katika vijiji ambavyo vinazunguka hifadhi. Leo wananchi wengi ukiwaambia hizi hifadhi zina maana zinaweza kusaidia nchi, hawaoni maana yake. Unamuuliza mwananchi kwa nini aendelee kuingiza ng’ombe ndani? Kwa nini aingie ndani ya pori kuwinda? Yeye anaona akiingia yeye binafsi anapata faida kubwa kuliko faida ambayo anasikia kwamba Taifa linapata, lakini tukimsaidia, akaona shule zinajengwa, barabara zinajengwa, vituo vya afya vinaboreshwa, anaweza kuelewa na akawa mtu namba moja katika kuhifadhi maliasili zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)